Kisa cha MwanaHALISI kufungiwa ni Habari ya "Nani anastahili kuombewa kati ya Lissu au Magufuli"


Mungu si mwanadamu na atatenda atakalo muda si mrefu.
 
Polisi na raia wengine waliouawa na majambazi KIBITI hakuna hata aliyethubutu kutangaza kuwaombea ndugu zetu wa KIBITI waliopoteza maisha yao.
Leo anatokea mtu mmoja amejeruhiwa watu wanatangaza maombi. Je, ni Mungu wa wapi huyo tunayemwomba?

Mkuu kila mtu ana vionjo vyake, huwezi kulazimisha kila mtu awaombee watu wa kibiti. Sio lazima wanaotaka kumuombea Lissu watake pia kuwaombea watu wa Kibiti. Kosa lingekuwa hao wanaotaka kumuombea Lissu kama walikataa watu wa kibiti kuombewa. Acha kubeba maneno ya propaganda za kizee hapa jukwaani na wewe kujifanya unajengea hoja zako toka hapo. Msilazimishe watu kuonyesha mapenzi yao kwa watu wasiofungamana nao. Hata wewe ukitaka kuwajibu vizuri hao wafuasi wa cdm wanaotaka kumuobea Lissu, kusanya wenzako kawaombee watu wa kibiti hakuna atakaye kukataza.
 
Ili gazeti kwa matusi haya lingefutwa kabisa..yani unamtukana Rais hivi uachwe? Shenzi.kabisa
 
Watanzania wanajuta sasa. Badala ya kuendeleza amani yetu ametuletea machafuko. 2020 ni bora tumrejeshe kwao akalime viazi vitamu. Hatufai kabisa.
 
Mkuu una maswali mazuri na fikirishi.. Sipendi nionekane najitetea au natetea serikali kuhusu hili.Nakupa mfano mmoja.,ukiwa unagombana na mkeo kila mara kwa sauti,huku ukiwa unampiga mikwara kibao.Huku majirani wakitega sikio na kusikiliza ugomvi wenu,siku ikitokea akapatwa na madhara moja kwa moja,majirani watajua kuna namna unahusika kutokana na ugomvi wenu wa mara kwa mara,wakati huo huo kutokana na ugomvi wenu kama kuna jirani yako yeyote alikuwa na visa binafsi na mkeo anaweza kumdhuru mkeo akijua wote watakuhisi wewe.Tukirudi kwenye ishu ya Lissu,kwa mtiririko wake wa kisiasa alikuwa anajenga hali tofauti,kumbuka tupo kwenye vita kali sana.Huwezi kunishawishi kwamba adui wa Lissu ni serikali ya TZ,hakuna mtu mwingine anaweza kuwa adui yake.So,yawezekana serikali ikahusika au akawa mtu mwingine,ila mimi hapa JF naongelea kwa ujumla Lissu angekosoa bila kejeli,na madharau na kuwa mwiba kwa serikali,asingetoa mwanya kwa serikali au mtu yeyote kumshoot kwa kisingizio chochote,inaweza isiwe serikali na bado aliyempiga risasi asipatine wala kujulikana milele,hata ungewaita CIA au scotland yard,aliyemuua JF Kennedy aliwahi patikana?,aliyemuua 2Pac aliwahi kujulilkana?,tukubali ukweli kuwa Lissu alisahau yeye sio Raisi wa Jamhuri,ingawa upo sahihi kauli nyingine za Raisi sio nzuri.
 
You are really, giant fool.
 
Bora yawe masahihisho sahihi sasa. Hao wakosoaji wenu wewe umeamua kuwaita"wakatisha tamaa" wakati wenzako wakiwaita wasaliti. Nikiwarejea hao wanao wakatisha tamaa kwa kukosoa approach inayo tumika sasa hivi huko nyuma waliwahi pia kukosoa mkawapa majina mabaya kama mnavo fanya sasa hivi!!!.....laiti wangesikilizwa hakika muda huu tungekuwa tunafanya mambo mengine. Ni takriban miaka 20 imepita ndo mmegutuka na kubaini makosa!!!!....wenye utambuzi wanapo waonya mkubali maonyo yao na si kuwapa majina mabaya! zingatieni mnacho ambiwa kwani uwezo wa ku load tunazidiana, wengine hutumia sekunde, dakika, siku,.........wengine miaka 20 kama nyinyi. Ndugu swala si kufanya masahihisho bali ni kuweka majawabu sahihi, ili baadaye usirudie kufanya masahihisho ya masahihisho!
 
You haven't said anything new!!! So obvious that even an imbecile knows that!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona unashindwa kuzipangua hizo hoja???
Msaliti ni mikataba mibovu, na walioiingiza nchi kwa maslahi yao AU ni Lisu anaeikosoa, na kuwaelimisha wananchi.???? HUONI KWAMBA HAPO KUNA FILAMU YA KICHINA???
 
