Kipindi cha Neema Ya Umeme Kimeanza Leo, Tupeane Taarifa

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,077
Katika ulimwengu wa watu waliostaarabika, ni aibu kubwa na kukosa nidhamu kwa kiwango cha juu kama mtu ukishindwa kutimiza ahadi yako mwenyewe, uliyoitoa kwa hiari yako mwenyewe bila ya kulazimishwa na mtu yeyote. Anayeshindwa kutekeleza ahadi yake mwenyewe, huyo amekosa nidhamu kwa nafsi yake mwenyewe.

Tukumbushane: Rais Samia na Serikali yake iliwaahidi Watanzania kuwa tatizo la umeme linaishia mwezi January 2024, na kwamba neema ya upatikanaji umeme wakati wote, umeme wa uhakika itaanza mwezi February 2024, kwa sababu mlango mmoja wa bwawa la Mwalimu Nyerere utafunguliwa. Akaongeza kuwa ziada kubwa ya umeme itapatikana kuanzia mwezi March 2024 watakapofungua mlango wa pili wa bwawa la Mwalimu Nyerere.

Leo ndiyo tarehe 1 mwezi February 2024, na kwa ahadi ya Rais na Serikali yake ndiyo tumeingia mwanzo wa kipindi cha neema kitakachotufanya tuyakumbuke masuala ya mgao wa umeme kuwa historia.

Naomba tupeane taarifa juu ya upatikanaji wa umeme kwa nchi nzima kuanzia leo, kupitia uzi huu ili tujue kuwa Rais wetu ni mtu mwenye nidhamu ya hali ya juu au la. Na kisha apongezwe kwa kutokomeza tatizo sugu la umeme au tumlaani kwa kutudanganya.

Tutambue kuwa yeyote anayefifisha au anayeshindwa kulihakikishia umeme wa uhakika Taifa, analiangamuza Taifa. Maendeleo ya nyanja zote yanategemea uwepo wa nishati ya uhakika ya umeme.
 
Lucas njoo na huku utoe utetezi wako kama kawaida,ama huwa unatoa kwa mwenezi pekee
Mwashambwa anajua sana jinsi Serikali hii ilivyojaa wababaishaji ila huwa anajitoa ufahamu ili mkono uende kinywani.

Huko aliko huenda sahizi umeme umekata, anahangaika kutafuta sehemu yenye kajenereta achaji simu yake. Ila kasimu kake kakipata tu chaji kidogo, atakuja hapa na yale maneno yake, "Rais wetu komandoo, chuma cha reli anahangaika usiku na mchana kuhakikisha nchi wakati wote inakuwa na umeme wa uhakika"!!
 
Katika ulimwengu wa watu waliostaarabika, ni aibu kubwa na kukosa nidhamu kwa kiwango cha juu kama mtu ukishindwa kutimiza ahadi yako mwenyewe, uliyoitoa kwa hiari yako mwenyewe bila ya kulazimishwa na mtu yeyote. Anayeshindwa kutekeleza ahadi yake mwenyewe, huyo amekosa nidhamu kwa nafsi yake mwenyewe.

Tukumbushane: Rais Samia na Serikali yake iliwaahidi Watanzania kuwa tatizo la umeme linaishia mwezi January 2024, na kwamba neema ya upatikanaji umeme wakati wote, umeme wa uhakika itaanza mwezi February 2024, kwa sababu mlango mmoja wa bwawa la Mwalimu Nyerere utafunguliwa. Akaongeza kuwa ziada kubwa ya umeme itapatikana kuanzia mwezi March 2024 watakapofungua mlango wa pili wa bwawa la Mwalimu Nyerere.

Leo ndiyo tarehe 1 mwezi February 2024, na kwa ahadi ya Rais na Serikali yake ndiyo tumeingia mwanzo wa kipindi cha neema kitakachotufanya tuyakumbuke masuala ya mgao wa umeme kuwa historia.

