WanaJF!
Katibu mkuu wa CCM, bwana Kinana, amefanya kweli kwa kuitimiza dhamira yake ya kumpeleka mchungaji Msigwa mahakamani endapo mchungaji huyo atakaidi fursa ya kumuomba radhi bwana Kinana.
Bwana Kinana alitoa fursa hiyo ya kuombwa radhi kufuatia kuchafuliwa taswira yake kwenye jamii, baada ya kudaiwa kuwa yeye ana jihusisha na masuala ya ujangili, jambo ambalo amelikanusha vikali.
Mchungaji Msigwa ameonekana mahakamani siku ya tar 14 akiwa na mawakili Tundu Lissu na Bwana Kibatala kama watetezi wa upande wa mshtakiwa.
My take,
Nilikuwa nasubiri kwa hamu sana kesi hii ya kumshtaki mchungaji Msigwa kwa tabia yake ya kuropoka ovyo ovyo. Shukrani bwana kinana kwa hatua uliyo chukua. Sasa kazi kwa Msigwa kuthibitisha tuhuma zake za ujangili kwa bwana Kinana.