Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,662
MTUNZI : NYEMO CHILONGANI
NAJISIKIA nimechoka sana, nimechoka sana kwa sababu nilikuwa nimetoka kucheza mpira uwanjani huku nikiwa nimechafuka kupita kawaida.
Ninapofika nyumbani, ninaoga na kisha kuchukua simu yangu kwa ajili ya kuangalia updates za facebook, sikukuta hata meseji moja zaidi ya notification tu, tena wala hazikuwa nyingi. Nilichokifanya ni kuanza kuzugazuga hapa na pale na kisha kutulia. Mara ghafla nikaona namba moja nyekundu kwenye sehemu ya meseji, kulikuwa na meseji imeingia, nilichokifanya, nikaifungua na kuanza kuchati na mtu huyo huyo.
EDUADO: Mambo vipi Shahruk Khan.
MIMI: Hahaha! Poa. Inakuwaje wewe mtu?
EDUADO: Kama kawa. Nilikuwa nakusubiri sana hewani. Nilikuwa na mzuka na wewe ile mbaya.
MIMI: Duh! Mzuka na mimi! Kuna nini tena?
EDUADO: Kuna bonge la kazi hapa. Unataka?
MIMI: Kwa nini nisitake? Nipe mawasiliano yao niandike barua ya kuomba kazi fasta.
EDUADO: Hahahaha! Kaka unakosea. Niliposema kazi sikumaanisha hiyo.
MIMI: Wewe ulimaanisha ipi sasa?
EDUADO: Kazi moja hivi. Kazi ambayo watu wengi wameishindwa hasa masharobaro.
MIMI: Hahahaha! Itakuwa kubeba zege hiyo watoto wa mama hawaiwezi. Mimi naiweza, hebu niambie ni jengo gani?
EDUADO: Siyo kazi ya kubeba zege. Kuna mtu nataka umfanyie kazi.
MIMI: Mtu gani?
EDUADO: Kuna mrembo fulani nipo naye hapa UDSM ni mkali ile mbaya. Yaani mkali mpaka nashindwa kusema ukali wake unafanana na nini.
MIMI: Hebu acha masihara kaka. Kwa hiyo kama mkali mimi nifanye nini?
EDUADO: Huyu mrembo anaringa mbaya. Yaani mrembo ananata utafikiri akanyagi ardhi hii tunayochimbia vyoo.
MIMI: Oke! Wazuri wapo wengi na hata wenye maringo wapo wengi pia. Hebu niambie kuhusu huyo. Kwanza anaitwa nani? Nipe maelezo ya kujitosheleza na siyo naanza kumtengeneza mrembo mkali kichwani mwangu ikawa ndivyo sivyo.
EDUADO: Huyu mrembo anaitwa Aziza Moddy, anaishi Msasani, baba yake ni mfanyabiashara mkubwa sana aisee. Ni mrembo fulani pini…yaani ni pini sana.
MIMI: Hebu acha masihara. Sasa inakuwaje watoto wa kisharobaro wamemshindwa?
EDUADO: Huyu mrembo hafagilii muonekano, ni mrembo fulani ambaye anapenda mtu amfuate kama jinsi alivyo. Yaani kama wewe ni mtu wa chini, mfuate hivyohivyo ila tatizo watoto wa hapa chuo wanapenda kumfuata kisharobaro kaka.
MIMI: Dah! Kwa hiyo kazi unayotaka kunipa ni ipi?
EDUADO: Umchukue huyu mtoto. Yaani ukifanikiwa, moyo wangu utakuwa mweupeee kama theluji.
MIMI: Hahaha! Usitake kunichekesha Eduado, hivi unamkumbuka Sikitu?
EDUADO: Sikitu yupi?
MIMI: Si yule mrembo wa mwaka jana ambaye ulikuwa unamsifia sanaaa kwamba mkali kumbe wala hakuwa mkali kama ulivyokuwa ukimsifia, mbaya zaidi alikuwa anakaa mbali, Musomaaa.
EDUADO: Achana na hayo, yule msahau kwani mimi mwenyewe alinitumia picha ambayo siyo yake. Ila kaka kiukweli Aziza ni mrembo mmoja mkali sana. Hapa chuo amekuwa gumzo kila kona, vijana wengi wamechemka.
