Kilio cha Mlalahoi: Kupanda kwa bei ya umeme wanasiasa mko wapi?

Haisikitishi tuna iliya ccm timing ya kuimaliza isionekane tena kwenye humviringo wa dunia.Kiama chao chaja!.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
CHADEMA yale maandamano yetu mbona kimya????? Au kwa sababu na nyinyi hamuoni shida kama MACCM?? tambueni sisi wananchi tunateseka
 
Ama wajitahidi wafute hizo kodi kwenye umeme maana ndo zinaua bendi.

Izo kodi ishakua kama maji ya kunywa, kila kitu kodi. Ivo hatuwezi kuishi bila kodi.

Lkn ni kudhulumiana tu, kwani izo kodi tunolipa sijui hata zinafaidisha wangapi?
 
FOR THE BENEFIT OF THE PEOPLE OF TANZANIA KAMA ILIVYO FOR THE BENEFIT OF THE PEOPLE OF THE AMERICA NAPENDEKEZA TANESCO IBINAFISHISHWE IWE NA MAKAMPUNI KAMA TIGO.VODA .AIRETELL !ZANT EL N.K nadhan itaxaidia hata kama siyo leo itakuwa kesho au kesho kutwa
 
Kwa hili la umeme nimeamini Watz tu watu wa ajabu sana,na hao viongozi tuliowapa dhamana ya kutuongoza ndio mizigo zaidi,inatia hasira........wachangiaji munashauri tupunguze matumizi wengine tulishapunguza muda mrefu,mfano mimi friji nilikuwa nawasha mchana tu ikifika usiku nalizima,sasa mkiniambie nipunguze maana yake nisiliwashe kabisa,pasi nanyoosha nguo za wiki nzima,tv siwashi maana siangaliagi,matumizi yangu makubwa ni computer kwa maana ya kufanyia kazi kucheki......jamani wengine tushapunguza vya kutosha lkn rhumba ni lile lile......
Yaani unatembea mule mule nilipo na mambo hayakai sawa! huu mlinganyo jawabu liko upande wa pili-ni kuilazimisha serikali ibatilishe hili ongezeko! kwa maana hata ukisema ubakishe vitu vya lazima tena kwa kujibana bado hesabu haivutii machoni!
 
Services charges ndio Janga sana,tuakikishe inafutwa viongozi wa upinzani tunaomba mtu saidie hili,mbona kwenye vocha za simu hatukatwi service charges?
Cc: Dr.W.Slaa ,Julius Mtatiro , John Mnyika, Rev. Mtikila, James Mbatia
Swahibu wangu kwa hali ilivyo si wakati wa kumuomba kaka (mwnasiasa) akusaidie ,hapa ni kuchukua hatua stahiki kama mwananchi kuhusiana na dhahama hii,makali yake hayatupi nafasi ya kusubiri huruma za wajomba!
 
endeleeni kunyakunya watanzania na magamba wenu wanaosema tz kuna amani. Mkiambiwe tuandamane mnaunyaunya mnadhani magamba watawahurumia. Hawawezi wahurumia hata mlie na machozi ya damu
 
Swahibu wangu kwa hali ilivyo si wakati wa kumuomba kaka (mwnasiasa) akusaidie ,hapa ni kuchukua hatua stahiki kama mwananchi kuhusiana na dhahama hii,makali yake hayatupi nafasi ya kusubiri huruma za wajomba!

Hapa amna huruma
 
Kitendo cha Zitto na Mkumbo kuivuruga Chadema kwa usaliti wakitumiwa na magamba matokeo yake ndiyo hayo "wananchi tukubali kufa tumepiga magoti badala ya kufa tumesimama" Ila bado ninaimani kubwa kuna siku wananchi watachoka na kujitambua hapo ndipo utakuwa mwisho wa kunyanyasika ndani ya nchi yetu iliyojaliwa kuwa na kila aina ya rasilmali ambayo haiwafaidishi wananchi waliowengi badala yake inafaidisha viongozi wachache wasiotosheka.
 
Chadema wakwap??? Au Ndo nao wana maslah mle tanesco??

