John Manoni
JF-Expert Member
- Sep 5, 2020
- 611
- 381
Mama Panya aliona mtego wa panya uliotegwa na binadamu, alisononeka sana kwa sababu ya mtego ule uliokuwa unatishia kuangamiza maisha yake na watoto wake.
Alimfuata Jogoo, akamuomba amsaidie kuutegua ule mtego lakini Jogoo alikataa, alipomfuata mbuzi alimfukuza, akaenda kwa Ng'ombe akamjibu, 'mambo ya mtego wa panya yanakuhusu wewe panya mimi Ng'ombe sina ugomvi na binadamu sasa mtego unanihusu?'
Wote hao hawakujua kwamba, mtego wa panya hunasa waliomo na wasiokuwamo! Mtego ulimnasa Nyoka, naye akamuuma binadamu, ndipo wale wote yalipowafika mauti!
Uchaguzi huu unawahusu walimu, polisi na wafanyakazi wote, unawahusu wakulima na wafanyabiashara, unawahusu wavuvi na wafugaji, unawahusu mijini na vijijini. Hata wanajidanganya kuwa wanalipwa mshahara na CCM unawahusu pia, kwa sababu kila mshahara ni kodi za watanzania.
Mwaka wa 59 wa uhuru bado tunafokewa kunyimwa maji! Bado wanahabari wanatetemeka! Nchi nzima hakuna kusema mfalme yuko uchi eti kwa sababu limejengwa daraja!
Wasalaam.
Alimfuata Jogoo, akamuomba amsaidie kuutegua ule mtego lakini Jogoo alikataa, alipomfuata mbuzi alimfukuza, akaenda kwa Ng'ombe akamjibu, 'mambo ya mtego wa panya yanakuhusu wewe panya mimi Ng'ombe sina ugomvi na binadamu sasa mtego unanihusu?'
Wote hao hawakujua kwamba, mtego wa panya hunasa waliomo na wasiokuwamo! Mtego ulimnasa Nyoka, naye akamuuma binadamu, ndipo wale wote yalipowafika mauti!
Uchaguzi huu unawahusu walimu, polisi na wafanyakazi wote, unawahusu wakulima na wafanyabiashara, unawahusu wavuvi na wafugaji, unawahusu mijini na vijijini. Hata wanajidanganya kuwa wanalipwa mshahara na CCM unawahusu pia, kwa sababu kila mshahara ni kodi za watanzania.
Mwaka wa 59 wa uhuru bado tunafokewa kunyimwa maji! Bado wanahabari wanatetemeka! Nchi nzima hakuna kusema mfalme yuko uchi eti kwa sababu limejengwa daraja!
Wasalaam.