Kipanya: Katuni hii imekataliwa na mhariri

Kipanya: Katuni hii imekataliwa na mhariri

Huu ni ukweli ambao ni mwiba kwa waandishi wa habari waliokiuka misingi na maadili ya taaluma zao kwa ajili ya vijisenti vya wanasiasa......
Wapo waandishi waliokuwa stadi kuwachafua au pengine kufichua maovu ya wanasiasa na ni waandishi hao hao waliochukua jukumu la kubeba kalamu zao mithili ya dodoki kuwasafisha hao hao wanasiasa....kwa maslahi yao huku wakiuacha umma ukiwa njia panda....
Mkuu hawa jamaa wamejisahau kwamba wanatakiwa kuweka mbele maslahi ya umma sio wanasiasa.
 
Samahani mkuu isomeke: waandishi wanatumiwa na wanasiasa ili kutimiza matakwa yao
 
KUna mwandishi alishawahi kuwatukana jamaa na kuwaita day prostitutes (malaya ya mchana). Mara nyingi hawapo kwa ajili ya kuwajulisha watu ukweli, huwajulisha watu kile mambwana zao wanachotaka watu wajue, na sio vinginevyo. Ukienda kinyume, you are fired
kocha wa inter milan kipindi hicho, Jose Mourinho, aliwaambia waandishi wa habari wanafanya 'intellectual prostitution' kutokana na kufanya kazi zao kishabiki shabiki sana
Mourinho rails against 'intellectual prostitution'
 
Looh huu ujumbe umekuja kwa wakati, Magufuli ni mwanasiasa ambaye ni Rais wa Tanzania na Ayub mwandishi wa habari nguli alietegemewa kwa uchumbuzi wa masuala mbalimbali ya kijamii.

Je Ayub atatimiza matakwa ya aliempa Ukurugenzi au atabakia kuwa mwanataaluma ya uandishi.

Tujikumbushe mwandishi mwingine wa kuheshimika katika habari Salva aliekuwa mwiba kwa utawala wa Mkapa kupitia gazeti lao la Rai alipoteuliwa kwenda Ikulu alitimiza matakwa ya mwanasiasa aliemchagua au alifanya kazi yake kitaaluma.

Nauliza tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom