Kiongozi anapoteua Watu wa kuzurura nao

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,555
41,066
Nchi yetu bado ni miongoni mwa nchi 50 maskini sana Duniani, yenyewe ikishikila nafasi ya 27 kwa umaskini, huku Burundi ikishika nafasi ya kwanza katika Dunia, na DRC nafasi 5 Duniani. Kwa kiasi kikubwa umaskini huu unaochangiwa na uongozi mbaya, uongozi usio na maono wala uthubutu.

Kiongozi aliyevunja rekodi ya Afrika kwa kuzurura na watu wengi Duniani anapoenda kwenye mataifa mengine ni Mobuto Seseko, aliyekuwa Rais wa DRC (wakati huo Zaire). Huyu alikuwa akizurura kwenye mataifa mengine akiwa na wapambe wa kuzurura naye wapatao 200. Kama uzururaji wa kiongozi mkuu wa nchi na kundi kubwa la watu kungekuwa kunaondoa umaskini, basi DRC pengine ilistahili kuwa nchi ya 5 kwa maendeleo badala ya kuwa nchi ya 5 kwa umaskini Duniani.

Wakati wa utawala wa awamu ya 4, kiongozi mkuu wa nchi alipewa jina la Rais mtalii na wakati mwingine Vasco Dagama, kwa sababu ya wakati wote kufanya utalii kwenye mataifa mengine. Lakini angalao alikuwa na timu ndogo ya watu aliokuwa anatalii nao.

Kiongozi wetu wa sasa anatafuta kuvunja rekodi ya kuzurura na kundi kubwa la watu kwenye mataifa mengine. Safari yake ya India, aliteua watu wa kuzurura nao wapatao 100, wote wakitumia kodi za Watanzania, walio wengi wakiishi kwenye umaskini kiasi hata cha kushindwa kuhudhuria hata baadhi ya misiba ya ndugu zao kwa kukosa nauli. Lakini kodi yao, kiongozi wao hana machungu nayo, anaamua kuitumbua kwa starehe pamoja na wale aliowateua kwa wakati husika.

Sijui kiongozi kwa kuzurura huko nje na kundi kubwa la watu, anataka kutatua nini. Labda kwa sababu watu wamekuwa wakimlaumu kwa safari zake zisizo na tija, sasa ameamua kwenda na watu wengi, kuzurura nao, kutumbua pesa ya umma, kula vinono na starehe mbalimbali, ili hawa watu baada ya kuonjeshwa starehe zote huko nje, aone kama baada ya kurudi wataendelea kusema kuwa kuzurura nje ni kubaya. Au watasifia kuzurura kwenye mataifa mengine ili waendelee kukumbukwa kwenye starehe hizo za kuzurura kwa gharama ya wananchi.

Rekodi ya kwanza ya kuzurura nje na kundi kubwa la watu kwa pesa ya umma, ilivunjwa kipindi cha awamu ya pili mwaka 1992, ambapo kiongozi mkuu wa nchi alienda na ujumbe wa watu wapatao 90 huko Rio de Janeiro, nchini Brazil, ambapo kundi kubwa la hao watu hawakuingia hata kwenye ukumbi wa mikutano, badala yake waliishia kwenye maduka makubwa kufanya shopping. Wakarudi toka huko, hata wasijue mkutano wenyewe ulikuwa unahusu nini.

Walivyotua uwanja wetu wa ndege walipoulizwa ulikuwa ni mkutano wa nini, wakasema kuwa ulikuwa ni mkutano wa Mazingira, kitu kilichoashiria kuwa walikuwa ni watu wajinga kabisa ambao walishindwa hata kuelewa kuwa mkutano huo ulikuwa ni wa SUSTAINABLE DEVELOPMENT, ambao ndani yake, mazingira ilikuwa component tu. Miaka mitano baadaye, UNDP ilishangazwa na Tanzania kushindwa kutekeleza hata azimio moja la maazimio ya Rio de Janeiro.

Sababu ilikuwa ni dhahiri, kiongozi alienda kuzurura na kundi kubwa la wazururaji ambao kwao kilichokuwa muhimu ni kupata nafasi ya kutumbua kodi.

