Kipimo halali kinachokubalika Tanzania kujipima mwenyewe HIV ni kipi?

Kipimo halali kinachokubalika Tanzania kujipima mwenyewe HIV ni kipi?

Farolito

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2018
Posts
14,952
Reaction score
34,959
Habari

Ni kipimo gani ambacho kinakubalika na serikali ya Tanzania kujipima mwenyewe(self test) virusi vya Ukimwi(HIV)

Ukienda kuuliza kwenye maduka ya dawa (pharmacy) hivi vipimo vya kupima kwa kutoa damu wengi wanauza kwa kificho kwa maana hairuhusiwi kumuuzia mtu binafsi.

Kuna kipimo cha kutoa sample mdomoni hiki hakipatikani sana maeneo mengi.

Je kipi ni kipimo halali na kupima HIV ambacho unapata bila kificho wala taabu na wapi unapata kirahisi.

Ahsante.

home-blood-test-kit-for-hiv-aids-cordelia-molloy.jpg
images.jpeg
 
Oralself test,nenda vituo vya tiba hasa vyenye CTC
 
Ukijipima mwenyewe ukajinyonga?
Au ukimpima mtu akaenda kufanya maamuzi ya kujiua kisa tu amegundua ana HIV?

Suala sio vipimo bali taratibu za upimaji unazingatiwa hadi kupata majibu?
 
Mkuu, nenda kwenye hospitali/kituo cha afya/zahanati wanaotoa huduma za tiba na matunzo (CTC) watakupatia jipime. Kwa sasa ziko za kutumia sampuli za kinywa (oral based ST) na za kutumia damu (blood based ST)

ANGALIZO:
Vipimo hivi vitumika kama 'screening tool' hivyo kuhakiki majibu yako lazima ufike hospitali/kituo cha afya /zahanati wataalam wakupime kwa bioline
 
Ukijipima mwenyewe ukajinyonga?
Au ukimpima mtu akaenda kufanya maamuzi ya kujiua kisa tu amegundua ana HIV?

Suala sio vipimo bali taratibu za upimaji unazingatiwa hadi kupata majibu?
Mbona watu wanajipima kisukari hawajinyongi?tuache tuache mawazo hasi
 
Mkuu, nenda kwenye hospitali/kituo cha afya/zahanati wanaotoa huduma za tiba na matunzo (CTC) watakupatia jipime. Kwa sasa ziko za kutumia sampuli za kinywa (oral based ST) na za kutumia damu (blood based ST)

ANGALIZO:
Vipimo hivi vitumika kama 'screening tool' hivyo kuhakiki majibu yako lazima ufike hospitali/kituo cha afya /zahanati wataalam wakupime kwa bioline
Asante kwa muongozo Mkuu
 
Kuna kina kimoja kinaitwa Abolt, alikuja nacho mtu tupime ili nile nyama nyama ni cha damu ( kinatumia damu ).
 
Back
Top Bottom