Kinana aivuruga Lumumba

Kinana aivuruga Lumumba

Wasilalamike, ni wazi kuwa CCM ndiyo imeasisi, kubariki na kuachia utaratibu wa viongozi kujiamulia kufanya wanayotaka. Ni serikali ya CCM iliyotupa kando uwajibikaji na maadili ya viongozi wa umma. Ni CCM na viongozi wake waliofikia hatua ya kuzidharau sheria na kukiuka katiba ya nchi kwa manufaa yao.

CCM ni chama pekee ambapo watu wenye kashfa za ubakaji kama Prof. Kapuya wanaweza kupeta na vyeo vyao bila kubughudhiwa na yeyote. Ni katika CCM ambapo kiongozi anayetuhumiwa na umma anaweza kugombea uongozi wa umma huku akipigiwa kampeni na Mwenyekiti wa chama hicho bila aibu!

Tena ni katika CCM na serikali yake ambapo kiongozi anaweza kuwaamuru polisi au jeshi kuvunja sheria na kutoheshimu katiba, na asiulizwe na yeyoye. Ni katika serikali ya CCM ambapo wahalifu wateule kama Kamuhanda wanaweza kupandishwa vyeo, pamoja na mauaji waliyoyasimamia kuwa na ushahidi wa wazi!

Kwani wao walitegemea nini kutokana na chama chao? Tell them to sit tight. Katika CCM kila kisichowezekana kwingineko kinawezekana kwao. Kila kisichoruhusiwa kwingine ndani ya CCM ni ruksa!

Neno moja lenye maana sawa na maelezo yako yote ni 'Mbugi '
 
Kinana kawashika pabaya sana machadema. Enzi za kinana, hakuna chama cha upinzani kitakachotamba
 
hahahaaaaa anakagua Ngozi za wanyama huebda zikawa dili nazo baada ya nanihiii kuwa aghali
 
Wasilalamike, ni wazi kuwa CCM ndiyo imeasisi, kubariki na kuachia utaratibu wa viongozi kujiamulia kufanya wanayotaka. Ni serikali ya CCM iliyotupa kando uwajibikaji na maadili ya viongozi wa umma. Ni CCM na viongozi wake waliofikia hatua ya kuzidharau sheria na kukiuka katiba ya nchi kwa manufaa yao.

CCM ni chama pekee ambapo watu wenye kashfa za ubakaji kama Prof. Kapuya wanaweza kupeta na vyeo vyao bila kubughudhiwa na yeyote. Ni katika CCM ambapo kiongozi anayetuhumiwa na umma anaweza kugombea uongozi wa umma huku akipigiwa kampeni na Mwenyekiti wa chama hicho bila aibu!

Tena ni katika CCM na serikali yake ambapo kiongozi anaweza kuwaamuru polisi au jeshi kuvunja sheria na kutoheshimu katiba, na asiulizwe na yeyoye. Ni katika serikali ya CCM ambapo wahalifu wateule kama Kamuhanda wanaweza kupandishwa vyeo, pamoja na mauaji waliyoyasimamia kuwa na ushahidi wa wazi!

Kwani wao walitegemea nini kutokana na chama chao? Tell them to sit tight. Katika CCM kila kisichowezekana kwingineko kinawezekana kwao. Kila kisichoruhusiwa kwingine ndani ya CCM ni ruksa!

Ndugu yangu ni ukweli usiofichika ktk chama hiki. Mf Mwenyekiti wao aliwahi kusema ana majina ya majangili wanaoua tembo wetu, ameshindwa nn kuwataja au kuyakabidhi ktk vyombo husika? Waziri ktk Wizara ya Maliasili na Utalii akihitimisha hotuba ya wizara yake hapo jana alisema hakuna ushahidi wakuwakamata majangili. Je yale meno yote yaliokamatwa sio ushahidi? Wakubal tu kwamba CCM ina wenyewe na wenye chama ndio MAJANGILI. Nawaomba ndugu zetu wa CCM watambue kwamba uzalendo umewashinda eti kwakuwa tu serikali iliyoko madarakani ni mali yao, watambue pia kuwa Nchi ni ya Wanzania wote na sio mali yao (ccm).
 
Ndugu yangu ni ukweli usiofichika ktk chama hiki. Mf Mwenyekiti wao aliwahi kusema ana majina ya majangili wanaoua tembo wetu, ameshindwa nn kuwataja au kuyakabidhi ktk vyombo husika? Waziri ktk Wizara ya Maliasili na Utalii akihitimisha hotuba ya wizara yake hapo jana alisema hakuna ushahidi wakuwakamata majangili. Je yale meno yote yaliokamatwa sio ushahidi? Wakubal tu kwamba CCM ina wenyewe na wenye chama ndio MAJANGILI. Nawaomba ndugu zetu wa CCM watambue kwamba uzalendo umewashinda eti kwakuwa tu serikali iliyoko madarakani ni mali yao, watambue pia kuwa Nchi ni ya Wanzania wote na sio mali yao (ccm).

