Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kama kuna kitu kimeanza kunigusa pabaya katika fikra zangu ni kauli za mara kwa mara za wale wanaotajwa kuwa ni viongozi wa zamani wa taifa letu ambao hutoa kauli mbalimbali za kujaribu kuonesha kuwa nchi imefika pabaya. Kauli za hivi karibuni za aliyekuwa Waziri Mkuu Bw. Joseph Warioba na zile za aliyewahi kuwa Waziri na Mkuu wa Mkoa kwa muda mrefu na Mdhamini wa CCM Bw. Paul Kimiti zinanifanya nianze kuona kuwa kama taifa tunaanza kuchezewa akili na wale ambao waliwahi kuwa viongozi.
Lakini vile vile kauli za aliyekuwa Rais wa Tanzania Mzee Ally Hassan Mwinyi kuhusu masuala ya madawa ya kulevya na viongozi wa dini nazo zinanifanya niamini kabisa kuwa viongozi wetu hawa wa zamani wanaishi katika ulimwengu wa wale wanaokana. Yaani, wale ambao hawajakaa chini na kuangalia ni kwa jinsi gani maamuzi yao wao wenyewe ndio yamelifikisha taifa letu leo hii.
Wazee hawa wanapozungumza japo inaonekana kana kwamba ni katika uzalendo ukweli ni kwamba wanajaribu kujitenga na matendo na misimamo yao wakati walipokuwa madarakani. Ndugu zangu, leo hii tunalipia hatia yao. Wanayo hatia na wakati umefika waanze kukiri hatia hiyo na kuliomba taifa letu msamaha na wawajibike kwa kuanza kukaa kimya.
SOMA ZAIDI HAPA:
Lakini vile vile kauli za aliyekuwa Rais wa Tanzania Mzee Ally Hassan Mwinyi kuhusu masuala ya madawa ya kulevya na viongozi wa dini nazo zinanifanya niamini kabisa kuwa viongozi wetu hawa wa zamani wanaishi katika ulimwengu wa wale wanaokana. Yaani, wale ambao hawajakaa chini na kuangalia ni kwa jinsi gani maamuzi yao wao wenyewe ndio yamelifikisha taifa letu leo hii.
Wazee hawa wanapozungumza japo inaonekana kana kwamba ni katika uzalendo ukweli ni kwamba wanajaribu kujitenga na matendo na misimamo yao wakati walipokuwa madarakani. Ndugu zangu, leo hii tunalipia hatia yao. Wanayo hatia na wakati umefika waanze kukiri hatia hiyo na kuliomba taifa letu msamaha na wawajibike kwa kuanza kukaa kimya.
SOMA ZAIDI HAPA: