Kisa cha Sindbad baharia na safari saba

Kisa cha Sindbad baharia na safari saba

SEHEMU 11
Baada ya maakuli ya jioni, Sindbad Baharia akampa Hindbad Hamali Reale mia za dhahabu ambazo Hindbad Hamali alizipokea kwa shukran na dua nyingi; akatoka, akaelekea kwake huku akizidi kustaajabu kwa yale alioyasikia kutoka kwa Sindbad.
Siku ya tatu, Hindbad Hamali, baada ya swala ya adhuhuri alielekea tena kwa mkarimu wake aliempokea tena mikono miwili, akataka aketi karibu yake wageni wengine walipofika Sindbad Baharia alianza kuwasimulia yaliompata katika safari yake ya tatu.
SAFARI YAKE YA TATU
Mjue, sahibu zangu, alianza Sindbad Baharia, kwamba baada ya kurejea kwetu kutoka katika ile safari yangu ya pili, nikawa kama nilivyowasimulia, naishi katika maisha furaha, raha na starehe nyingi. Lakini baada ya muda nikachoshwa tena na yale maisha ya kukaa katika jiji LA Baghdad nikila na kulala tu bila kufanya kazi yoyote.
Basi kwa mara nyengine tena niliingiwa na hamu ya kusafiri kufanya biashara na kuuona ulimwengu.
Bila kujali yale yalionikuata awali, nilianza kujitayarisha tena kwa safari yangu ya tatu. Basi nikanunua bidhaa nyingi mbali mbali nikasafiri kwenye mto Tigris mpaka basrah ambako nilijiunga na wafanya biashara wengine. Tupanda merkeb kuelekea baharini.
Safari yetu ilianza vizuri kwani tulisafiri kwa upepeo mzuri bila matatizo yoyote, tukawasili katika bandari tofauti za kigeni, tukifanya biashara ya kununua na kuuza bidhaa zetu kwa faida kubwa bila tatizo lolote.
Siki kuja, walakin, wakati tulipokua tukisafiri katikati ya bahari kuu, mara dhoruba kali ikavuma na upepo wenye nguvu ulituchukua kutoka katika mkondo wetu, ukatupeleka mbali kusikojulikana.
Baada ya muda tukamsikia nadhodha wetu ambae alikua kwenye omo akiangalia upeo wa macho, akapiga mayowe! Alikua akijipiga ngumi za usoni na kifuani huku akinyofoa ndevu na kuzichana nguo zake.
"Tumeangamia" alikua akipiga makelele, "upepo umetuchukua mbali na kutuelekeza kwenye kile kisiwa kwenye upeo wa macho, hicho ni kisiwa kinachojulikana kwa kina la Zughb ambako wanaishi viumbe mbilikimo waliofanana zaid na amanyani kuliko wanadadu, ma ambako hakuna msafiri yeyote aliewahi kufika huko na akaokoka Salama!"
Upepo ulipotufikisha karibu na like kisiwa, mara vile viumbe alivyovitaja nahodha wetu vikajazana pwani, vikaanza kuogelea kutuelekea. Baada ya muda mfupi, kwa wingi wa nzige vikapanda merkebuni mwetu vilikua vifupi vyenye sura mbaya ya kutisha.
Na vyenye macho madogo yenye rangi ya manjano na mwili uliojaa manyoya. Vilika vingi kama utitiri! Hapo nahodha akatuhadharisha na kutuonya tusijaribu kuvishambulia wala kuviudhi, visije vikatuvamia na kutuangamiza!
