Kiongozi anapoonekana anajua kila kitu

Kiongozi anapoonekana anajua kila kitu

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,769
Reaction score
288,331
Wanyakyusa wanasema: "Indalama syalile Juta", yaani Fedha ilimla au ilimuua Yuda [Iskarioti]! Tanzania ya leo, mtu mwenye pesa na mamlaka anaweza kumfundisha na kumuamrisha hata Askofu Mkuu au Mufti katika mambo ya imani hata kama mtoa amri hana hata Cheti cha Theologia au Tauhidi! Ole wake Askofu Mkuu au Mufti akatae, kesho yake anaweza kukuta migogoro kwenye Taasisi yake yenye lengo la kutaka kumng'oa na akipona hiyo, Taasisi yake itawekewa vikwazo katika kupata vibari maalum ikiwemo hata kunujua viwanja!

Hata kama hana Cheti cha Fundi Mchundo (Technician), lakini mtu mwenye Fedha na mamlaka anaweza kutoa maelekezo ya kitaalam kwa Mhandisi (Engineer) mwenye Shahada ya Uzamivu. Ole wake Mhandisi akosoe! Hata kama hana hata Cheti cha Uhasibu Ngazi ya Msingi, mtu huyo anaweza kutoa maelekezo kuhusu utalaam wa Fedha kwa Mhasibu mwenye Cheti za Ubingwa katika Uhasibu (CPA, ACCA, CIMA).

Hata kama hana hata Astashahada ya Kodi, mtu mwenye mamlaka na Fedha anaweza kumfundisha namna ya kupanga mfumo wa Kodi mtu ambaye ni Mkadiliaji wa Kodi (Tax Assessor) mwenye Shahada ya Ubingwa masuala ya Fedha na Kodi (MSc in Fiscal Studies/Policies). Hata kama hana Cheti cha Sheria kutoka Chuo cha Lushoto, mtu huyo anaweza kumpangia namna ya kutafsiri Sheria Jaji Mkuu. Hata kama hana hata Cheti cha masuala ya Siasa na Utawala, mtu huyo anaweza kumfundisha taaluma ya siasa mbombezi aliye Profesa wa Sayansi ya Siasa na Utawala.

Ikifikia hatua hiyo, jamii au nchi inakoma kufuata maadili ya uongozi na mifumo ya uendeshaji nchi (Katiba), bali inaongozwa kwa utashi wa viongozi. Kiongozi anachukuliwa kuwa anajua kila kitu. Taratibu na Kanuni za Kazi na uendeshaji nchi hukoma, badala yake Taasisi na nchi huongozwa kwa matamko. Wakurugenzi huacha kufuata miongozo na kanuni za kazi, badala yake kila siku husubiri matamko ya viongozi na watawala! Watu huanza kuabudu Fedha, vyeo na wenye madaraka. Haki anageuka kuwa kaburi la marehemu asiyekuwa na ndugu ambalo haliwezi hata kufagiliwa.

Hivi ni malaika gani atakayeshuka kutoka mbinguni ili kulionya Taifa la namna hii? Je, ni Gabrieli (Jibrili), Raphael au Mikaeli? Ole wao kizazi kisichosikia sauti na dhamiri ya Mungu kupitia kwa watumishi wake (Ezekieli 33:1-20).

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Mkuu Bandekile Mwamakula

34436676-5455-409A-968C-AC0FB0256D9F.jpeg
 
Kujua kila kitu ni jambo zuri sana kama kweli mtu anajua. Inawezekana kabisa mtu akawa anafanya assessment ya ufanisi katika mambo mbalimbali yanayofanyika chini yake, na kwa bahati mbaya watu wanaofanya hayo mambo wako shallow kuliko kiongozi wao. Kingozi bora ama atahitaji kuinua viwango vya watu wake ili wafanye sahihi kama atawahitaji kuwa nao kwa muda mrefu, ama atawakosoa na kuwangoza katika ufanisi bora wa majukumu hayo kwa wakati ule.

