Kipi tujifunze kama Taifa katika picha hii ya Mama Maria Nyerere akiwa pamoja na Mbowe na Dr. Slaa

Kuna utofauti mkubwa kati ya baba wa Taifa na Baba wa chama cha mapinduzi.
Hapa picha ya J.K.Nyerere imetumika kama Baba wa Taifa na Mjane wake hapa anawakilisha taswira ya uasisi wa Taifa.
Hakuna anayekatazwa kutumia jina au picha ya baba wa Taifa kwa maslahi ya Taifa ilihali tu asivunjiwe heshima.
Huoni kuwa huu ni unafiki uliopitiliza kwa hawa viongozi wa CHADEMA kutumia picha ya kiongozi wanayemfahamu kuwa ni muongo na mdanganyifu na alilidanganya taifa kwa muda mrefu na taifa limeendelea "kudanganyika".
 
Mkuu MwanaDiwani

Kwa ufupi tokea Dr.W.Slaa achukue uungu mtu ndan ya chama hiko basi unafiki na uwongo umetamalaki kwa kasi ya hali ya ajabu

Plus nguvu ya Ayatollah Mtei na program zake za ukanda na ukabila hiki chama ni kama wamekizika moja kwa moja

Hata kama mtu kama tundu lisu atafurukuta vipi kujikwamua kwa hoja zake za kucopy na upaste haitasaidia

Ukiangalia hii picha kwa undan utajifunza unafiki uliokomaa na kushika mizizi walionao chadema
Ndugu nimekuelewa vizuri.

Mimi huwa ninasema, CHADEMA kimejengwa ndani kwa misingi ya kilaghai. Wawe wanaohoji na kutaka kuufahamu ukweli wakiwa ndani ya CHADEMA kama viongozi au wananchama, huwa wanalazimishwa kujiuzuru au wanaishia kufukuzwa.

Hii ndiyo CHADEMA.
 
Nyerere hakuwa Mungu wala Malaika, alichokisema TL ni kukosoa baadhi ya mambo yaliyofanywa chini ya utawala wa Nyerere ambayo mpaka sasa yanaligharimu taifa hili. Hii ndio democracy ya kweli na sio unafiki wa kukumbatia maovu. Kukusoana ni nyenzo muhimu ya kufikia ukweli.

  • :der:
Tumezoea kuwa wanafiki, unaamini hivi kinywani mwako unaongea vinginevyo. Namuheshimu Tindu Lissu kwa sababu anakisema kile anachokiamini, mimi binafsi sikuyapenda sana maneno ya Lisu ya kumkashifu Mwalimu lakini hivyo ndivyo Lisu anavyoamini na anasema anachokianmini tofauti na wengi wa viongozi wetu wengi wanaojifanya ni waumini wa Mwalimu wakati hawaishi yale aliyoyaamini Mwalimu, ni wezi, walafi, wabinafsi, mafisadi, wanyonyaji kama walivyo wajumbe wa bunge la katiba kule Dodoma. Najua angekuwepo Mwalimu leo lile bunge la katiba lingekuwa limesha sambaratishwa kwa sababu ule ni mradi wa kufisidi kodi za wavuja jasho wa nchi hii ulioratibiwa na Ikulu yenyewe - hakika ni wizi mtupu - shame upon you.
 
Nani kasema Baba wa Taifa alikuwa Mungu?.

Kukosoa na kumuita mtu muongo na tapeli achilia mbali binadamu mwenye stature ya Baba wa Taifa, Mwl. Nyerere ni vitu viwili tofauti.

Kilichotakiwa kukosolewa (kama kipo) ni kazi alizozifanya na siyo personality yake kama viongozi wa UKAWA-nje na ndani walivyofanya wakiongozwa na viongozi wakuu wa CHADEMA
Wewe umesema!... Huyu ni baba yako, ni baba ya baba yako na baba ya mama yako... Sasa huu uwezo katoa wapi?
 
Tumezoea kuwa wanafiki, unaamini hivi kinywani mwako unaongea vinginevyo. Namuheshimu Tindu Lissu kwa sababu anakisema kile anachokiamini, mimi binafsi sikuyapenda sana maneno ya Lisu ya kumkashifu Mwalimu lakini hivyo ndivyo Lisu anavyoamini na anasema anachokianmini tofauti na wengi wa viongozi wetu wengi wanaojifanya ni waumini wa Mwalimu wakati hawaishi yale aliyoyaamini Mwalimu, ni wezi, walafi, wabinafsi, mafisadi, wanyonyaji kama walivyo wajumbe wa bunge la katiba kule Dodoma. Najua angekuwepo Mwalimu leo lile bunge la katiba lingekuwa limesha sambaratishwa kwa sababu ule ni mradi wa kufisidi kodi za wavuja jasho wa nchi hii ulioratibiwa na Ikulu yenyewe - hakika ni wizi mtupu - shame upon you.
Wewe ndivyo unaamini, lakini Nyerere hajatukanwa wala kukashfiwa!... TUNDU LISU kasema ukweli.
 
Ndugu nimekuelewa vizuri.

Mimi huwa ninasema, CHADEMA kimejengwa ndani kwa misingi ya kilaghai. Wawe wanaohoji na kutaka kuufahamu ukweli wakiwa ndani ya CHADEMA kama viongozi au wananchama, huwa wanalazimishwa kujiuzuru au wanaishia kufukuzwa. Hii ndiyo CHADEMA.

Wewe mnafiq, kama chadema ni walaghai? HUYO Edwin Mtei umemwaminije?
 
Hivi kwanini tunakuwa wanafiki. Hakuna watu wanaomsema vibaya na kumtukana Nyerere "off record" kama viongozi wa CCM, hasa kipindi cha 1995-2005. Hata sasa, Nyerere kusemwa vibaya na kutukanwa na makada wa ccm huko juu ni jambo la kawaida. Majina yapo, ushahidi upo.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hebu tuache kurumbana juu ya Nyerere. Maana yeye aliijenga inchi yetu ya wakati huo vyema kulingana na mazingira duni ya wakati huo. Tumefaidi matunda yake, tunamshukuru kwa kutuonesha njia, ametukabidhi inchi ikiwa shwari. Leo tunajadili ni namna gani tutaijenga inchi yetu itakayoendana na wakati tulionao na ujao. Hayo ya Lisu ni mchango wake na maoni tu. Sio lazima yachukuliwe japo hata yeye ana nia ile ile ya kujenga.
 
Huoni kuwa huu ni unafiki uliopitiliza kwa hawa viongozi wa CHADEMA kutumia picha ya kiongozi wanayemfahamu kuwa ni muongo na mdanganyifu na alilidanganya taifa kwa muda mrefu na taifa limeendelea "kudanganyika".

Haijalishi Nyerere alikuwa Muongo au Mkweli. Nyerere atabaki kuwa BABA WA TAIFA LA TANGANYIKA na sio Tanzania.
Pia mimi CHADEMA, wewe CCM, yule wa CUF, yule wa NCCR na wengineo wooote haituzuii kutumia picha ya Baba wa TAIFA. Nyerere ni Baba wa Taifa na sio baba wa CCM. Nasema hivyo kwa sababu vyama vingi vimekuja baadae sana ila sisi wote ni uzao wa TANU kwa uongozi wa nyerere. Kwahiyo kama sisi wote ni uzao wa TANU pia vyama vyote ni uzao wa TANU au ujukuu wa TANU kwahiyo Mbowe kutumia picha ya baba wa Taifa sio haramu.
 
Back
Top Bottom