Kinacho fanywa na mawakala wa TRA

Kinacho fanywa na mawakala wa TRA

Sidhani kama mkuu unachosema kina ukweli wowote. Mimi napita hapo si chini ya mara 16 kwa siku na ni kila siku. Sijawahi ona kitu kama hicho.
IMG-20170707-WA0009.jpg
 
Sio vibaya kama wanakagua risiti, ni kweli kasi ya kutoa na kudai risiti imepungua sana, hivyo kama hili linafanywa ni ubunifu mzuri na ni vyema ukaendelezwa.
 
Wamenisimamisha kwenye taa sa Sarender Bridge, wakasema wanataka wakague Mafuta. Akaangalia gauge kwenye dashboard akakuta kuna nusu tank, akauliza risiti. Nikamuuliza risiti ya nini? Eti ya nilijiwekea mafuta. Uzuri nilikuwa nayo, akaisoma kisha akaondoka.
Swali:-
Je huu ni utaratibu rasmi wa TRA au ndio utapeli na upigaji mpya jijini?
Wataalamu wa sheria watusaidie maanake siamini haya matamko ya TRA yana mashiko kisheria ndo maana wakawekwa TRA ili wakusanye sio jukumu la mteja au mtumiaji kuchukua risiti.

Kuchukua risiti ni haki yako sio wajibu kama mtumiaji

Na kutoa risiti ni wajibu sio haki yako kama muuzaji

Wataalamu wa sheria watusaidie hapa

Na kwa ushauri serikali inatakiwa ielimishe watu umuhimu wa kuchukua risiti na sio kulazimisha wanachi wachukue risiti kilazima
 
Wanaforce mambo kuna mawakala wanalazimisha leseni na kadi ya gari vifanane majina ilikujua wanaonunua bila kubadili majina hii nimeiona Mbeya.
Wanasahau mtu unaweza endesha gari si lako hlf hata mwenyenayo humjui.
 
Wamenisimamisha kwenye taa sa Sarender Bridge, wakasema wanataka wakague Mafuta. Akaangalia gauge kwenye dashboard akakuta kuna nusu tank, akauliza risiti. Nikamuuliza risiti ya nini? Eti ya nilijiwekea mafuta. Uzuri nilikuwa nayo, akaisoma kisha akaondoka.
Swali:-
Je huu ni utaratibu rasmi wa TRA au ndio utapeli na upigaji mpya jijini?

Upuuzi mtupu
 
Ila ni sawa... Kama wanahimiza kila unachonunua dai risiti... Kwa nini usichukue risiti ya mafuta...



Cc: mahondaw
Na wale wanaenda guest mchana wanapewa risiti ?

Tuendako hata ukitoa sadaka kanisani/msikitini watasema dai risiti,
 
Sidhani kama mkuu unachosema kina ukweli wowote. Mimi napita hapo si chini ya mara 16 kwa siku na ni kila siku. Sijawahi ona kitu kama hicho.
Kutoona kwako hakumfanyi mtoa mada kuwa muongo jadili swali lake wewe si kipimo cha ukweli labda uwe tra
 
Heeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee makubwa kama nilijaza full tank na receipt nikapeleka kudai changu mavi kabisa aisee kweli ndio akili za makinikia zimetua huku kweli tutayaona mengi mno.......... Just stay turn
 
Sidhani kama mkuu unachosema kina ukweli wowote. Mimi napita hapo si chini ya mara 16 kwa siku na ni kila siku. Sijawahi ona kitu kama hicho.
Ngoja mpaka kikukute. Ila kwa tahadhari ukijaza mafuta kituoni hakikisha unapewa risiti na unaitunza kwenye gari lako vinginevyo Tsh 30,000 zitakutoka na huchomoki kaka.
 
Miaka yote hapa jf nimekuamini Bujibuji lakini kwa hili kama nabisha vile! Kama kweli wana muda huo kwa nini wasiwe wanaangalia mashimo yaliyojaa mabarabarani!
 
Sidhani kama mkuu unachosema kina ukweli wowote. Mimi napita hapo si chini ya mara 16 kwa siku na ni kila siku. Sijawahi ona kitu kama hicho.
kwa sasa wew chukua funzo ayo mengine yakikukuta ndo utajua hujawah ona watu wanaibiwa daily lakini wengine hawajui hata kuibiwa ni nini
 
Sidhani kama mkuu unachosema kina ukweli wowote. Mimi napita hapo si chini ya mara 16 kwa siku na ni kila siku. Sijawahi ona kitu kama hicho.
Ni kweli. TRA wapo katika zoezi la kukagua kama wauzaji wa mafuta watatoa risiti na pia kama wanunuzi wanadai na kupewa risiti. Ukiuza toa risiti na usinunue dai risiti.
 
Wale tunaonyonya mafuta kwenye SU na STK itakuaje sijui
 
Back
Top Bottom