Kama unataka kutumia hoja hiyo kumtia hatiani bwana Kinana basi nisewe umepotoka, mahakamani kesi haziamuriwi kwa kutumia ushahidi mwepesi hivyo.
Itakumbukwa kuwa Kinana ni shareholder wa hiyo kampuni ya Sharaf shipping, na ukiwa shareholder haimaanishi una husika na day to day operations za kampuni. Kampuni inakuwa na management na shareholder wapo kwa ajili ya ku-finance na ku-enjoy dividends, sasa iweje Kinana ahusishwe na ujangili au usafirishaji wa pembe za ndovu?, hapo wa kuhusishwa moja kwa moja ni watendaji wa kampuni ya Sharaf shipping na watu wa TRA.
Kuhusu mfano wako; pale Bilicanas kuna vijana uwa wanakamatwa na polisi kwa kubwia unga, je nikisema Mbowe ahusishwe na unga kwa kuwa yeye ni mmiliki wa bilicanas utanielewa?, ni sawa sawa na ndege inavyo wasafirisha "punda" au wabeba unga, huwezi kumuhusisha owner wa ndege kuwa yeye ana husika, ila utawahusisha wale wakaguzi wa airport, nadhani umeelewa mkuu.