Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

Kimenuka Dodoma, magamba yapata moto

Halisi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2007
Posts
2,802
Reaction score
617
Kuna taarifa kwamba, vikao vya awali vya CCM mjini Dodoma vimeanza kwa kuwahoji vijana kadhaa wa UVCCM wanaotajwa kuwa karibu na Watuhumiwa wa ufisadi walotakiwa kujivua gamba.

Haijafahamika kama vijana hao watakua kafara la baba zao ama ndio kipima joto cha maamuzi magumu yanayotarajiwa kufanywa wiki hii. Hakika mwandishi mahiri wa makala katika Raia Mwema alisema, "mbele giza nyuma kaburi" na sasa uamuzi wa kurudi nyuma ni CCM kuingia kaburini na kwenda mbele ni gizani maana magamba yana nguvu za ajabu na kila kukicha yanakua magumu.

Je, CCM itaamua kuingia gizani kuvua magamba ama kurudi nyuma na kuyaacha iwe ni kaburi la CCM?

Taarifa zaidi baadae.

attachment.php

cc2.jpg
 
Natabiri
- Lowassa atang'oka. Kung'oka kwake kutaleta mpasuko mkubwa CHADEMA wengine wakitaka aalikwe CHADEMA na wengine wakiapa "over my dead body".
- Sitta atapewa karipio kali, na kwa kuwa ni ndumilakuwili ataufyata.
- Chenge is not as powerfull as those two, yeye ataondolewa kirahisi na haraka sana.
- Itapangwa mikakati mikali ya kuhakikisha SUGU anang'oka Mbeya kwa hali na mali, haswa baada ya kuitwa Rais wa Mbeya.
 
Si wapigane wao kwa wao tuone yupi atakaelindwa na FFU
 
hakuna jipya litalotokea hapo, sana sana maridhiano na kusameheana na kuanza kuimba wimbo wa sisi sote ni ndugu.
 
Mkulu hatatoa orodha mpya ya wanaofuatia kwenye mpango wa kupewa polium -210?
 
baada ya kuona dalili zote za kuvuliwa gamba. Sasa wanatumia vijana wa ccm kuwaokoa. Sasa wametumwa dodoma kuweka mikakati ya vijana kumlilia baba yao
 
Fred Lowasa, Julius Kalanga ( chair uvccm monduli), Isack Kadogoo ( Diwan Monduli), James Millya (chair uvccm mkoa arusha) wako kazini mjini Dodoma
 
Leo mchana nikijadiliana na mbunge mmoja wa CCM kutoka mkoa wa Dar, aliniambia wazi kwamba, Lowassa hawezi kufukuzwa chamani, kwani ndiye anayeunganisha chama. Kabla ya EL kungo'lewa gamba, mwenyekiti atakuwa wa kwanza kwani matatizo lukuki ndani ya chama na taifa yametokea katika utawala wake. Amesema udini, ufisadi, umasikini, siasa ya makundi yameendelezwa na mwenyekiti wa chama na siyo Lowassa, kwa maana hiyo gamba kubwa ni Rais mwenyewe na siyo EL.

EL akingo'lewa basi tutaelekea kwenye uchaguzi mara moja na CCM itakufa kwa maana 70% ya wabunge CCM wanamuunga mkono EL. JK hawezi kumgusa EL na anajua hilo
 
Natabiri
- Lowassa atang'oka. Kung'oka kwake kutaleta mpasuko mkubwa CHADEMA wengine wakitaka aalikwe CHADEMA na wengine wakiapa "over my dead body".
- Sitta atapewa karipio kali, na kwa kuwa ni ndumilakuwili ataufyata.
- Chenge is not as powerfull as those two, yeye ataondolewa kirahisi na haraka sana.
- Itapangwa mikakati mikali ya kuhakikisha SUGU anang'oka Mbeya kwa hali na mali, haswa baada ya kuitwa Rais wa Mbeya.
kwa sugu watachemka.
 
Back
Top Bottom