Kiranga yupo sahihi: Ujinga katika jamii ya Kitanzania umekaa kiutamaduni zaidi, ni ngumu sana kuutokomeza kwa kwenda shule

Youngblood

JF-Expert Member
Aug 1, 2014
18,962
55,059
Kiranga hii pointi yake tangu jana imenifikirisha sana, uliyosema yote hapa ni ukweli mtupu.

Juzi kati nilienda kijijini huko nyanda za juu kusini nimekuta watu wanafanya mambo ya kijinga wasomi na ambao sio wasomi, watu wengi bado wana imani potofu sana, kwakweli inasikitisha sana.

Nina mifano kadhaa ambayo nimeishuhudia mwenyewe.

1. Kuna dogo ameungua na moto wakaenda kwa mganga akawaambia amemwagiwa maji ya moto na mizimu, kama sio kurumbana sana dogo angekufa na kile kidonda mana waligoma kumpeleka hospitali anapakwa mavi ya ngombe ndo dawa.

2. Kuna jirani yetu alikuwa ana kansa ya shingo ya kizazi, hii nina uhakika nayo kabisa mana mtu wangu wa karibu kabisa aliugua ugongwa kama huu wa jirani akapona, ila hawa majirani walimuacha huyo mgonjwa tangu 2022 januari, amefariki December mwaka 2023 kwa upungufu wa damu, ndugu waligoma kumpeleka hospitali wanadai umerogwa na mke mwenzake.

3 Kuna mshkaji wangu mamake mdogo alipata shida wakati wa kujifungua, ikapelekea kupata fistula, bado yupo nyumbani kila siku kwa waganga anadai amelogwa.

Ujinga wa watanzania ni kweli upo kama utamaduni au tuseme ni kama dini (imani) hata utumie nguvu nyingi kiasi gani kuwaelewesha watakuona wewe ndo umepotea.

Watu wanatorosha wagonjwa hospitali wanapeleka kwa waganga wa kienyeji.

Kwa kweli tuna safari ndefu sana.

Credit Kiranga
 
Mkuu,

Asante kwa kutambua matatizo yetu makubwa na kutoa mifano.

Ni vizuri pia kutambua kuwa hatutakiwi kuchoka wala kukata tamaa, kwamba hata ikiwa katika watu mia utakaojitahidi kuwaelewesha, akielewa mmoja tu, bado tunatakiwa kuendelea na kazi ngumu ya kufundishana, kuelimishana.

Kila maisha ya mtu yana stahili kupewa nafasi sawa kuhifadhiwa. Hivyo tuendelee kusaidiana kwa hali kama si kwa mali.

Watu wakikataa knowledge kwa ujinga wao, hilo ni tatizo lao.
 
Ujinga na umaskini ndo vinapelekea watu kuamini ushirikina japokuwa uchawi wenyewe haupo. Case in point, ni nadra sana kusikia story za watu kufufuka, kupaa na ungo, kutoweka kichawi, kujifungua jiwe, mauaji ya albino nk jijini Dar ambako kuna watu wengi wenye kipato cha Kati na wameelimika kuliko kule Chitipa au Geita let alone Ulaya/Amerika. Hizi story za kipuuuzi hazipo kabisa huko. Huwezi kuta BBC au Al Jazeera wanaripoti ujinga wa mtu kufufuka au kuanguka na ungo, wanajua wasomaji wao wengi Wana akili timamu na implications za kutoa habari za kipuuuzi. Hizi habari unazikuta Millard ayo, Geita yetu, Kigoma yetu, Mbeya yetu blog.
 
Hii mifano umetoa ni wajinga kweli mkuu, ila kuna makombora wanarushiwa watu halionekani kwenye kipimo chochote ata wakupeleke u.s.a muulize Mwakyembe...alitupiwa kitu ngozi inanyonyoka mabaka kama kenge. Mwiko kujihusisha ila vzuri ujue yapo, kama kuna evil basi kuna good

Tustick na Muumba Alpha na Omega 🙏
 
Kiranga hii pointi yake tangu jana imenifikirisha sana,uliyosema yote hapa ni ukweli mtupu

Juzi kati nilienda kijijini huko nyanda za juu kusini nimekuta watu wanafanya mambo ya kijinga wasomi na ambao sio wasomi, watu wengi bado wana imani potofu sana, kwakweli inasikitisha sana.