Vilipojazana merkebuni mwetu vilipanda kwenye mlingoti, vikashusha tanga halafu vikashika usukani na kuiongoza merkebu yetu mpaka kisiwani ambako vilituteremsha mmoja mmoja, halafu vikarejea merkebuni vikatweka tanga vikatoweka na merkebu yetu.
Basi tukawa hatuna la kufanya ispokua kumshukuru mungu kwa kuokoka kwetu, pale kisiwani tukaanza kusaka kitu cha kula na Maji ya kunywa. Kwa bahati nzuri tuliona mito mingi na miti iliojaa matunda ya kutosha, hapo tukaoga tukapumzika tukila matunda tulioyachuma.
Tulipopumua tilianza kutembea tembea pale kisiwani mpaka katikati ya miti mikubwa, mbali na pale tulipokua tiliona jumba moja kubwa sana ambako tulitumaini kuupitisha Salama ule usiku.
Walakini, tulipokaribia tulistaajabu kuona ukubwa wa lango lake lililikua wazi. Bila kisita sita tukaingia ndani-lakini kwa hadhari kubwa - tukitumaini kukitana na watu, lakini tulistaajabu kuona hamna hata mtu mmoja.
Uwani kwenye pembe moja tukaona rundo la mifupa na kwa upande wa pili tukaona bao kubwa refu kupita kiasi. Karibu yake palikua na tanuri kubwa, masufuria, vikaangio vikubwa na nondo ndefu sana zenye ncha kali.
Kwa kua tulikua tumechoka kupita kiasi tukajibwaga pale ukumbini bila kujali tukalala kidogo. Kulipokuchwa mara tuliamshwa na kishindo kikubwa kama ngurumo, ardhi ilianza kutetemeka na ghafla lilelango lilianza kufunguka likaingia jitu kubwa, refu kama mnazi tena jeusi kama makaa, lenye jicho moja jeupe utosini! Domo lake kubwa la chini lilikua likining'inia mithili ya la ngamia, na maskio yake mapana yaliofika mabegani yalifanana na ya tembo, na kucha zake kali kama za simba zilijitokeza.
Kuliona tu, sote tukazimia kwa woga tukabaki pale kama wafu. Tulipopata fahamu tukalikodolea macho kwa khofu, wakati lenyewe likiranda randa huko na huko mle uani, mwisho lilikaa kwenye lile bao, likatuangalia kwa muda bila kutoa sauti yoyote, ghafla lilinyanyuka likaelekea kwangu, likanishika shingoni likaninyanyua juu likaanza kunikagua mwili mzima kwa kunitomasa tomasa na kunibonyeza bonyeza kwa dole lake kama mtu amkaguavyo kondoo atakae mchinja.
Lilipoona nimekonda kijiti na ni mifupa tu, lilinibwaga chini likaanza kuwakagua wenzangu mmoja mmoja mpaka likamfikia nahodha wetu ambae alikua mrefu tena mnene mwenye mabega mapana. Lile jitu likavutiwa naye likamshika kama mchinjaji amshikavyo kondoo atakae Mchinja,
Likamvunja shingo kwa guu lake; halafu likachukua moja ya zile nondo zilizokua na ncha kali likamchoma nalo kutoka nyuma hadi kinyani.
Itaendelea.
 
