Mzurulaji
JF-Expert Member
- Sep 25, 2021
- 280
- 566
X Alikuwa Ni mwanamke niliompenda kwa dhati, niliachana naye kizembe sana na hakutaka kurudiana na mimi. Nakumbuka baada ya kuona simuelewi elewi, niliandaa mpango mzima wa kumtia wivu ili akumbuke wajibu wake ni nini.
Niliandaa mpango wa watu wake wa karibu wampe taarifa niko kwenye mahusiano mengine, kitu ambacho si cha kweli lengo ni kumtia wivu na arejee kwangu kwa Speed ya 4G. Lengo la mpango huu ndio ulienda kuharibu kila kitu, maana nilitahamaki baada ya kumuona akija maghetoni huku akiwa amefula sana. Hakutaka hata kukaa alizungumza huku akiwa amesimama.
"Kabla sijatoka na wewe niliwahi kuwa kwenye mahusiano pia, sikutaka kuingia kwenye mahusiano na wewe kwa miguu yote, sababu nilishaumizwa na sikutaka kuumia zaidi. Niseme tu ahsante kwa upendo wako ila sitoweza kushare na mtu yoyote"
Kisha akaondoka tangu siku hiyo namba yake kila muda alikuwa anatumika, njiani ananikwepa, nilimfukuzia sana arudi maishani mwangu na kuwasihi watu wake wa karibu wamwambie ukweli, ajabu wao wanadai hata jina langu hakutaka kulisikia. Mwisho wa siku familia yao nzima walihama mkoa jirani baada ya baba yake kuhamishwa kikazi maana alikuwa mwalimu mkuu katika shule X.
Shuka na wewe Juto gani? ambalo lilishakutokea na ukajutia katika maisha yako ya kimahusiano.......
Niliandaa mpango wa watu wake wa karibu wampe taarifa niko kwenye mahusiano mengine, kitu ambacho si cha kweli lengo ni kumtia wivu na arejee kwangu kwa Speed ya 4G. Lengo la mpango huu ndio ulienda kuharibu kila kitu, maana nilitahamaki baada ya kumuona akija maghetoni huku akiwa amefula sana. Hakutaka hata kukaa alizungumza huku akiwa amesimama.
"Kabla sijatoka na wewe niliwahi kuwa kwenye mahusiano pia, sikutaka kuingia kwenye mahusiano na wewe kwa miguu yote, sababu nilishaumizwa na sikutaka kuumia zaidi. Niseme tu ahsante kwa upendo wako ila sitoweza kushare na mtu yoyote"
Kisha akaondoka tangu siku hiyo namba yake kila muda alikuwa anatumika, njiani ananikwepa, nilimfukuzia sana arudi maishani mwangu na kuwasihi watu wake wa karibu wamwambie ukweli, ajabu wao wanadai hata jina langu hakutaka kulisikia. Mwisho wa siku familia yao nzima walihama mkoa jirani baada ya baba yake kuhamishwa kikazi maana alikuwa mwalimu mkuu katika shule X.
Shuka na wewe Juto gani? ambalo lilishakutokea na ukajutia katika maisha yako ya kimahusiano.......