MIMI: Sasa kama wengine wamechemka mimi nitaweza vipi?
EDUADO: Hahahaha! Kaka ninakuamini sanaaa, wewe mtu unaweza sana kuongea, unaweza sana kuandika. Endapo nitakupa kazi hii na ukishindwa, hakika nitajua kweli duniani kuna wasichana wagumu.
MIMI: Kwa hiyo kazi yako ina malipo au?
EDUADO: Ikitokea umempata, nitakupa zawadi kaka. Yaani ninachokitaka huyu mrembo umchukue tu, basiii. Anaringa sana, ananata sana, yaani sijui niseme vipi.
MIMI: Ila si anaringa kwa sababu mzuri?
EDUADO: Ndiyo. Ila yeye kazidi.
MIMI: Ila kwa sasa aisee nahisi nimepoteza kumbukumbu zangu za kuongea na hawa watoto wa kike, sijui kama nitaweza.
EDUADO: Acha kunitania kaka. Nakuamini sana kwamba unaweza kuliko mtu yeyote na ndiyo maana nikakufuata wewe. Hivi haujiulizi kwa nini sikumfuata Thomas? Thomas kwenye kuongea mkali sana ila kwenye kuandika hakuna kitu, ila wewe, aisee una kipaji kila kona, sidhani kama kuna demu ambaye utamtokea asikukubali!
MIMI: Hahaha! Hebu acha kunipamba. Hebu niambie, huyo mrembo yupo Facebook?
EDUADO: Amejaa teleee…yaani kajaa teleee. Anajiita Aziza M Aziza. Ni mrembo mkali sana. Hebu mcheki kwanza.
MIMI: Sawa.
Sikutaka kuchelewa, tayari kichwa changu kikaanza kujazwa na sura nyingi za wasichana wazuri huku nikianza kuzigawanya kimakundi kwamba huyu alikuwa Aziza mwenyewe huyu hakuwa mwenyewe. Nilikuwa namfahamu Eduado tangu tukiwa sekondari alipokuwa akisema msichana fulani ni mzuri, mzuri kweli japokuwa kwa Sikitu alikuwa ameniingiza choo cha kike.
Itaendelea
NAJISIKIA nimechoka sana, nimechoka sana kwa sababu nilikuwa nimetoka kucheza mpira uwanjani huku nikiwa nimechafuka kupita kawaida.
Ninapofika nyumbani, ninaoga na kisha kuchukua simu yangu kwa ajili ya kuangalia updates za facebook, sikukuta hata meseji moja zaidi ya notification tu, tena wala hazikuwa nyingi. Nilichokifanya ni kuanza kuzugazuga hapa na pale na kisha kutulia. Mara ghafla nikaona namba moja nyekundu kwenye sehemu ya meseji, kulikuwa na meseji imeingia, nilichokifanya, nikaifungua na kuanza kuchati na mtu huyo huyo.
EDUADO: Mambo vipi Shahruk Khan.
MIMI: Hahaha! Poa. Inakuwaje wewe mtu?
EDUADO: Kama kawa. Nilikuwa nakusubiri sana hewani. Nilikuwa na mzuka na wewe ile mbaya.
MIMI: Duh! Mzuka na mimi! Kuna nini tena?
EDUADO: Kuna bonge la kazi hapa. Unataka?
MIMI: Kwa nini nisitake? Nipe mawasiliano yao niandike barua ya kuomba kazi fasta.
EDUADO: Hahahaha! Kaka unakosea. Niliposema kazi sikumaanisha hiyo.
MIMI: Wewe ulimaanisha ipi sasa?
EDUADO: Kazi moja hivi. Kazi ambayo watu wengi wameishindwa hasa masharobaro.
MIMI: Hahahaha! Itakuwa kubeba zege hiyo watoto wa mama hawaiwezi. Mimi naiweza, hebu niambie ni jengo gani?
EDUADO: Siyo kazi ya kubeba zege. Kuna mtu nataka umfanyie kazi.
MIMI: Mtu gani?
EDUADO: Kuna mrembo fulani nipo naye hapa UDSM ni mkali ile mbaya. Yaani mkali mpaka nashindwa kusema ukali wake unafanana na nini.
MIMI: Hebu acha masihara kaka. Kwa hiyo kama mkali mimi nifanye nini?
