dah ustadh ungepitia kwanza andiko lako kabla hujaileta hapa.. naona unachanganya destroyer na aircraft carrier.. destroyer inabeba makombora na kushambulia wakati aircraft carrier ndo inabeba ndege nyingi zikiwa za mashbulizi kwa ajili ya kusogeza mashambulizi karibu.. destroyer inabeba helicopter moja au mbili tu kwa ajili ya kufanya operation ndogo ndogo karibu na meli husika japo nyingi hua zinatumika kutrack nyambizi... na kwa suala la uwepo wa S-300 na S-400 ndani ya Syria na kua kwa kua zipo Syria haikutakiwa kua inashambuliwa na nchi kama Israel na jana Usa nadhan kuna ushabiki unatufanya kutofuatilia mambo kwa uhalisia wake.. ulinzi wa anga hua sio swala dogo hasa kama unajilinda dhidi ya adui mwenye uwezo kama Usa na Israel.. kujilinda dhidi ya nchi kama hizi unahitaji kua na mtandao ambao uko intergrated unaounda kitu kama mwamvuli juu ya anga la nchi husika.. mfano unahitaji SAM batteries atleast katika kila eneo ambalo ni strategic, kua na early warning radars, early warning satellites na centeres za kucontrol hizi assets zote.. hivyo kwa kesi ya Syria hii inakua ngumu kwa kua mitambo ya kisasa iliyopo ni minne tu tena nayo iko kwenye base za Russia tu za Tartus na Hynemym(sina uhakika na spelling).. mitambo yenyewe ni S-300V(special kwa kutungua makombora, S-400(special kwa kutungua ndege hasa fixed wing kama fighters), Pantsir S1 (special kwa helicopter, vifaru na drones) ila pia kuna mtambo wa Bastion anti ship(ulinzi wa pwani).. hii mitambo ni michache kwa ulinzi wa nchi nzima na isitoshe ilipelekwa Syria kwa ajili ya kulinda ndege na base za Urusi ndo maana karibu yote imepelekwa pale tu Uturuki walivotungua ndege ya Russia.. Syria ana mitambo yake kwa ajili ya ulinzi wake sema almost yote ni ya enzi za soviet na ni michache pia.. S-300 na S-400 zisingekua na chochote kama makanjanja wengi mnavodai leo China, India, Iran, Turkey na nchi nyingine nyingi zisingekua eager kutaka kuinunua hii mitambo pia Netanyahu asingehaha kwenda Moscow kumshawishi Putin asiruhusu uuzwaji wa S-300 kwa Iran.. Pia isingekua na chochote tungesikia base na ndege za Russia nchini Syria zinahujumiwa lakini hamna kitu kama hicho... Kwa hiyo sa nyingine ni vizuri kuongelea na kuchambua mambo ya bashite na gwajima, mange na diamond maana ndo tunayoyajua sio haya mengine