madindigwa
JF-Expert Member
- Aug 30, 2017
- 2,453
- 2,849
DuhYule mwalimu akalalamika sana eti mwarabu anakutafuta nikajua ni soo nikataka kusema siendi yule mwalimu akasema amenipa hadi pesa nikutafute mwanae amekataa walimu wengine anasema wewe ndio anakuelewa kumbe yule mwarabu hana soo wala nini na dogo ananikubali maana alijaribu kupeleka mwalimu mwingine anayefuata miiko ya ualimu hakumsoma dogo dogo akamkataa eti ni mkali ,basi nikasema kesho lazima niende yule mwalimu akamaidi akasema niende siku hiyohiyo so jioni nitatimbakkoo
Kufika dogo akafurahi akakimbia kimwamsha mamake mama kuja ndio nikajua kumbe wanakula madawa ya kulevya na wanauza pia kuwa wako bongo kusukuma ndaga maana mama yule alikuja akiwa sober hatari ila akafurahi kifaransa king mix English alivyorudi ndani nikaanza story na michezo maana ile haikuwa tuition yalikuwa maagizo na aliyeyaleta ni dogo na mimi nilitaka pesa tu.
Baada ya kumaliza kama lisaa hivi nikataka kutoka siku ile yule mwarabu hakuwepo so dogo akaingia ndanikuniletea pesa mzee nikajua leo ni elfu hamsini ndogo akarudi akasema mamake ananiita ndani mzee kufika sebuleni namkuta kama kazima hivi akasema chukua hapo pesa nikachakua hamsini dogo akasema mbona unachukua kidogo mzee nikapiga kama laki tatu nikasepa .nikajiona mjinga sana kwa kuwa cocaine niliiona na mapesa kibao kwa kwanini nimechukua kidogo hivyo so nikajiapia kuwa next time nikirudi nakomba haswaa nachukua tax
Kesho yake jioni kama kawaida nikaibuka na michezo ukawa ile ile hapa sasa dogo ananiletea leo laki 3 kesho laki nne kiukweli ukawa ni kuondoka na mapesa ila nikajipa moyo kuwa siku dogo qkiniambia niingie ndani nichukue ndio basi
Snilikuwa na pesa na nilijua kuwa zinakotoka na pia mshua alianza kujua kuwa nimebadilika na pesa ninayo ,mshua huwa anatabia ya kukagua vyumbani mwetu bila sisi kujua na alikuwa ananitaka niingie jeshini hivyo alikuwa kwenye maandalizi ya kuona inakuwaje chuo au jeshi na aliniambia anatafuta chuo nje ya nchi ,mshua alikuwa haamini kabisa elimu ya bongo so katika kukagua kwake alibaini ninakiwango kikubwa cha pesa kuliko mtumishi wa umma so akawa nanifatilia kimyakimya ingekuwa leo ningeitwa mhujumu uchumi
USSR
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app