Kinachowaangusha vijana wetu huko mamtoni/ ughaibuni

Kinachowaangusha vijana wetu huko mamtoni/ ughaibuni

nzalendo

Platinum Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,901
Reaction score
14,611
Naam vijana wetu na watoto wetu pia wajukuu huamua kufunga safari na kwenda nchi za mbali katika kujitafutia riziki,

Wengi huenda kwa njia ya kupata Elimu na baadae huamua kufanya kazi,,,wengine huenda kama kutembea na kujilipua nk nk wengine hupata Green Card kwa wale wa magharibi ya mbali.

Sasa ukweli ni kwamba,,wengi wana maisha magumu sana sana tofauti na tunavyodhani,

NItajaribu kutoa simulizi chache......

Kuna kijana mmoja alifika magharibi ya mbali kama mwanafunzi akapata degree yake akaunga na Masters na kupata kibarua saafi cha kumuwezesha kumudu maisha.

KIjana kwa bakhti mbaya alipata mtihani katika mahusiano,,,kapata mwanamke...na katika nchi ya magharibi ya mbali...mwanamke ni adui namba moja ya mwanaume.

Wakajaaliwa mtoto.....mwanamke katunga ya kutunga baada ya kumchoka jamaa.....jamaa akazushiwa ya kuzushiwa kesi juu ya kesi.....mwishowe.....mahakama ikaamuru jamaa awe analipa kila mwezi matumizi ya mtoto(wenyewe wanaita child support)

Huku na kule akapata mwanamke mwingine wa kupooza....ghafla nae akajaaliwa kupata mtoto,,,,,,yakamkuta ya kumkuta nae kwa amri ya mahakama akalazimika kutoa child support.

kutokana na hali ya mazingira pengine upweke n.k kijana akawa na kitu kama depression akatumbukia kwenye ulevi wa kupindukia akapoteza kazi,,

Kurudi nyumbani anaona aibu,,maana hana kitu,,,,kula yake ni food bank(misosi ya bure) kulala kwake ni shelter,,,inatia uchungu lakini ndio hali halisi,,,huku nyumbani,,,,,,"Tuna kijana wetu yupo magharibi ya mbali".....
 
Kurudi nyumbani anaona aibu,,maana hana kitu,,,,kula yake ni food bank(misosi ya bure) kulala kwake ni shelter,,,inatia uchungu lakini ndio hali halisi,,,huku nyumbani,,,,,,"Tuna kijana wetu yupo magharibi ya mbali".....
Kijana alikua na malengo yenye ndoto safi kasoma kapata kazi maisha yakaanza vizuri ila hao wanawake aliojivuruga nao ndio wamemchafulia malengo angejua asingejivuruga kua nao angeishia kuwanunua tu kwani huko si wapo wanaouza bila kupigwa mimba maana hakuna masuala ya child support na wanauza shingapi? ameshindwa kununua na kupiga na kupita hivi mpaka anavuta ndani wanamgeuzia kibao kumbe wote wauzaji tu wametegesha mimba wanataka walipwe sasa huko km sio kujiuza ni nini?
 
Naam vijana wetu na watoto wetu pia wajukuu huamua kufunga safari na kwenda nchi za mbali katika kujitafutia riziki,

Wengi huenda kwa njia ya kupata Elimu na baadae huamua kufanya kazi,,,wengine huenda kama kutembea na kujilipua nk nk wengine hupata Green Card kwa wale wa magharibi ya mbali.

Sasa ukweli ni kwamba,,wengi wana maisha magumu sana sana tofauti na tunavyodhani,

NItajaribu kutoa simulizi chache......

Kuna kijana mmoja alifika magharibi ya mbali kama mwanafunzi akapata degree yake akaunga na Masters na kupata kibarua saafi cha kumuwezesha kumudu maisha.

KIjana kwa bakhti mbaya alipata mtihani katika mahusiano,,,kapata mwanamke...na katika nchi ya magharibi ya mbali...mwanamke ni adui namba moja ya mwanaume.

Wakajaaliwa mtoto.....mwanamke katunga ya kutunga baada ya kumchoka jamaa.....jamaa akazushiwa ya kuzushiwa kesi juu ya kesi.....mwishowe.....mahakama ikaamuru jamaa awe analipa kila mwezi matumizi ya mtoto(wenyewe wanaita child support)

Huku na kule akapata mwanamke mwingine wa kupooza....ghafla nae akajaaliwa kupata mtoto,,,,,,yakamkuta ya kumkuta nae kwa amri ya mahakama akalazimika kutoa child support.

kutokana na hali ya mazingira pengine upweke n.k kijana akawa na kitu kama depression akatumbukia kwenye ulevi wa kupindukia akapoteza kazi,,

Kurudi nyumbani anaona aibu,,maana hana kitu,,,,kula yake ni food bank(misosi ya bure) kulala kwake ni shelter,,,inatia uchungu lakini ndio hali halisi,,,huku nyumbani,,,,,,"Tuna kijana wetu yupo magharibi ya mbali".....
“ghafla naye akajaliwa kupata mtoto” hizi huwa ni juhudi za kutotaka kubeba responsibility kwamba kama mwanaume alizingua kuzalisha hovyo.

Maisha ya ughaibuni hayataki watu wasio na uwezo wa kupanga na kuchagua mambo.

Pole yake kwa changamoto, aende rehab akasaidike na hiyo alcoholism, sivyo soon mtachangishana hela ya kumrudisha akiwa ndani ya sanduku.
 
Yani huyo jamaa yako mmoja ndio anakufanya uanzishe uzi kwa kusema ''Vijana wetu?" ungeandika ''Kijana wetu'' umetumia wingi kwa kuwasilisha tatizo la mtu mmoja,

Huja jamaa yako ameingia kwenye matatizo yakujitakia,Child support inawaumiza wengi sana.
 
Kaka yetu alienda kama chokoraa, akabahatija kupata kazi, ajapata mtaji akaanza biashara, baadae akawa tajiri mkubwa, na hata hapa bongo amewekeza kwa sana tu, ndiye mmiliki wa StoneL====!
Huyo wa kwenu bakini naye
 
Mbona hiyo child support hata hapa bongo ipo? Mdada akikupeleka dawati lazima uzitoe Kama Yule IGP Mstaafu omari mahita- kijasho kilimtoka house girl alivyo mpeleka dawati/ustawi wa jamii… matunzo ya Mtoto.

Kuna kipondi Paul Makinda Bashite alitangaza msako wa wababa wasiolipa child support, pressure ilikuwa juu sana kwa akina baba, sijui yale mambo yaliishia wapi?

We sema tu lengo la uzi wako lilikuwa kusema kwamba wanawake ni sumu… hivyo tu basi tusiwaguse…
 
Hao vijana wa kwenu ila hapa kwetu vijana kibao wapo SA na home kwao wamebadilisha maisha pakubwa tu
 
Back
Top Bottom