Elections 2010 Kiravu-tunaomba majina ya mawakala wa chadema waliosaini fomu za matokeo ya hai na ub

Jatropha

JF-Expert Member
Apr 9, 2009
1,151
199
jana tar 04 nov 2010 wakati wa kutangazwa kwa matokeo ya kura za urais, tume ya uchaguzi iliwakaribisha waandishi wa habari waliokuwepo kuuliza maswali. Moja kati ya maswali yaliyoulizwa ni madai ya dr slaa aliyoyatoa tar 03 nov 2010 kuhusu kura zake kupunguzwa kwa makusudi akitoa mfano wa matatu ya majimbo ya hai, ubungo na geita.

Akijibu swali hilo mkurugenzi wa tume hiyo ndg rajabu kiravu alisema kuwa tume imefanikiwa kupata fomu za kujumlisha matokeo kutoka katika majimbo hayo na akataja kuwa idadi ya kura katika majimbo ya hai na ubungo iko sahihi na imethibitishwa na mawakala wa chadema. Ila akakiri kuwa tume ilifanya makosa katika jimbo la geita kutangaza kura za dr slaa pungufu.

Kwa kuwa tuhuma hizi ni nzito sana, nilitarajia majibu ya tume yatakuwa exhaustive enough kwa kutaja jina la mawakala wa chadema wanaoonekana katika fomu za matokeo kwa majimbo ya hai na ubungo. Kutotaja majina ya mawakala hawa bado kumebakiza wingu zito katika suala hili.

Tunamuomba dr slaa atuulizie swali hili ili tupate majibu ya kuridhisha kama kweli mawakala wa chadema walishiriki na kuthibitisha ujumlishaji wa kura za dr slaa katika majimbo ya hai na ubungo.
 
Kama waligushi tiketi za ndege ya serikali aliyotumia Salma watashindwa kwenye hili?
 
Back
Top Bottom