You are very right. Ile makala nimeisoma jana imenitoa machozi nilipomkumbuka mzalendo wa kweli na mtz muhimu zaidi nchini anayepaswa kuombewa.......hawa walaaniwa ccm na baradhuri wao mkuu wanaharibu nchi wkt hawana faida yoyote..
 
we mbwa acha uongo....watz wanatafuta hizo t-shirt bila mafaniko
 

Sasa naona umejadili kwa hoja, huo udhaifu wa Lissu kila mtu anaujua hilo halina ubishi, lakini nimekuambia kila mtu ana madhaifu yake. Kuna watu wana viherere, waongo, wanafiki, washirikina nk. Lakini tunaishi nao hivyo hivyo na kero hizo na sio sahihi kuondoa uhai wao kisa wana tabia zinazokera. Sisemi serekali inahusika lakini kwa mazingira ndio kinara namba moja hata ukiangilia mfano wa mtu mwenye ugomvi na mkewe. Nikupe mfano mmoja unaaocha shaka, kwenye eneo aliloshambuliwa Lissu kulikuwa na askari polisi wa kulinda eneo lile. Kwa askari wenye weledi halafu usikie mlio wa smg tena risasi zaidi ya 30, halafu litoke gari eneo hilo hilo bila kulizuia, inahitaji uwezo wa kufikiri uwe umefika mwisho ndio usione huo utata. Hata mimi sina utaalamu wa silaha, lakini mlio wa bunduki ukilia tena risasi zisizopungua 30 nitajua hilo eneo sio salama, sembuse askari anayejua silaha?

Mkuu hebu tujadili mengine sio hili, ndo maana nakuambia hata uwe mzalendo vipi, kipimo chake hakiwezi kuwa kilichomkuta Lissu. Kumbuka Lissu ana rekodi nzuri ya kutetea raslimali zetu kuliko mzalendo academia. Kama wengine ndio wanahisi vita ya raslimali zetu zimeanza leo, tunabaki tunawashangaa kumbe wenzetu ndio wanaamka sasa wakati vita vilianza muda mrefu tu. Kwa hiyo kwetu sisi tunaona ni kick za kisiasa tu, tulitarajia tuombwe msamha wa wizi uliotokea na kukubali hadharani jitihada za wale waliopigania raslimali hizo toka zamani. Kisha kama taifa tusonge pamoja. Lakini kiongozi wetu leo kujiona ndio mzalendo sana, kwa sisi wakristo tuna mfananisha na mtu aliyealikwa harusini kisha akalazimisha kukaa katika kiti cha mbele.
 
Sawa uwezo wangu mdogo ila usini ban,ila pingana na mimi kwa kushindana na serikali,anza na kuandamana tu,anzisha movement yoyote ya kelele zozote mtaani kwenu,waje FFU wakutengue kiuno ukaugulie halafu urudi hapa uelezee u GENIOUS wako hapa.Shwein.
Nampigia mbuzi gitaa
 
Ila miaka hii kazi ipo kweli kweli,ngoja tuone,yangu macho bora tufike salama
 
haka kakipande ka hii habari ngoja ni kakariri katanifaa sana 2020...katanisaidia kuombea kura zote, lakini pia nikiwa kwenye foleni ya kura kataniliwaza...
 
Kwani Rais wako watatu?
Ni kweli ni watatu"
Rais wa kwanza ni mikataba ya wizi, iliosainiwa na serikali zilizopita,, akiwepo huyu rais wasasa. Itawakandamiza hadi muda waliokubaliana kuiba uishe.

Rais wa pili ni Magu, anatuchezea filamu yakutokuitambua, mikataba ambayo mwanzo aliijua na kuikubali.

Rais wa tatu, ni rais Tundu Lisu. Huyu ni wa kujitolea, na wa Muda wote.
Alianza kuikosoa na kuipinga hio mikataba tangu miaka 16 iliopita, kwa marais wengine.
Huyu ndie anaewapigania wa nyonge, kwa kuisema kweli yoote...
Mfno:: Swala la kukamatwa ndege,serikali iliwadanganya wananchi. Lisu akasema ukweli. ..baadae serikali ikakiri na kuongea ukweli.

KINACHOMUUA LISU NI UKWELI.
 

Mungu akubariki sana Mkuu.Ni Watu wachache wenye Ubinadamu ktk Dunia hii ,inasikitisha sana kuona Raia asie na silaha/mtetezi wa Raia anashambuliwa kwa Silaha za moto (kali) kama Mnyama mkali alieingilia makazi ya Watu ..Inahuzunisha zaidi kuona na kusikia baadhi ya Watu wasio na Ubinadamu wakilifurahia hili na kushangilia.

Umasikini na Ujinga umetufanya kiasi tumepoteza ule uwezo wa kufikiri mpaka tunawaaabudu na kuwatukuza Binadamu wengine na kuwageuza Miungu (Watu) wasiokosea....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…