Kuna sintofahamu katika Ofisi Ndogo za CCM-Lumumba kuhusu ziara zinazoendelea za Katibu Mkuu wa CCM,Kanali Mstaafu Abdurahman Kinana. Patashika hiyo ya kichama ni kuhusu hasa timu inayoambatana na Kinana katika ziara za mikoani.Makada waandamizi wa Lumumba wanadai kuwa ziara za Kinana hazilengi kuimarisha chama kama zinavyoonekena ila ni kujitangaza na kuwatangaza anaoambatana nao ili kujiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwakani.
"Werevu tunajua.Katibu Mkuu na timu yake wako katika kujitangaza na kujitafutia umaarufu wa kisiasa. Hakuna jipya ambalo wanalifanya. Ndiyo maana hata timu yake haibadiliki.Ni kwamba amechagua vijana wa kuwatangaza na wengine kuwatenga. Kwanini timu haibadiliki? Kwani nani hawezi kuhutubia na nani hataki posho?" aliuliza kwa kulalama kada mmoja maarufu aliyehamia CCM katika miaka ya karibuni.
"Ziara za Katibu Mkuu zitaleta ubaguzi chamani na mpasuko usio na maana. Chama hakiimarishwi na watu wale wale kila siku.Kila kada anaweza kwenda mikoani na kukitangaza chama. Kwanini wale wale hata kama wanaonekana kusema mambo ya kawaida sana? Tunajiandaa kuchukua hatua juu ya hili" alidakia kada mwingine wa Ofisi Ndogo Lumumba
Nionavyo,lengo kuu ni posho na umaarufu. Kumbe!??
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Hii post ukiisoma kwa ndani ni uoga kutoka upande wa pili wa shilingi kwa maana ukawa and companies,kama mtakuwa wafuatiliaji kuna kipindi mzee kinana aliposhila ukatibu mkuu alifanya ziara mbili na baadaye kukaa kimya,wengi mlijitokeza na kuhoji ziara za kinana zipo wapi ? Hali hiyo ilijitokeza kwa kudhani ilikuwa nguvu ya soda,sasa inawatisha wengi,kinana anapiga kazi maeneo mbalimbali,anakagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na kuwasilikiza wananchi.Amefanikiwa kuibua ari ya wana ccm kutambua wajibu wao na hii itasaidia hata katika ngazi nyingine za mikoa na wilaya mpaka kata na matawini viongozi wa ccm kufanya majukumu yao na kutokana na kuwa chama chenye mtandao mpana na madhubuti,itakuwa ni vigumu kwa vyama vya ushindani kupenyeza umbeya na propaganda katika jamii