Tatizo ni kuujisahau au kulewa madaraka. Kwamba kuna watu wanadhani CCM itatawala milee. Vinginevyo sidhani kama tena wanafikiria hata kabla ya kuongea jambo. Jambo moja wasemaji watano, kila mtu na lake. Leo Rais ana orodha ya wauza madawa ya kulevya, kuwakamata hapana! Kesho ana listi ya majangili, kuwashitaki...haiwezekani! Kuna mtu anayefikiria kuwa maana ya hilo ni kuwa rais ni muhalifu? Kwa sababu kisheria huwezi kusaidiana na jangili wewe usiwe jangili. Kisheria wakati jangili anashtakiwa, wewe pia unashtakiwa, ila kwa kosa la kusaidiana na majangili! Huyo ndiyo Rais wetu na mawaziri wake!

Limekuja hili la mwaka Meno ya tembo kibao yanakamatwa kila siku. Wahusika hawaonekani! Ukiwauliza watakwambia hii ni idara ya wanyama pori inafanya kazi yake. Hivi kuna anayejua kati yao kuwa kitendo cha kukamatwa kwa meno ya tembo, bila wahalifu kila mara, ni dalili ya uchafu uliokithiri? Kwamba ni aidha majangili yanaachiwa kwa kutoa rushwa, au yanaachiwa kwa amri za viongozi flani? Au huenda hakuna jangili wala meno yanayokamatwa kabisa. Ni meno yanachukuliwa ghalani, yanakwenda kupandwa eneo, kisha yanatangazwa na kupewa publicity tu ili muone wanachapa kazi. Ni kweli siyo rahisi watu kushtuka, lakini ni mbinu hiyohiyo polisi wamekuwa wakiitumia kila siku. Tangu lini polisi akawa na tabia ya kupanda kwenye media kila siku? Na kama wahalifu wandhibitiwa kiasi hicho mbona hawaishi mitaani? Na kama ni kweli polisi ina uwezo kiasi hicho mbona wahalifu wanaojulikana kabisa wanazunguka tu mitaani baada ya kuachiwa bila maelezo ya kutosha?

Najua kuna siku itafika. Siku ambayo udhalimu utafika mwisho. Na siku hiyo ikifika, nawahakikishia wengi wa mnaowaita viongozi, watakimbia Nchi hii kwa kuhofia kuwajibishwa kwa makosa yao! Hiyo ndiyo siku ninayoingojea kwa hamu.
 
Kaileta mh Mbowe hiyo, ni mpira wa miguu ila mchezaji yeyote anafunga kokote, hamna sheria zinazofuatwa, hata usipovaa jezi sawa tu. Ndio ccm, yeyote anasema chochote popote
 
Vijana wa lumumba wana njaa kali sana hasa ukizingatia kwamba ajira hakuna.
 
Kuna sintofahamu katika Ofisi Ndogo za CCM-Lumumba kuhusu ziara zinazoendelea za Katibu Mkuu wa CCM,Kanali Mstaafu Abdurahman Kinana. Patashika hiyo ya kichama ni kuhusu hasa timu inayoambatana na Kinana katika ziara za mikoani.Makada waandamizi wa Lumumba wanadai kuwa ziara za Kinana hazilengi kuimarisha chama kama zinavyoonekena ila ni kujitangaza na kuwatangaza anaoambatana nao ili kujiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwakani.

"Werevu tunajua.Katibu Mkuu na timu yake wako katika kujitangaza na kujitafutia umaarufu wa kisiasa. Hakuna jipya ambalo wanalifanya. Ndiyo maana hata timu yake haibadiliki.Ni kwamba amechagua vijana wa kuwatangaza na wengine kuwatenga. Kwanini timu haibadiliki? Kwani nani hawezi kuhutubia na nani hataki posho?" aliuliza kwa kulalama kada mmoja maarufu aliyehamia CCM katika miaka ya karibuni.

"Ziara za Katibu Mkuu zitaleta ubaguzi chamani na mpasuko usio na maana. Chama hakiimarishwi na watu wale wale kila siku.Kila kada anaweza kwenda mikoani na kukitangaza chama. Kwanini wale wale hata kama wanaonekana kusema mambo ya kawaida sana? Tunajiandaa kuchukua hatua juu ya hili" alidakia kada mwingine wa Ofisi Ndogo Lumumba

Nionavyo,lengo kuu ni posho na umaarufu. Kumbe!??

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Kwani hawa akina Shonza et al hawajui kuwa CCM ina wenyewe? Watambue kuwa wao walitumika kama condom na sasa ni makapi yasiyofaa mbele ya CCM ... Mtabwabwaja sana lakini angalieni huko huwa wanavuta kucha na kung'oa meno ikibidi! ...
 
Kinana anatisha.

Kinena hana lolote zaidi ya kuuwa Tembo wetu. Kama anajidanganya kufanya kampeni ili kugombea Urahisi wa nji hii mwaka 2015 basi anapoteza muda wake bure! Kwanza ameshatutukana Watanzania kwa kutuita MAEMBE kwa vile tu tunawashabikia wapinzani!

Hatuwezi kukubali nchi ya Watanganyika itawaliwe na Nyang'au la Kisomali. Never ever! Kama anataka urahisi wa kula nchi kwa kuuza pembe za Ndovu arudi kwao Somalia au akajiunge na Al-shaabab!!
 
Haha..nidhani ni kiboko ya CDM km wanavyojitangaza kumbe ni kiboko ya CCM?
 
Back
Top Bottom