Kipanya kalewa sifa na kukosa uzalendo sasa

Kipanya kalewa sifa na kukosa uzalendo sasa

Avanti

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2010
Posts
1,209
Reaction score
240
Katika katuni yake ya leo anasema "Hiyo ndege iliyopotea bora ingekuwa imebeba wajumbe wa bunge la Katiba".
Naamini hii ni kulewa sifa na kukosa ubinadamu kabisa. Siku zote napenda katuni zake lakini hii hapana!
 
HIVI WEWE UNALIANGALIAGA BUNGE LA KATIBA?
MAMBO WANAJADILI KWA USHABIKI WA KICHAMA NA KUACHA MAMBO MUHIMU,
MPAKA JANA KILA MJUMBE WA BUNGE LA KATIBA AMEPOKEA POSHO YA SH MILIONI KUMI
ndugu fikiri tofauti
 
Katika katuni yake ya leo anasema "Hiyo ndege iliyopotea bora ingekuwa imebeba wajumbe wa bunge la Katiba".
Naamini hii ni kulewa sifa na kukosa ubinadamu kabisa. Siku zote napenda katuni zake lakini hii hapana!

Yuko sahihi kwani wewe huoni upuuzi wanaotufanyia?Wametumia fedha zetu nyingi halafu wanajadili upuuzi.
 
Tena ingekubeba wewe pamoja na wanafiki wenzio wote ndo ingekuw poa zaidi
 
Huo msemo niliuandika hapa JF juzi nikisema kuna jamaa yangu kanitumia sms anasema ni heri ile ndege ya malaysia ingepotea na wabunge wa bunge la Katibakuliko wale raia wasio na hatia.........kama hivyo ndivyo basi aongeze ubunifu maana msg ya huo msemo naona wanayo wengi.
 
jamaa anaongea ukweli tatizo ni kuwa wale wajumbe ni wanadamu km sisi kuwaombea wapotee ni sawa na kuwahukumu wafe kitu ambacho ni dhambi kwa Mwenyezi Mungu.
 
Yuko sahihi, angeongeza mtu mmoja kati ya wajumbe wote...na kikwete angekuwamo humo na ikapotea milele
 
Katika katuni yake ya leo anasema "Hiyo ndege iliyopotea bora ingekuwa imebeba wajumbe wa bunge la Katiba".
Naamini hii ni kulewa sifa na kukosa ubinadamu kabisa. Siku zote napenda katuni zake lakini hii hapana!

Nadhani umemwelewa kwa mtazamo huo ila mimi kwa upande wangu nimeelewa kua hayo ni maneno ya wananchi kupitia katuni hiyo na inaonyesha ni kiasi gani wananchi wamechoshwa na kukerwa na maigizo yanayoendelea bungeni huku kodi zetu zikiteketea.

Kwa hiyo mdau, nionavyo mimi, hayo si maneno ya Kipanya ila ni ya wananchi. Kipanya kayawasilisha tu.

Huu ni mtazamo wangu pia.
 
Katika katuni yake ya leo anasema "Hiyo ndege iliyopotea bora ingekuwa imebeba wajumbe wa bunge la Katiba".
Naamini hii ni kulewa sifa na kukosa ubinadamu kabisa. Siku zote napenda katuni zake lakini hii hapana!

Yuko sahihi kabisa ktk hili,koz wanachokifanya hakistahili kabisa
 
Wewe ni mbunge wa bunge la katiba............?......

Mimi sio lakini madhara ya kupotea ndege yanajulikana ni kwamba wale watu walikufa kwa hiyo na hawa wabunge ina maana ni bora wafe kivile? Huu sio ubinadamu sasa
 
Katika katuni yake ya leo anasema "Hiyo ndege iliyopotea bora ingekuwa imebeba wajumbe wa bunge la Katiba".
Naamini hii ni kulewa sifa na kukosa ubinadamu kabisa. Siku zote napenda katuni zake lakini hii hapana!

Kipanya ana haki na uhuru wa kuongea kama Mtanzania mwengine kupitia katuni zake. Hayo ni maoni yake, hajamtukana mtu haina shida kabisa kama hujaipenda wewe bahati mbaya, hata hizo unazoipendaga wewe kunawengine huwa zinawudhi. Kuna mambo mengi ya msingi ya kujadili
 
Back
Top Bottom