EDUADO: Huyu mrembo anaringa mbaya. Yaani mrembo ananata utafikiri akanyagi ardhi hii tunayochimbia vyoo.
MIMI: Oke! Wazuri wapo wengi na hata wenye maringo wapo wengi pia. Hebu niambie kuhusu huyo. Kwanza anaitwa nani? Nipe maelezo ya kujitosheleza na siyo naanza kumtengeneza mrembo mkali kichwani mwangu ikawa ndivyo sivyo.
EDUADO: Huyu mrembo anaitwa Aziza Moddy, anaishi Msasani, baba yake ni mfanyabiashara mkubwa sana aisee. Ni mrembo fulani pini…yaani ni pini sana.
MIMI: Hebu acha masihara. Sasa inakuwaje watoto wa kisharobaro wamemshindwa?
EDUADO: Huyu mrembo hafagilii muonekano, ni mrembo fulani ambaye anapenda mtu amfuate kama jinsi alivyo. Yaani kama wewe ni mtu wa chini, mfuate hivyohivyo ila tatizo watoto wa hapa chuo wanapenda kumfuata kisharobaro kaka.
MIMI: Dah! Kwa hiyo kazi unayotaka kunipa ni ipi?
EDUADO: Umchukue huyu mtoto. Yaani ukifanikiwa, moyo wangu utakuwa mweupeee kama theluji.
MIMI: Hahaha! Usitake kunichekesha Eduado, hivi unamkumbuka Sikitu?
EDUADO: Sikitu yupi?
MIMI: Si yule mrembo wa mwaka jana ambaye ulikuwa unamsifia sanaaa kwamba mkali kumbe wala hakuwa mkali kama ulivyokuwa ukimsifia, mbaya zaidi alikuwa anakaa mbali, Musomaaa.
EDUADO: Achana na hayo, yule msahau kwani mimi mwenyewe alinitumia picha ambayo siyo yake. Ila kaka kiukweli Aziza ni mrembo mmoja mkali sana. Hapa chuo amekuwa gumzo kila kona, vijana wengi wamechemka.
MIMI: Sasa kama wengine wamechemka mimi nitaweza vipi?
EDUADO: Hahahaha! Kaka ninakuamini sanaaa, wewe mtu unaweza sana kuongea, unaweza sana kuandika. Endapo nitakupa kazi hii na ukishindwa, hakika nitajua kweli duniani kuna wasichana wagumu.
MIMI: Kwa hiyo kazi yako ina malipo au?
EDUADO: Ikitokea umempata, nitakupa zawadi kaka. Yaani ninachokitaka huyu mrembo umchukue tu, basiii. Anaringa sana, ananata sana, yaani sijui niseme vipi.
MIMI: Ila si anaringa kwa sababu mzuri?
EDUADO: Ndiyo. Ila yeye kazidi.
MIMI: Ila kwa sasa aisee nahisi nimepoteza kumbukumbu zangu za kuongea na hawa watoto wa kike, sijui kama nitaweza.
EDUADO: Acha kunitania kaka. Nakuamini sana kwamba unaweza kuliko mtu yeyote na ndiyo maana nikakufuata wewe. Hivi haujiulizi kwa nini sikumfuata Thomas? Thomas kwenye kuongea mkali sana ila kwenye kuandika hakuna kitu, ila wewe, aisee una kipaji kila kona, sidhani kama kuna demu ambaye utamtokea asikukubali!
MIMI: Hahaha! Hebu acha kunipamba. Hebu niambie, huyo mrembo yupo Facebook?
EDUADO: Amejaa teleee…yaani kajaa teleee. Anajiita Aziza M Aziza. Ni mrembo mkali sana. Hebu mcheki kwanza.
MIMI: Sawa.
Sikutaka kuchelewa, tayari kichwa changu kikaanza kujazwa na sura nyingi za wasichana wazuri huku nikianza kuzigawanya kimakundi kwamba huyu alikuwa Aziza mwenyewe huyu hakuwa mwenyewe. Nilikuwa namfahamu Eduado tangu tukiwa sekondari alipokuwa akisema msichana fulani ni mzuri, mzuri kweli japokuwa kwa Sikitu alikuwa ameniingiza choo cha kike.
Itaendelea