Hakuna mantiki ya kuacha kukosoa uharibifu ama ubovu wa watendaji wa chini wanapokosea mara nyingi kwa kuogopa kwamba utaonekana "Unajua/unapinga/unakosoa kila kitu". Lazima vitu vibovu vikosolewe hata kama ni mara zote as long as viko chini ya viwango . Haijalishi mkosoaji ni yule yule, taasisi ni ile ile ama namna gani so long as mkosoaji anajua, na ama anahakikisha mambo yanaendeshwa kwa viwango.
Kujua kila kitu si tusi na si uharifu. Wako watu wanajua mambo mengi sana na si uungwana wakinyamaza kimya huku waliokabidhiwa (kwa kuwa hawawezi kufanya kila kitu), wanavurunda.

Ninachokifahamu kukataa kukosolewa ni tatizo la watu wajinga, wanaoamini katika unafiki, wivu ama hila za kutaka kumkwamisha mkosoaji ama kupitisha mambo maovu, au kukosa upeo.

Hoja hapa, ni pale kiongozi anapotumia madaraka kuamurisha namna ya utendaji wa masuala ambayo hana ufahamu nayo. Yaani mwanasiasa, anaamurisha ratios za concrete na mchanga kweny ujenzi wa madaraja, mwenye pesa anataka kupanga number za wachezaji uwanjani wakati hajui, au mwenye cheo atumie cheo chake kuongoza watu namna ya kuabudu Mungu wao wakati yeye hamjui huyo Mungu na imani ile. Huo unaitwa UJINGA WA UONGOZI.

KICHWA CHA HABARI, KABADILISHWE ILI KI AKSI DHANA KWAMBA VIONGOZI WAJIFANYE KUJUA MASUALA AMBAYO HAWANA UJUZI NAYO. Kujua kila kitu ni vizuri sana, lakini kujifanya kujua vitu ambayo mtu havijui kwa kuwa ni kiongozi, ni uharibifu na haikubaliki.
 
Kuna mkemia aliwahi kushauri kuanzishwa kwa somo la Historian ya Tanzania huku tayari lipo somo la Historia linafundishwa mashuleni! R.I P JPM
 
Hivi ni malaika gani atakayeshuka kutoka mbinguni ili kulionya Taifa la namna hii? Je, ni Gabrieli (Jibrili), Raphael au Mikaeli? Ole wao kizazi kisichosikia sauti na dhamiri ya Mungu kupitia kwa watumishi wake (Ezekieli 33:1-20).[emoji1545][emoji1534][emoji1545][emoji1534][emoji1545][emoji1534]
 
Kuna mkemia aliwahi kushauri kuanzishwa kwa somo la Historian ya Tanzania huku tayari lipo somo la Historia linafundishwa mashuleni! R.I P JPM
Mpaka leo najiuliza hivi aliwaza nini yule kiumbe!
 
Samahani kwa kukukosoa lakini ukweli ni kwamba hakuna cheti cha Tawhid kwenye Uislam.

mtu mwenye pesa na mamlaka anaweza kumfundisha na kumuamrisha hata Askofu Mkuu au Mufti katika mambo ya imani hata kama mtoa amri hana hata Cheti cha Theologia au Tauhidi!
 
TOO MUCH KNOW, Yesu alitembea na mke wake kwenda kuhesabiwa!
Dawa zinatusaidia kutibu maradhi mbalimbali lakini zikitumiwa nyingi na kwa muda mrefu huathiri mfumo wa ufahamu na ubongo pia
 
Kuna mkemia aliwahi kushauri kuanzishwa kwa somo la Historian ya Tanzania huku tayari lipo somo la Historia linafundishwa mashuleni! R.I P JPM

yalikuwa ni maandalizi ya kutengeneza historia ya jiwe bahati nzuri akafutika yye na historia yake
 
Back
Top Bottom