Wakati Serikali ya Iran ilipozima intaneti na kuanza kuwamiminia risasi wananchi wa Iran waliokuwa wakidai haki zao, tukio hili halkupewa uzito, waliofyatliwa risasi walilaaniwa na hata kusingiziwa ni raia wa kigeni kutoka Israel na Marekani, wakachukuliwa kama wahaini wa taifa, wakati wale waliokuwa wanawamiminia risasi wakionekana kama mashujaa. Kilio cha wale waliokufa kilionekana kama 'propaganda tu,' huku vifo vikitetewa kama ‘collateral damage.’ taarifa ya vifo hata zilipoonesha idadi kubwa, wengine wakasema "kitakwimu" watu elfu 30 hawafikii hata asilimia moja ya idadi ya waoran, kwahio hakuna shida kabisa.’ Yote haya yalikuwa ni jitihada za kuwa upande wa Serikali ya Iran, kwa sababu... siyo siri, chuki dhidi ya Marekani na Israel ilikuwa kubwa zaidi kuliko haki za binadamu."
Sasa, leo, Marekani na Israel wameamka na kujivika vyeo vya 'wakombozi wa Iran kwa kuwaua viogozi walioratibu mauaji hayo akiwemo mkuu wa jeshi, mkuu wa usalama wa taifa, na inasemekana hadi kiongozi mkuu Ayatolla wamepita naye lakini ghafla watu wanageuka na kuwa upande wa kuwaonea huruma wananchi wa Iran ambao wengi kiuhalisia hawataki huruma ya watu waliowabeza kipindi wanauawa na kwa sasa wanafurahia sana kinachoendelea.
Katika operseheni zinazoendelea kuwaua viongozi wakuu wa serikali na jeshi la Iran, pale inapotokea athari zimewapata raia mfano kuna vifo vya watu watatu raia wa kawaida tunaona habari hizi zikipewa ukubwa sana, lakini walipouliwa zaidi ya wananchi elfu 30 walikuwa wapi ? ilikuwa ni sawa tu ila ghafla sio sawa ?