Negotiator
JF-Expert Member
- Aug 9, 2010
- 303
- 44
Upinzani ukituzidi tutawatumia Mwinyi, Mkapa-Kinana
Mwenyekiti wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi
Mwenyekiti wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa watashiriki kampeni za Rais Jakaya Kikwete iwapo kitazidiwa na upinzani.
Taarifa ya Kinana ilitolewa jana kwa niaba yake na mjumbe wa kamati ya kampeni za CCM, Dk. Raphael Chegeni alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Kinana alisema hali ya kampeni ilivyo sasa inaashiria kuwa mambo yanakwenda vizuri.
"Sio kwamba mgombea wetu ametengwa na marais wastaafu, tunaona chama hakijazidiwa na wapinzani hivyo hakuna sababu ya kuwasumbua mzee Mwinyi na Mkapa," alisema.
Pia alisema CCM inamtambua mshindi wa kura za maoni kuwania ubunge wa jimbo la Nzega mkoani Tabora, Hussein Bashe.
Bashe alishinda kura za maoni lakini Kamati Kuu (CC) ya CCM ilimuengua kwa kile kilichodaiwa kwamba si raia wa Tanzania.
Alisema CCM ipo tayari kumtumia Bashe katika shughuli mbalimbali za chama, ikiwemo kusaidia kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu.
SOURCE; NIPASHE http://www.ippmedia.com/frontend/index.php?l=21247
Mwenyekiti wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi
Mwenyekiti wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa watashiriki kampeni za Rais Jakaya Kikwete iwapo kitazidiwa na upinzani.
Taarifa ya Kinana ilitolewa jana kwa niaba yake na mjumbe wa kamati ya kampeni za CCM, Dk. Raphael Chegeni alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Kinana alisema hali ya kampeni ilivyo sasa inaashiria kuwa mambo yanakwenda vizuri.
"Sio kwamba mgombea wetu ametengwa na marais wastaafu, tunaona chama hakijazidiwa na wapinzani hivyo hakuna sababu ya kuwasumbua mzee Mwinyi na Mkapa," alisema.
Pia alisema CCM inamtambua mshindi wa kura za maoni kuwania ubunge wa jimbo la Nzega mkoani Tabora, Hussein Bashe.
Bashe alishinda kura za maoni lakini Kamati Kuu (CC) ya CCM ilimuengua kwa kile kilichodaiwa kwamba si raia wa Tanzania.
Alisema CCM ipo tayari kumtumia Bashe katika shughuli mbalimbali za chama, ikiwemo kusaidia kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu.
SOURCE; NIPASHE http://www.ippmedia.com/frontend/index.php?l=21247