Kipanya: Kulikoni tena!

Kipanya: Kulikoni tena!

Kibonzo hicho kinaweza kuwa na maana nyingi, lakini kwa ujumla kinachora picha ya hali ya kisiasa nchini Tanzania, hasa kati ya vyama vya CCM na Chadema.

Mtu aliyechimba kaburi na kuingia humo akichota maji anaweza kuashiria juhudi za kuondoa matatizo au changamoto zilizopo, lakini pia kuna uwezekano wa kuwa anajitafutia matatizo zaidi kwa kujiingiza katika hatari.

Hali hii inaweza kutafsiriwa kama juhudi za kuleta mabadiliko katika mazingira magumu.

Kwa upande mwingine, mwanachama wa CCM anayelala pembeni anaweza kuashiria utepetevu au kutokujali hali iliyopo, ambayo inaweza kuwa ni kielelezo cha watu walio katika madaraka kutokuwa na hamu ya kushughulikia matatizo ya wananchi.

Katika muktadha wa kauli za "no reform, no elections" kutoka kwa Chadema na wengine wanaosema kuna uchaguzi, kibonzo hicho kinaweza kuwakilisha mgawanyiko wa mawazo kwenye chama.

Wengine wanataka mabadiliko ya kweli kabla ya uchaguzi, huku wengine wakiona uchaguzi kama njia ya kuleta mabadiliko, bila kujali mfumo wa kisasa.

Hivyo, kibonzo hiki kinaweza kuwa kielelezo cha mgawanyiko wa mawazo na hisia kuhusu mwelekeo wa kisiasa na hali ya demokrasia nchini Tanzania.
 
Sehemu kubwa ya kaburi na mchanga vinawakilishwa na rangi ya wazee wa no reforms no election ivyo ni chadema.

Shati la 🌲ni chama kilichoshika hatamu.

Mtu aliyedumbukia kaburini ni afisa mipango wa chama kinachowakilishwa na ilo shati ambapo kwa mtego walioutega walitegemea kukiua chama kinachowakilishwa na rangi ya hiyo ardhi na kukizika humo, kwa bahati mbaya matarajio yamekua ni magumu na kaburi linajaa maji ikiwa ni ishara ya marehemu aliyetarajiwa kufa mpk sasa yupo hai.

Kutumbukia kwa mtu na kutoa maji kaburini inaweza kuwa ni ishara mpya ya kujaribu kutengeneza matatizo na misuguano mipya ndani ya chama ili kukitetelesha na kukiua na hatimaye kaburi lipate marehemu wa kuzikwa umo .

Wingi wa maji kwenye kaburi ukilinganisha na yaliyofanikiwa kutolewa ni ishara ya uimara wa chama mpinzani unaopelekea mtoa maji kucheka kwa kuona kazi iyo ni ngumu na inaweza ikamchosha anayeyatoa maji kaburini.
Nyumbu wamejiingiza kwenye shida kweli kweli ya kiakili.......hawana jingine wanalowaza zaidi ya unyumbu wao. Poleni.
 
1744083655985-png.3296618

Magulification must go on
 
Kila mtu anatafsi yake!
KIjani baada ya kupandikiza G55 wanajaribu tena kusafisha kaburi kuona kama wanaweza kuizika Khak!
 
Itapendeza ukitoa tafsiri yako
Tafsiri yangu ni, wenye nguo za kijani mbinu yao si maiti iisubiri kaburi, ni kaburi lisubiri maiti. Meaning makaburi yao wanayachimba mapema halafu yanakaa wazi yakisubiri maiti.

Sasa mhusika yu mahututi, kaburi linapaswa kuwa wazi tayari kwa kupokea maiti, mchimbaji anayaondoa maji na anafurahia hiyo hali sababu alijiandaa mapema kwa kichimba kaburi, kuchimba ni kugumu kuliko kuondoa maji.

Mhusika asipofariki, kaburi litabaki wazi likiendelea kusubiri.
 
Sehemu kubwa ya kaburi na mchanga vinawakilishwa na rangi ya wazee wa no reforms no election ivyo ni chadema.

Shati la 🌲ni chama kilichoshika hatamu.

Mtu aliyedumbukia kaburini ni afisa mipango wa chama kinachowakilishwa na ilo shati ambapo kwa mtego walioutega walitegemea kukiua chama kinachowakilishwa na rangi ya hiyo ardhi na kukizika humo, kwa bahati mbaya matarajio yamekua ni magumu na kaburi linajaa maji ikiwa ni ishara ya marehemu aliyetarajiwa kufa mpk sasa yupo hai.

Kutumbukia kwa mtu na kutoa maji kaburini inaweza kuwa ni ishara mpya ya kujaribu kutengeneza matatizo na misuguano mipya ndani ya chama ili kukitetelesha na kukiua na hatimaye kaburi lipate marehemu wa kuzikwa umo .

Wingi wa maji kwenye kaburi ukilinganisha na yaliyofanikiwa kutolewa ni ishara ya uimara wa chama mpinzani unaopelekea mtoa maji kucheka kwa kuona kazi iyo ni ngumu na inaweza ikamchosha anayeyatoa maji kaburini.
Shukrani bwana Kipanya, ila michoro yako inakuwaga migumu sn kuitafsiri, kwnn?
 
Hii ni series Ndefu sana Faana
Yaani inabidi Ucheze na Matukio yote..

Ilianza Hivi..
20250408_081342.jpg


Ikaja Hivi..
20250408_081358.jpg


Ikaja Kuwa Hivi..
20250408_081406.jpg


Ikafikia Huku
20250408_081347.jpg


Sasa Imefika Huku
20250408_081857.jpg



Maana Yake walichokiandaa Mwanzoni Kilielekea Kusua sua ila kwa Sasa Kinaelekea Kukamilika na Ndo maana Anatoa Maji kujiandaa
 
Baada ya Chadema kuingia kwenye uchaguzi wa ndani ... Huyu jamaa mwenye shati la kijani

Alichimba makaburi yake akijua lazima tu huu mvutano baina ya hizo pande mbili zitawatengenezea kulikuwa chama

Lakini baada ya hoja kutibu majeraha na kuvuka salama ... Maana makuburi yake yakageuka kuwa kama swimming pool

Baada ya G55 kuibuka tenaaa

Jamaa kaona usinichezee acha nitoe maji kwenye kaburi maana Tumaini la chama kuingia kwenye mauti ni kubwa 🤣
Hii Ni Tafsiri Yangu Kwa leo imeenda Na Matukio Yote
 
Unganisha dots uchaguzi ndani ya CDM na hili kundi jipya la waasi wa G55 ndani ya CDM. Hilo shati ni jezi ya CCM maana yake anayesuka mipango yote ya kuidhoofisha CDM ni CCM japokuwa ule uliosukwa kipindi cha uchaguzi ulifeli. Je, safari hii huu mkakati CCM waliokuja nao wa kuanzisha waasi wa G55 ndani ya CDM utafaulu? Ndio maana jamaa anatoa hayo maji huko shimoni akitegemea chochote kitaikumba CDM.
 
Back
Top Bottom