Rekodi hii ya awamu ya pili ya kuzurura na kundi kubwa nje, leo inavunjwa na bintiye.

Rais Mkapa aliwahi kusema:
"Kama kukitokea kiongozi yeyote akakuambia kuwa huko nje kuna pesa nyingi inayoweza kuiletea Tanzania maendeleo, mwambie mjinga wewe"
 
Huyo ni wa kwenu. Mimi mama yangu ni dalali wa viwanja vikubwa kabisa nchini ambapo kuna wafugaji aliowaona washamba walifukuzwa.
Mama mdogo sijui anafanya kazi gani ila kuna jambo anataka awatumikie wajomba zake anawafanyia mpango awamilikishe bure chanzo kikuu cha mapato cha familia.
 
Kila kitu in excess ni ubatili. Kula kupita kiasi ni ulafi lakini kula ni hitaji la lazima.
Kwamba FISI wale Kwa urefu wa kamba!!!

Pia kula inategemea ukubwa wa tumbo , appetite na capacity ya kutanuka misuli ya tumbo.


Acha tuchezee viboko akili zitukae sawa.
 
Nchi yetu bado ni miongoni mwa nchi 50 maskini sana Duniani, yenyewe ikishikila nafasi ya 27 kwa umaskini, huku Burundi ikishika nafasi ya kwanza katika Dunia, na DRC nafasi 5 Duniani. Kwa kiasi kikubwa umaskini huu unaochangiwa na uongozi mbaya, uongozi usio na maono wala uthubutu.

Kiongozi aliyevunja rekodi ya Afrika kwa kuzurura na watu wengi Duniani anapoenda kwenye mataifa mengine ni Mobuto Seseko, aliyekuwa Rais wa DRC (wakati huo Zaire). Huyu alikuwa akizurura kwenye mataifa mengine akiwa na wapambe wa kuzurura naye wapatao 200. Kama uzururaji wa kiongozi mkuu wa nchi na kundi kubwa la watu kungekuwa kunaondoa umaskini, basi DRC pengine ilistahili kuwa nchi ya 5 kwa maendeleo badala ya kuwa nchi ya 5 kwa umaskini Duniani.

Wakati wa utawala wa awamu ya 4, kiongozi mkuu wa nchi alipewa jina la Rais mtalii na wakati mwingine Vasco Dagama, kwa sababu ya wakati wote kufanya utalii kwenye mataifa mengine. Lakini angalao alikuwa na timu ndogo ya watu aliokuwa anatalii nao.

Kiongozi wetu wa sasa anatafuta kuvunja rekodi ya kuzurura na kundi kubwa la watu kwenye mataifa mengine. Safari yake ya India, aliteua watu wa kuzurura nao wapatao 100, wote wakitumia kodi za Watanzania, walio wengi wakiishi kwenye umaskini kiasi hata cha kushindwa kuhudhuria hata baadhi ya misiba ya ndugu zao kwa kukosa nauli. Lakini kodi yao, kiongozi wao hana machungu nayo, anaamua kuitumbua kwa starehe pamoja na wale aliowateua kwa wakati husika.

Sijui kiongozi kwa kuzurura huko nje na kundi kubwa la watu, anataka kutatua nini. Labda kwa sababu watu wamekuwa wakimlaumu kwa safari zake zisizo na tija, sasa ameamua kwenda na watu wengi, kuzurura nao, kutumbua pesa ya umma, kula vinono na starehe mbalimbali, ili hawa watu baada ya kuonjeshwa starehe zote huko nje, aone kama baada ya kurudi wataendelea kusema kuwa kuzurura nje ni kubaya. Au watasifia kuzurura kwenye mataifa mengine ili waendelee kukumbukwa kwenye starehe hizo za kuzurura kwa gharama ya wananchi.

Rekodi ya kwanza ya kuzurura nje na kundi kubwa la watu kwa pesa ya umma, ilivunjwa kipindi cha awamu ya pili mwaka 1992, ambapo kiongozi mkuu wa nchi alienda na ujumbe wa watu wapatao 90 huko Rio de Janeiro, nchini Brazil, ambapo kundi kubwa la hao watu hawakuingia hata kwenye ukumbi wa mikutano, badala yake waliishia kwenye maduka makubwa kufanya shopping. Wakarudi toka huko, hata wasijue mkutano wenyewe ulikuwa unahusu nini.