Nina mifano kadhaa ambayo nimeishuhudia mwenyewe.

1. Kuna dogo ameungua na moto wakaenda kwa mganga akawaambia amemwagiwa maji ya moto na mizimu,kama sio kurumbana sana dogo angekufa na kile kidonda mana waligoma kumpeleka hospitali.anapakwa mavi ya ngombe ndo dawa.

2. Kuna jirani yetu alikuwa ana kansa ya shingo ya kizazi,hii nina uhakika nayo kabisa mana mtu wangu wa karibu kabisa aliugua ugongwa kama huu wa jirani akapona,ila hawa majirani walimuacha huyo mgonjwa tangu 2022 januari, amefariki December mwaka 2023 kwa upungufu wa damu,ndugu waligoma kumpeleka hospitali wanadai umerogwa na mke mwenzake.

3 Kuna mshkaji wangu mamake mdogo alipata shida wakati wa kujifungua,ikapelekea kupata fistula,bado yupo nyumbani kila siku kwa waganga anadai amelogwa.

Ujinga wa watanzania ni kweli upo kama utamaduni au tuseme ni kama dini(imani) hata utumie nguvu nyingi kiasi gani kuwaelewesha watakuona wewe ndo umepotea.

Watu wanatorosha wagonjwa hospitali wanapeleka kwa waganga wa kienyeji.

Kwa kweli tuna safari ndefu sana.

Credit Kiranga
Uko sahihi. Ila umekosea kwa kusema shule haiwezi kuutokomeza. Shule zenye elimu sahihi zinatokomeza. Tatizo ni kuwa shule zetu hazina elimu sahihi. Mwalimu anayefundisha unakuta naye anaamini hayo hayo na anawaaminisha wanafunzi yapo.
 
Hii mifano umetoa ni wajinga kweli mkuu, ila kuna makombora wanarushiwa watu halionekani kwenye kipimo chochote ata wakupeleke u.s.a muulize Mwakyembe...alitupiwa kitu ngozi inanyonyoka mabaka kama kenge. Mwiko kujihusisha ila vzuri ujue yapo, kama kuna evil basi kuna good

Tustick na Muumba Alpha na Omega 🙏
Tunarudi kulekulee.

Wewe umejuaje hili kombora na si kitu kingine chochote tu?
 
Uko sahihi. Ila umekosea kwa kusema shule haiwezi kuutokomeza. Shule zenye elimu sahihi zinatokomeza. Tatizo ni kuwa shule zetu hazina elimu sahihi. Mwalimu anayefundisha unakuta naye anaamini hayo hayo na anawaaminisha wanafunzi yapo.
Mkuu,

Magufuli alivyoenda kunywa kikombe cha babu alikuwa na Masters au Ph.D tayari?

Regardless. Alikuwa at least na Masters ya Kemia. Nafikiri alikuwa hajapata Ph.D bado. Alikuwa yupo kwenye top leadership ya nchi. Ana access na mambo kibao mpaka ya cabinet level.

Anaenda kuhangaika kunywa mikombe kwa Babu na yeye.

Sasa hapo ukija kwa mwanakijiji, ingawa hakuna direct correlation, lakini chances are atakuwa susceptible zaidi kuamini hayo mambo ya ramli na supernatural powers.
 
Ujinga na umaskini ndo vinapelekea watu kuamini ushirikina japokuwa uchawi wenyewe haupo. Case in point, ni nadra sana kusikia story za watu kufufuka, kupaa na ungo, kutoweka kichawi, kujifungua jiwe, mauaji ya albino nk jijini Dar ambako kuna watu wengi wenye kipato cha Kati na wameelimika kuliko kule Chitipa au Geita let alone Ulaya/Amerika. Hizi story za kipuuuzi hazipo kabisa huko. Huwezi kuta BBC au Al Jazeera wanaripoti ujinga wa mtu kufufuka au kuanguka na ungo, wanajua wasomaji wao wengi Wana akili timamu na implications za kuwapa habari za kipuuuzi. Hizi habari unazikuta Millard ayo, Geita yetu, Kigoma yetu, Mbeya yetu blog.
 