SEHEMU 9
Nilipoingia ndani nilikiziba kile kiingilio kwa jiwe kubwa nikifikiri labda humo nitasalimika usiku ule na kwamba, kukicha mwenyezimungu anajua yatakayo tokea.
Lakini kabla sijachukua hatua chache baada ya kuingia mle pangoni nikaona, mbali na pale nilipokua kwenye ukingo wa pili wa lile pango joka kubwa limejikunja linatamia mayai yake! Kuona vile nywele zikanisimama wima, na kwa woga mkubwa niliokua nao nikashindwa kujongea popote,
Kwa kukosa njia nyengine yoyote ya kujisalimisha, walakin nilimwamini mungu kwani mwamini mungu si mtovu, nikabaki pale pale nilipokua; nikiwa macho usiku kucha, kulipokucha nililisukuma lile jiwe nikatoka mle pangoni nikipepesuka kama mlevi kwa uchovu na usingizi.
Wakati nilipokua nikipepesuka vile pale bondeni mara niliona mzoga mkubwa wa mnyama mbichi limeporomoka kutoka juu, nilipolikagua niligundua kuwa alikua ni kondoo mkubwa aliyechunwa ngozi, nilizidi kushangaa kwa kioja kile kwani hapakuwa na binadamu yeyote pale.
Ndipo nikakumbuka hadithi niliyoisikia zamani kutoka kwa wasafiri waliofika kwenye mlima almasi na jinsi watu wanavyojipatia almasi kutoka katika bonde hilo lisilofikika kwa kutupa mizoga ya kondoo kutoka juu ili almasi zinate kwenye mizoga hiyo inapoiangukia.
Ifikapo mchana madege makubwa kama vile Rok au tai wakubwa hushuka kwa kasi na kuinyakua mizoga na kuruka nayo mlimani kwenye viota vyao. Hapo ndipo wafanyabiashara walioitupa ile mizoga hutokea na kuyapigia makeleke, na madege huiacha mizoga hiyo na kuruka.
Hapo wafanya biashara huikagua na kugoboa almasi zilizo nata na kuyaachia madege mizoga yao. Nilipokumbuka hadhithi hiyo fikira zilinijia. Lakini kwanza nilikusanya almasi nyingi nzuri, safi tena zathamani.
Nikazitia kibindoni nyingine nikazijaza mifukoni na kila palipokua na nafasi ya kuzihifadhi, halafu nikachukua kilemba changu nikakijaza almasi pia halafu nikakikunja vizuri, nikajilaza chini yamzoga mmoja mkubwa, muda si mrefu mara nikanyakuliwa kwa makucha makubwa ya ndege yalioushika imara ule mzoga.
Lile dege lilipaa nami juu kwa juu mpaka baada ya muda likatua juu ya kilele cha mlima. Lilipotua tu lilianza kuurarua ule mzoga. Mara palisikika sauti za makelele ya watu kutoka nyuma ya jabali lililokua karibu.
Lile dege lilishtuka likaruka likauacha ule mzoga, hapo bila kuchelewa nilijifungua nikasimama nikiwa nimejaa damu. Mara akatokea mwanamume mmoja akakimbilia pale palipokua na ule mzoga.
Lakini aliponiona alisimama ghfla bila kutamka neno lolote aliinama. Akaanza kuukagua ule mzoga huku mara kwa mara akinitupia macho kwa was wasi.
Alipoona hakuna almasi yoyote akanyoosha mikono juu akapiga kelele: "O mwenyez mungu wangu menye uwezo na rehema tuepushe na balaa la masheitwaan na majinni yaliyotapakaa note!"
Kabla sijamweleza jinsi nilivyofika pake, yule bwana huku akitetemeka kwa khofu akanigeukia akaniuliza: "wewe ni nani na imekuaje uko hapa?"
Itaendelea...
Yani nasubiri kwa hamu
 