Walivyotua uwanja wetu wa ndege walipoulizwa ulikuwa ni mkutano wa nini, wakasema kuwa ulikuwa ni mkutano wa Mazingira, kitu kilichoashiria kuwa walikuwa ni watu wajinga kabisa ambao walishindwa hata kuelewa kuwa mkutano huo ulikuwa ni wa SUSTAINABLE DEVELOPMENT, ambao ndani yake, mazingira ilikuwa component tu. Miaka mitano baadaye, UNDP ilishangazwa na Tanzania kushindwa kutekeleza hata azimio moja la maazimio ya Rio de Janeiro.

Sababu ilikuwa ni dhahiri, kiongozi alienda kuzurura na kundi kubwa la wazururaji ambao kwao kilichokuwa muhimu ni kupata nafasi ya kutumbua kodi.

Rekodi hii ya awamu ya pili ya kuzurura na kundi kubwa nje, leo inavunjwa na bintiye.

Rais Mkapa aliwahi kusema:
"Kama kukitokea kiongozi yeyote akakuambia kuwa huko nje kuna pesa nyingi inayoweza kuiletea Tanzania maendeleo, mwambie mjinga wewe"
Wanaenda shopping ya Xmas na mwaka mpya.
 
Safari za viongozi zinaratibiwa na watu wa PROTOKALI....

Kwa kuwa ni majukumu yao tungewauliza maswali yafuatayo:-

-Je Rais wa nchi hapewi nafasi moja ya mume/mke ?!!

-Ikiwa mume/mke hatokwenda naye je nafasi hiyo haiwezi kujazwa na MTOTO mkubwa ?!!

Haya maswali ni vema yakajibiwa na wanadiplomasia wa protokali.....

Kuhusu kijana mwenzetu Abdul.....

Tunajuaje kama alikuwa na safari yake binafsi na AKALIPA nauli ya kwenda India.....WHO KNOWS?!!

#SiempreJMT
 
Nchi yetu bado ni miongoni mwa nchi 50 maskini sana Duniani, yenyewe ikishikila nafasi ya 27 kwa umaskini, huku Burundi ikishika nafasi ya kwanza katika Dunia, na DRC nafasi 5 Duniani. Kwa kiasi kikubwa umaskini huu unaochangiwa na uongozi mbaya, uongozi usio na maono wala uthubutu.

Kiongozi aliyevunja rekodi ya Afrika kwa kuzurura na watu wengi Duniani anapoenda kwenye mataifa mengine ni Mobuto Seseko, aliyekuwa Rais wa DRC (wakati huo Zaire). Huyu alikuwa akizurura kwenye mataifa mengine akiwa na wapambe wa kuzurura naye wapatao 200. Kama uzururaji wa kiongozi mkuu wa nchi na kundi kubwa la watu kungekuwa kunaondoa umaskini, basi DRC pengine ilistahili kuwa nchi ya 5 kwa maendeleo badala ya kuwa nchi ya 5 kwa umaskini Duniani.

Wakati wa utawala wa awamu ya 4, kiongozi mkuu wa nchi alipewa jina la Rais mtalii na wakati mwingine Vasco Dagama, kwa sababu ya wakati wote kufanya utalii kwenye mataifa mengine. Lakini angalao alikuwa na timu ndogo ya watu aliokuwa anatalii nao.

Kiongozi wetu wa sasa anatafuta kuvunja rekodi ya kuzurura na kundi kubwa la watu kwenye mataifa mengine. Safari yake ya India, aliteua watu wa kuzurura nao wapatao 100, wote wakitumia kodi za Watanzania, walio wengi wakiishi kwenye umaskini kiasi hata cha kushindwa kuhudhuria hata baadhi ya misiba ya ndugu zao kwa kukosa nauli. Lakini kodi yao, kiongozi wao hana machungu nayo, anaamua kuitumbua kwa starehe pamoja na wale aliowateua kwa wakati husika.