Tunarudi kulekulee.

Wewe umejuaje hili kombora na si kitu kingine chochote tu?
Honestly hujawahi kusikia hili mtu anaumwa kazunguka hospital anaambiwa ugonjwa hauonekani? Unaish bongo? Au uko diaspora miaka mingi mkuu?

Haya mambo ya imani kuna siku nlikuuliza wafanya mazingaombwe mtu anakula viwembe, misumari, anakanyangwa na gari na hafi hukunijibu kitu, nna imani uliona bbc docu ya tb joshua ile karama yake anapoint mtu unaruka hukoo ni maigizo?? Nachagua kutojihusisha na ushirikina ila haimaanishi si amini kama upo tena dhahiri

Mimi sio rocket scientist ila hainizuii kuamini watu wanaenda space hata kama sijawahi enda why limit your self the world is an enigma.
 
Umeamua kutuchafua watu wa Nyanda za juu kusini au siyo??.Nenda Uchagani pia kajionee Matambiko yao,nenda Usukumani huko kajionee vituko huko.Sipingani na wewe hili tatizo ni Almost Afrika nzima mkuu.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
Ni kweli mkuu,ili ni Afrika nzima,sijui hata tunalitatua kwa namna gani!
 
Honestly hujawahi kusikia hili mtu anaumwa kazunguka hospital anaambiwa ugonjwa hauonekani? Unaish bongo? Au uko diaspora miaka mingi mkuu?

Haya mambo ya imani kuna siku nlikuuliza wafanya mazingaombwe mtu anakula viwembe, misumari, anakanyangwa na gari na hafi hukunijibu kitu, nna imani uliona bbc docu ya tb joshua ile karama yake anapoint mtu unaruka hukoo ni maigizo?? Nachagua kutojihusisha na ushirikina ila haimaanishi si amini kama upo tena dhahiri

Mimi sio rocket scientist ila hainizuii kuamini watu wanaenda space hata kama sijawahi enda why limit your self the world is an enigma.
Mkuu,

Mtu akizunguka hospitali za Bongo madaktari wakashindwa kugundua tatizo, tayari ni kombora?

Unaelewa kuna magonjwa mengi modern medicine haijayatambua na si makombora wala nini?

Unajua kwamba mpaka Ulaya walikotuzidi teknolojia na usomi mpaka leo kuna magonjwa hayaeleweki, na kutoeleweka huko hakumaanishi magonjwa hayo ni uchawi?

Unaelewa medicine ni science na science is an ever evolving domain?

Unajua kutojua ugonjwa ni nini haimaanishi kuwa ni uchawi?

Unajua kwamba unaweza usiujue ugonjwa ni ugonjwa gani, na ugonjwa ukawa si uchawi?

Unajua mambo ya magonjwa ya watu maarufu mara nyingi huwa yanafichwafichwa kwa kufuatilia kanuni za faragha za wagonjwa na mara nyingine unaweza kuambiwa ugonjwa haujulikani kwa sababu mgonjwa hajataka tu kutangaza ugonjwa?
 
Mkuu,

Asante kwa kutambua matatizo yetu makubwa na kutoa mifano.

Ni vizuri pia kutambua kuwa hatutakiwi kuchoka wala kukata tamaa, kwamba hata ikiwa katika watu mia utakaojitahidi kuwaelewesha, akielewa mmoja tu, bado tunatakiwa kuendelea na kazi ngumu ya kufundishana, kuelimishana.

Kila maisha ya mtu yana stahili kupewa nafasi sawa kuhifadhiwa. Hivyo tuendelee kusaidiana kwa hali kama si kwa mali.

Watu wakikataa knowledge kwa ujinga wao, hilo ni tatizo lao.
Noted, tutaendelea kuwapa elimu
 
Back
Top Bottom