KISA CHA SINDBAD BAHARIA

SEHEMU 10

" basrah, baada ya kupumzika basrah kwa muda wa siku chache nilielekea Baghdad jiji la amani, huku nimejaa kila namna ya vitu vya tunu na almasi nyungi.


Itaendelea...
SinBad angefufuka leo nakuiona Baghdad ilivyoaribiwa na akina Bush na Blair angelia sana jiji lake la amani
 
KISA CHA SINDBAD BAHARIA

SEHEMU 10

"Bwana wangu" nikamjibu "usiwe na khofu mimi si sheitwaan wala si jinni, wala si pepo mbaya, bali ni mwanadamu kama wewe tena mfanyabiashara, kisa changu kilichonifanya nifike hapa ni cha ajabu kishindacho kisa chengine chochote kilichowahi kumpata mtu, kwanza tafadhali hebu pokea almasi hizi ambazo mimi mwenyewe nimezikusanya kutoka katika lile bonde la kutisha.

Hapo nikachagua almasi chache nzuri kutoka mfukoni mwangu nikamkabidhi yule mtu, nikisema: "almasi hizi zitakuletea utajiri wowote unaoutaka."

Yule bwana alipozipokea na alipoona uzuri wake alifurahi sana; akanishukuru na kuniombea dua njema.

Wakati tulipokua tukiongea vile wakatokea wafanya biashara wengine kutoka pande nyengine za ule mlima. Wakatuzunguka wakisikiliza kwa mastaajabu makubwa yale yalionipata. Wakanipongeza wakisema, "hakika kuokoka kwako ni kwa ajabu sana, kwani hakuna mtu yeyote aliewahi kukanyaga bonde lile akarejea hai, mwenyezi mungu ashukuriwe kwa kuokoka"

Basi wale wafanya biashara wakanichukua mpaka kwenye kambi yao wakanipa chakula na kinywaji, halafu nikalala kama mfu, mapema asubuhi ya pili tukang'oa kambi na baada ya kusafiri kwa muda mrefu kupitia milima mirefu, tukafika kwenye ukingo wa bahari, huko tukapanda merkebu tukasafiri mpaka tukafika kwenye kisiwa kimoja kilichojaa miti yenye mashina manene.

Watu mia wangeweza kukaa kwenye kivuli cha mti mmoja, ni kutoka katika mashina ya miti hii ndiko kafuri inayotoa harufu nzuri baada ya watu kichimba mashina ya miti hiyo. Utomvu utokao huangukia kwenye vyombo maalum vilivyotegwa chini yake. Utomvu huo unapoganda hua kafuri.

Kwenye kisiwa hicho niliona pia wanyama wakubwa waitwao karkadan waliofanana na vifaru, wanyama hawa wamefanana na ng'ombe au nyati lakini warefu kuliko hata twiga, karkadan wanapembe katikati ya paji la uso na huwashambulia tembo kwa pembe yao hio na kuwakita nayo na kuwabeba kila waendako mpaka tembo hufa.

Baada ya muda mafuta ya tembo humyenyukia machoni na kumpofoa nakumuuwa yule karkadan. Hapo madege Rok kushuka kwa kasi na kuwabeba wote wawili tembo na karkadan mpaka kwenye vilele vya mlima kwenye viota vyao.

Basi hapo kisiwani nikawauzia wafanya biashara sehemu ya almasi zangu na nyengine nilibadilishana nao kwa bidhaa nyengine nyingi. Baada ya muda tulitweka matanga tukaendelea kufanya biashara kutoka bandari hadi bandari, na kutoka kisiwa kimoja hadi kingine mpaka tukawasili basrah, baada ya kupumzika basrah kwa muda wa siku chache nilielekea Baghdad jiji la amani, huku nimejaa kila namna ya vitu vya tunu na almasi nyungi.

Bila kukawia nilielekea nyumbani kwangu nilipokelewa mikono miwili na ndugu, jamaa na marafiki zangu na majirani. Wote nikawapa zawadi halafu nikatoa sadaka kwa maskini, yatima na wajane.

Baada ya muda nilisahau kabisa yale masaibu yote yalionipata katika safari yangu ya pili, nikaishi kwa raha, furaha na starehe zisizo na kifani nikawa nawaalika ndugu na marafiki kuja kwangu kila siku kushiriki maakuli mbali Mali.

Ikiwa navaa lebasi ghali za thamani mpaka sifa zangu zikaenea kote. Watu wakawa waja kusikiliza visa vya safari zangu zilizonifikisha nchi za mbali. Wote wakawa wanastaajabu kwa hatari nilizozikabili na kuokoka kwangu.

"Na hiyo waungwana ndio ilikua safari yangu ya pili" alimalizia kusimulia Sindbad Baharia. "Kesho in sha Allah nitawasimulia yaliyonipata safari yangu ya tatu."

Itaendelea...
Asante sana kwa hii hadithi yani ina suspense
 
Back
Top Bottom