Sijui kiongozi kwa kuzurura huko nje na kundi kubwa la watu, anataka kutatua nini. Labda kwa sababu watu wamekuwa wakimlaumu kwa safari zake zisizo na tija, sasa ameamua kwenda na watu wengi, kuzurura nao, kutumbua pesa ya umma, kula vinono na starehe mbalimbali, ili hawa watu baada ya kuonjeshwa starehe zote huko nje, aone kama baada ya kurudi wataendelea kusema kuwa kuzurura nje ni kubaya. Au watasifia kuzurura kwenye mataifa mengine ili waendelee kukumbukwa kwenye starehe hizo za kuzurura kwa gharama ya wananchi.

Rekodi ya kwanza ya kuzurura nje na kundi kubwa la watu kwa pesa ya umma, ilivunjwa kipindi cha awamu ya pili mwaka 1992, ambapo kiongozi mkuu wa nchi alienda na ujumbe wa watu wapatao 90 huko Rio de Janeiro, nchini Brazil, ambapo kundi kubwa la hao watu hawakuingia hata kwenye ukumbi wa mikutano, badala yake waliishia kwenye maduka makubwa kufanya shopping. Wakarudi toka huko, hata wasijue mkutano wenyewe ulikuwa unahusu nini.

Walivyotua uwanja wetu wa ndege walipoulizwa ulikuwa ni mkutano wa nini, wakasema kuwa ulikuwa ni mkutano wa Mazingira, kitu kilichoashiria kuwa walikuwa ni watu wajinga kabisa ambao walishindwa hata kuelewa kuwa mkutano huo ulikuwa ni wa SUSTAINABLE DEVELOPMENT, ambao ndani yake, mazingira ilikuwa component tu. Miaka mitano baadaye, UNDP ilishangazwa na Tanzania kushindwa kutekeleza hata azimio moja la maazimio ya Rio de Janeiro.

Sababu ilikuwa ni dhahiri, kiongozi alienda kuzurura na kundi kubwa la wazururaji ambao kwao kilichokuwa muhimu ni kupata nafasi ya kutumbua kodi.

Rekodi hii ya awamu ya pili ya kuzurura na kundi kubwa nje, leo inavunjwa na bintiye.

Rais Mkapa aliwahi kusema:
"Kama kukitokea kiongozi yeyote akakuambia kuwa huko nje kuna pesa nyingi inayoweza kuiletea Tanzania maendeleo, mwambie mjinga wewe"
Walioko ndani ya ccm wengi ni zao la juzi tu, hata misingi ya kuanzishwa kwa ccm hawajui, wapo so far wapo kwenye uongozi, machungu ya ukombonzi kutoka katika minyororo ya ukoloni hawajui, na mbaya hata kusoma vitatu vya history hawana mda,

Kuwa na fikra wapi taifa lifike baada ya miaka mia ijayo kwao ni kama mpigia mbuzi gitaa, hawajui leo wapo kesho hawatakuepo bali vitakuepo vizazi vingine, so hujiaminisha ni wateule wa mungu kwao kifo ni mwiko.

Fuatilia ziara za rais wa Zambia, simple ila zenye maana kubwa katika nchi yake.

The only solution ni ccm kuondoka madarakani na ilisha kuwa ni swala la mda tu.
 
Safari za viongozi zinaratibiwa na watu wa PROTOKALI....

Kwa kuwa ni majukumu yao tungewauliza maswali yafuatayo:-

-Je Rais wa nchi hapewi nafasi moja ya mume/mke ?!!

-Ikiwa mume/mke hatokwenda naye je nafasi hiyo haiwezi kujazwa na MTOTO mkubwa ?!!

Haya maswali ni vema yakajibiwa na wanadiplomasia wa protokali.....

Kuhusu kijana mwenzetu Abdul.....

Tunajuaje kama alikuwa na safari yake binafsi na AKALIPA nauli ya kwenda India.....WHO KNOWS?!!

#SiempreJMT
Safari yake wapi wewe, shida viongozi wa kiafrika wakisha kuwa basi kila mwanafamilia ni kiongozi, na nchi huongozwa kama shamba la babies tu,
 
Back
Top Bottom