King'amuzi gani ni bora ukiacha DSTV

King'amuzi gani ni bora ukiacha DSTV

Ba Loreen

Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
75
Reaction score
14
Wapendwa wanajamvi. Kwa sasa kuna ving'amuzi kadhaa wa kadha vinatangazwa ila ubora wake wa channeli na Resolution pia usasa wake ni muhimu kuzingatia. Ningependa wanaovijua vyema wanijuze ili nijiunge. DSTV ni nzuri lakini gharama za kila mwezi nazo zinakwaza. HizoContinental, Digitek, Easy TV, Ting, Startimes, na zingine kama zipo ipi ni zaidi?

Natanguliza shukrani.
 
ZUKu kaka, July wanaingiza channel za English Premier League kama ni mpenzi wa haya maswala
 
Kwanza interest yako ni nini kwenye TV?
Maigizo ya bongo,movie,taarifa ya habari,muziki
 
star times mie sikushauri hata kidogo maana kwa sasa vinascratch kama cd iliyokwisha hata raha hakuna,picture quality yao wala sio nzuri na pia hata programs sio nzuri saana! Pia hata program info hawana ili kuweza kujua ni kipindi gani na kinahusu nini. Ila they're the cheapest.
Upande wa dstv japokuwa bei zao zipo juu kidogo lakini they're the best na ukiangalia bundle zao zipo za kawaida kama compact na compact plus(kama ni mpenzi wa epl). Compact ni around 48 elfu hivi wakati inayoitwa the best kwa star times ni 40000 plus low picture quality!
Pia kwa dstv unaweza kuseti reminder kwa tv program zijazo hata kwa cku 3 zijazo so hapo hupitwi kitu ambacho star times hakuna! Go for dstv and am sure you wont regret it
 
siku zote kwenye hii mambo bei pekee ndio inayoamua. mkuu kama uko vizuri ni DSTv pekee hutojuta na kupata presha za mara kwa mara. hizi startimes ni kifafa any time chaliiiii.
 
TING! JAPO KUNUNUA ILE SET NZIMA NI GHALI, LAKINI WANA FREE CHANELS ZA NYUMBANI KAMA TBC1, CH 10, STAR TV, NA ITV....KAMA ni mpenzi wa soka za ulaya zipo channels, lakini pia malipo yao kwa mwezi ni buku 15
 
40,000/= sio mchezo jamani labda kwa wapenzi wa fooootbolu,hebu tupeane uzuri wa hii DIGTEK ni vipi maana ninayo Startimes ila nimelipia napata sauti tu hela inaendelea kuliwa naangalia nichukue DIGTEK au ZUKU
 
DSTV wakiziweka tv za nyumbani zote hawatakuwa na mpinzani kwani wazamaji wengi wanapenda michezo
 
Kwanza interest yako ni nini kwenye TV?
Maigizo ya bongo,movie,taarifa ya habari,muziki


Mkuu Belo, kwa mtu mwenye interest na Action Movies... unamshauri achukue king'amuzi gani? mbali na DSTV.

-Kaveli-
 
DSTV wakiziweka tv za nyumbani zote hawatakuwa na mpinzani kwani wazamaji wengi wanapenda michezo
Leo hii 2017 DSTV wana channel karibia zote za Tanzania

E
TBC
ITV
Clouds
Star TV
Chanel Ten
 
Back
Top Bottom