Ninyi ndio wale wash.enzi mnaosakizia wengine kuwa front halafu polisi wakitisha kidogo mnaanza kuwazodoa waliojitoa mbele kupigania haki za watanzania wote.Kwa nini iwe Chadema na isiwe wananchi bila kujali vyama?Wananchi tunatakiwa kuamka na kujitetea halafu Chadema watatuunga mkono na siyo kinyume chake!Upum.ba.avu wa kudhani kuna watu maalum wa kukupigania haki yako wakati wewe mwenyewe hujali utasababisha hii midude ccm itupande sana kichwani

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Mbona Kama hatujui cha kufanya? tunamalizia hasira zetu JF! hivi CHADEMA,CUF,NCCR, N.k Wapo Wapi? Watuongoze Kupinga Bei hzi nasi tuko nyuma yao. WAKUU tufanye kama SYRIA Na EGYPT.
 
Stabilaiza

Ni kweli mada yako ina mashiko, ila napata shaka EWURA ipo kwa masilahi ya nani?serikali, watumiaji huduma za umeme, maji, nishati na mafuta?

Kimsingi inatia shaka kama ipo kwa masilahi ya wananchi au kama ni kupata posho na mishahara minono kwa kazi ndogo sana za ubabaishaji kama kusingizia wadau wamekutana na EWURA , hivyo kuridhia kupanda bei.Tatizo la kupanda bei ya umeme ni makosa ya wizara kwa kuridhia capacity charges, kuridhia kuendelea kuendesha mtambo wa IPTL, kuridhia kuwa na mikataba ya mitambo ya kutumia mafuta yapata miaka minne sasa, huku bei zao za umeme ni kubwa mno kiasi tanesco haikuwa na uwezo wa kununua umeme huo.

Nakumbuka akina JOHN MNYIKA walipinga kiasi kikubwa bungeni hiyo mitambo kuwa italeta mzigo wa watumiaji ikasemekana ni kwa muda tu.na serikali wakati huo kukopa pesa kwenye vyombo vya fedha kwa riba kubwa kulipia mafuta. Hiyo yote ndo imeleta hii kadhia.Kimsingi hao walioridhia walipashwa kufikishwa mahakamani kulinginza taifa kwenye utata huu na gharama kubwa za umeme ambao umeongeza bei ya umeme. Tatizo nchi yetu watanzania si watu wakuhoji ubabaishaji.

Simbachawene alipohojiwa akasema mtu atakaye shindwa kulipa bei ya kupanda umeme akawashe kibatari , ikuwa kuwa kila namna umeme lazima upande hata kama wadau mtahusishwa kama daganya toto kuridhia, lakini iwe funika kombe serikali ipandishe bei.

Kimsingi kupanda bei ya umeme, ni kupandisha ugumu wa maisha , hivyo tukaze kamba tu, maana mfumko wa bei inakuja sasa hivi.
Tunabanwa kushoto, kulia. hakuna pa kukumbilia. Umeme na sasa kuna kilio cha EFD. Mama mmoja aliyefunga duka lake amenifurahisha kwa kusema hizo EFD zinajua mauzo tu hazijuia unanunua kwa gharama gani.
 
CHADEMA yale maandamano yetu mbona kimya????? Au kwa sababu na nyinyi hamuoni shida kama MACCM?? tambueni sisi wananchi tunateseka

Kura unapiga CCM mambo yakiwa magumu unataka CDM wasaidie. K wanini usiombe msaada kwa Uliyempa madaraka ukiona ndiye anayefaa.
 
Nimeshangazwa sana na ukimwa wa wanasiasa kuhusu kupanda kwa bei ya umeme.

Ifike mahali wanasiasa wawajibike kwa wananchi dhidi ya ugumu wa maisha kila kukicha. Kupanda kwa bei ya umeme kutasababisha ugumu wa maisha na mfumko wa bei hivyo kuimarisha umaskini kwa wanachi. Au ni maandalizi ya uchaguzi mwaka 2015 ili kuwahonga kirahisi watu chumvi, kanga na sukari kwa sababu ya ugumu wa maisha?

wanasiasa wana nafasi kubwa y kuletea watu unafuu w bidhaa au huduma msingi kw wale wanaowaongoza wakishirikiana na viongozi wenye mamlaka serikalini. Bei y umeme imepanda. Kulikoni wasitusaidie? Wanaweza kwakachukua hatua wakianzia na mikataba y wazalishaji umeme. Mikataba imekaaje madhara ya kuvunja mikataba ni hatari tutakuja kulipishwa umeme zaidi y hivi sasa. Ila swali la msingi mzee w Richmond hana uhusiano na gharama hii tunayotozwa na subsidy inayotolewa na serikali?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom