Kilio cha Simba chasikika. Kayoko kuwekwa kikaangoni

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,817
4,566
MWENYEKITI wa Kamati ya Waamuzi, Nassor Hamduni, amewaambia wanachama na mashabiki wa Simba kuwa wamesikia kilio chao dhidi ya mwamuzi Ramadhani Kayoko na jambo hilo litakwenda kufanyiwa kazi na Kamati na Nidhamu na anaweza kuadhibiwa iwapo itathibitika kuwa alikuwa na mapungufu kwenye uamuzi wake.

Ijumaa iliyopita baada ya mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Azam FC kumalizika, mashabiki wa 'Wekundu wa Msimbazi' hao walifanya maandamano ndani ya uwanja wa CCM Kirumba, wakimshutumu mwamuzi huyo kwa kutochezesha mechi hiyo kwa haki, wakidai aliwanyima haki kwenye baadhi ya matukio na kuwafanya kutoka sare ya bao 1-1.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Hamduni aliwaomba radhi mashabiki na wadau wote waliokwazwa kwa njia moja ama nyingine kutokana na ufanyaji kazi wa waamuzi katika mechi za hivi karibuni ambazo zimeonekana kuwa na malalamiko mengi.

"Tumeyasikia, tunaheshimu kauli za mashabiki kwa sababu hao ndio wadau wetu wa soka na waswahili wanasema ndiyo wanaotuweka mjini, tumesikia na naomba kuwaeleza.

"Suala la kukataa mwamuzi si la mashabiki, viongozi au kamati yetu waamuzi, bali lipo kwenye kamati maalum ambayo inachunguza mwenendo wa waamuzi, na kama Kayoko ataonekana ana matatizo kwenye mechi aliyochezesha atachukuliwa hatua na si yeye tu, yeyote yule ambaye itabainika amevurunda, tunaomba mashabiki watulie wasubiri Kamati ya Nidhamu ambayo imeshajua hayo, watachukua hatua na sisi Kamati ya Waamuzi ikitufikia tutaridhika na maamuzi watakayochukua," alisema.
 
Huyu wanatakiwa wamfukuze kabisa sio adhabu..mimi nilishasema timu mbovu inaweza kuchukua kombe ligi kuu kwasababu uduni,rushwa na mbereko za waamuz,mfano mechi pia ya kagra na yanga,mashujaa na yanga waamuzi wameamua kuibeba yanga wazi wazi,na hili linachangiwa na waamuzi wa bahasha,uwezo duni,na ushabiki wa kimavx,maelekezo ya wanasiasa n.k,kwa hiyo makombe mengi aliyochukua yanga niyawaamuzi sio ya yanga kama yanga.
Kipimo cha timu bora na kubwa nchini ni timu ambayo inafanya vizuri katika league za kimataifa kwasababu inachezeshwa na waamuzi bora na wenye uweledi mkubwa na zinacheza na timu kubwa na bora barani Africa na timu hiyo ni Simba sc tu.
 
Huwa anageuka Floyd Mayweather, anapiga biti sana huku akisahau wajibu wake ni kusimamia tu sheria 17 za soka.

Atakula alikopeleka mboga.
 
Huyu wanatakiwa wamfukuze kabisa sio adhabu..mimi nilishasema timu mbovu inaweza kuchukua kombe ligi kuu kwasababu uduni,rushwa na mbereko za waamuz,mfano mechi pia ya kagra na yanga,mashujaa na yanga waamuzi wameamua kuibeba yanga wazi wazi,na hili linachangiwa na waamuzi wa bahasha,uwezo duni,na ushabiki wa kimavx,maelekezo ya wanasiasa n.k,kwa hiyo makombe mengi aliyochukua yanga niyawaamuzi sio ya yanga kama yanga.
Kipimo cha timu bora na kubwa nchini ni timu ambayo inafanya vizuri katika league za kimataifa kwasababu inachezeshwa na waamuzi bora na wenye uweledi mkubwa na zinacheza na timu kubwa na bora barani Africa na timu hiyo ni Simba sc tu.
Vipi Ile ya November 5, Yanga walibebwa kama kawaida yao?
 