Naomba tupeane taarifa juu ya upatikanaji wa umeme kwa nchi nzima kuanzia leo, kupitia uzi huu ili tujue kuwa Rais wetu ni mtu mwenye nidhamu ya hali ya juu au la. Na kisha apongezwe kwa kutokomeza tatizo sugu la umeme au tumlaani kwa kutudanganya.

Tutambue kuwa yeyote anayefifisha au anayeshindwa kulihakikishia umeme wa uhakika Taifa, analiangamuza Taifa. Maendeleo ya nyanja zote yanategemea uwepo wa nishati ya uhakika ya umeme.

Mod: Tafadhali kwenye heading, isomeke, "kimeanza", siyo "umeanza"
Msijiuzulu holela (kwa sauti ya hussein mwinyi)
 
Katika ulimwengu wa watu waliostaarabika, ni aibu kubwa na kukosa nidhamu kwa kiwango cha juu kama mtu ukishindwa kutimiza ahadi yako mwenyewe, uliyoitoa kwa hiari yako mwenyewe bila ya kulazimishwa na mtu yeyote. Anayeshindwa kutekeleza ahadi yake mwenyewe, huyo amekosa nidhamu kwa nafsi yake mwenyewe.

Tukumbushane: Rais Samia na Serikali yake iliwaahidi Watanzania kuwa tatizo la umeme linaishia mwezi January 2024, na kwamba neema ya upatikanaji umeme wakati wote, umeme wa uhakika itaanza mwezi February 2024, kwa sababu mlango mmoja wa bwawa la Mwalimu Nyerere utafunguliwa. Akaongeza kuwa ziada kubwa ya umeme itapatikana kuanzia mwezi March 2024 watakapofungua mlango wa pili wa bwawa la Mwalimu Nyerere.

Leo ndiyo tarehe 1 mwezi February 2024, na kwa ahadi ya Rais na Serikali yake ndiyo tumeingia mwanzo wa kipindi cha neema kitakachotufanya tuyakumbuke masuala ya mgao wa umeme kuwa historia.

Naomba tupeane taarifa juu ya upatikanaji wa umeme kwa nchi nzima kuanzia leo, kupitia uzi huu ili tujue kuwa Rais wetu ni mtu mwenye nidhamu ya hali ya juu au la. Na kisha apongezwe kwa kutokomeza tatizo sugu la umeme au tumlaani kwa kutudanganya.

Tutambue kuwa yeyote anayefifisha au anayeshindwa kulihakikishia umeme wa uhakika Taifa, analiangamuza Taifa. Maendeleo ya nyanja zote yanategemea uwepo wa nishati ya uhakika ya umeme.

Mod: Tafadhali kwenye heading, isomeke, "kimeanza", siyo "umeanza"
Waluiluwi kama ChoiceVariable wapo bize kupambania legacy uchwara hawana hili wala lile kwenye maendeleo. Wao wakipewa ahadi wanacheza sebene hata kama ni ahadi hewa
 
Mwashambwa anajua sana jinsi Serikali hii ilivyojaa wababaishaji ila huwa anajitoa ufahamu ili mkono uende kinywani.

Huko aliko huenda sahizi umeme umekata, anahangaika kutafuta sehemu yenye kajenereta achaji simu yake. Ila kasimu kake kakipata tu chaji kidogo, atakuja hapa na yale maneno yake, "Rais wetu komandoo, chuma cha reli anahangaika usiku na mchana kuhakikisha nchi wakati wote inakuwa na umeme wa uhakika"!!
Hahahahaaaa..........😁😅
 
Usiwaamini CCM, ni waongo hata shetani anawashangaa jinsi walivyo waongo
Jana nilipita jimboni kwa Bashe, kulikuwa hakuna umeme. Wananchi walikuwa wakilalamika kuwa Bashe anahangaika kujaza mabango ya yake na Rais mitaani badala ya kushugulikia tatizo la umeme, maana karibia kila siku mchana hakuna umeme, wanaletewa umeme usiku.
 
Back
Top Bottom