habari ni njema mkuu.
Ila next time usinikweze kiasi hicho, mkuu wetu ni Maulid Baraka wa Kitenge,
mimi sistahili hata kufunga gidhamu za viatu vyake.
Sawasawa?
aaah mkuu?
Usifike mbali hivyo, kwani kuna vingine vya umeme kaka?
Hahahaha,..
Kamuulize Thabit Abdul mtoto wa Ilala a.k.a mchawi wa kinanda a.k.a mkono wa nini sijui
au muulize Alan Mapigo a.k.a Mapigiyaniyeno.
drums je?
zikipigwa kama unapoenda rock music, huezi acha kutingisha mguu, kichwa, mwishowe mwili mzima unaitikia.
Nina wasi wasi na utamu wa kinanda unaouongelea hapa
Isije ikawa wamaanisha mengine wakati sisi tunakijua kinannda cha kawaida aise
kinanda mara zote mlio wake hutegemea zaidi vidole vya mpigaji,mimi hapa naona sifa ziende kwenye vidole zaidi cuz bila vidole hakuna mlio ati...msikikweze kinanda bure
ahaa?
Kwa hiyo sifa kisipewe kinanda, apewe mpigaji, au vidole vyake, sio?
Je, mpigaji huyuhuyu tunaweza kumpa kifaa/ala nyingine tofauti na kinanda na akaleta utamu ule ule kama aliouleta through kinanda?
Sasa hapo inategemea na kipaji na utaalam wa mpigaji katika kuvishughulisha vidole vyake,maana wapo watu mahiri kuvitumia vidole hivyo hivyo katika ala mbali mbali,kama ngoma,gitaa,filimbi n.k.kwa hiyo ndio au hapana yote yaweza kuwa majibu
mambo ya do-re-mi-fa-so-ra-ti-do.do-ti...........Hakuna siri kubwa,vyombo haviwez kuwa sawa vyote.Kinanda babalao.
O o oh, knanda!raha yake kubwa ni ujuz wa mshka nyuz ajue kupanda na kushuka co kushka sehem ile ile ktapoteza radha!
kinanda kina nyuzi tena dadangu?
Najua ni weekend, lakini taratibu bwana. Afu hapa hata hatumaanishi vinanda vyenu hivyo.
Hapa tunachambua kinanda kama ala ya muziki.
Kuna siri gani ndani yake?