MWENYEKITI wa Kamati ya Waamuzi, Nassor Hamduni, amewaambia wanachama na mashabiki wa Simba kuwa wamesikia kilio chao dhidi ya mwamuzi Ramadhani Kayoko na jambo hilo litakwenda kufanyiwa kazi na Kamati na Nidhamu na anaweza kuadhibiwa iwapo itathibitika kuwa alikuwa na mapungufu kwenye uamuzi wake.

Ijumaa iliyopita baada ya mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Azam FC kumalizika, mashabiki wa 'Wekundu wa Msimbazi' hao walifanya maandamano ndani ya uwanja wa CCM Kirumba, wakimshutumu mwamuzi huyo kwa kutochezesha mechi hiyo kwa haki, wakidai aliwanyima haki kwenye baadhi ya matukio na kuwafanya kutoka sare ya bao 1-1.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Hamduni aliwaomba radhi mashabiki na wadau wote waliokwazwa kwa njia moja ama nyingine kutokana na ufanyaji kazi wa waamuzi katika mechi za hivi karibuni ambazo zimeonekana kuwa na malalamiko mengi.

"Tumeyasikia, tunaheshimu kauli za mashabiki kwa sababu hao ndio wadau wetu wa soka na waswahili wanasema ndiyo wanaotuweka mjini, tumesikia na naomba kuwaeleza.

"Suala la kukataa mwamuzi si la mashabiki, viongozi au kamati yetu waamuzi, bali lipo kwenye kamati maalum ambayo inachunguza mwenendo wa waamuzi, na kama Kayoko ataonekana ana matatizo kwenye mechi aliyochezesha atachukuliwa hatua na si yeye tu, yeyote yule ambaye itabainika amevurunda, tunaomba mashabiki watulie wasubiri Kamati ya Nidhamu ambayo imeshajua hayo, watachukua hatua na sisi Kamati ya Waamuzi ikitufikia tutaridhika na maamuzi watakayochukua," alisema.
Mnalazimisha Kayoko aonekane ana tatizo Mechi na Azam lakini mkiulizwa tukio alilokosea hamsemi.
 
Huyu wanatakiwa wamfukuze kabisa sio adhabu..mimi nilishasema timu mbovu inaweza kuchukua kombe ligi kuu kwasababu uduni,rushwa na mbereko za waamuz,mfano mechi pia ya kagra na yanga,mashujaa na yanga waamuzi wameamua kuibeba yanga wazi wazi,na hili linachangiwa na waamuzi wa bahasha,uwezo duni,na ushabiki wa kimavx,maelekezo ya wanasiasa n.k,kwa hiyo makombe mengi aliyochukua yanga niyawaamuzi sio ya yanga kama yanga.
Kipimo cha timu bora na kubwa nchini ni timu ambayo inafanya vizuri katika league za kimataifa kwasababu inachezeshwa na waamuzi bora na wenye uweledi mkubwa na zinacheza na timu kubwa na bora barani Africa na timu hiyo ni Simba sc tu.
Unazi unakusumbua!... Tatizo lenu simba na yanga mnataka mpewe special attention na marefa hata kama kwa kuonea timu pinzani.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Huyu wanatakiwa wamfukuze kabisa sio adhabu..mimi nilishasema timu mbovu inaweza kuchukua kombe ligi kuu kwasababu uduni,rushwa na mbereko za waamuz,mfano mechi pia ya kagra na yanga,mashujaa na yanga waamuzi wameamua kuibeba yanga wazi wazi,na hili linachangiwa na waamuzi wa bahasha,uwezo duni,na ushabiki wa kimavx,maelekezo ya wanasiasa n.k,kwa hiyo makombe mengi aliyochukua yanga niyawaamuzi sio ya yanga kama yanga.
Kipimo cha timu bora na kubwa nchini ni timu ambayo inafanya vizuri katika league za kimataifa kwasababu inachezeshwa na waamuzi bora na wenye uweledi mkubwa na zinacheza na timu kubwa na bora barani Africa na timu hiyo ni Simba sc tu.
Kuandika Kiswahili unapata tabu akili utatoa wapi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom