Kilio cha Maalim Seif chafikishwa UN

Kilio cha Maalim Seif chafikishwa UN

Where there are too many policemen, there is no liberty.
Where there are too many soldiers, there is no peace.
Where there are too many lawyers, there is no justice.

Hiyo kitu nimeikubali sana
 
Watanzania wakiona kizungu wanatamani wawe wazungu. Hivi wanayofanya Libya, Syria, Iraq na kwingine hawajui?

Huyu anayejidanganya aendelee.

nakumbuka ile ya UKAWA Kwenda nao Uholanzi eti wazungu wasaidie kutengua uchaguzi.

Seif angeenda Uganda ndo ajuwe maana ya upinzani. Hapa watu kuhojiwa tu wanalalama.
 
Si tuliambiwa Maalim Seif kajifungia chumbani wajameni ? Huko Ulaya na Marekani kaenda lini ?
Na Jecha anastahili kupewa tuzo

Au mimi ndio sielewi kitu
 
Au ndio maana mkuu hataki kujizoesha raha za kusafiri ili asije kuumia pindi wakipigwa zuio?
Labda Mzee kaona mbali na kuamua kujiepusha na fedheha
 
Hapa ndio huwa nazichukia siasa za Afrika.. Kwamba hatuwezi kufanya mambo yetu wenyewe kwa ustaarabu na kuheshimiana mpaka mzungu atushikie fimbo..
Yaani nakereka pale tunapoenda kusemea kwa wazungu eti ndo waje kutushinikiza kufanya jambo Fulani... Childish
 
ZIARA ya kimataifa aliyoifanya Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Marekani, Ulaya, Canada na Umoja wa Mataifa kulalamikia uvurugaji wa uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba mwaka jana, imeanza kuzaa matunda, anaandika Jabir Idrissa.

Tayari taasisi ya kimataifa ya umoja wa wanaliberali – Liberal International (LI) – imeliandikia Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) kutaka kutolewa kwa vikwazo dhidi ya Serikali ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kwenye tovuti ya LI, taasisi hiyo imetaka baraza hilo lenye jukumu la kulinda misingi ya haki za binadamu kwenye mataifa yote wanachama wa UN, kuchukua hatua kali ili kukomesha “uvunjaji mkubwa wa haki za binaadamu na ukandamizaji wa haki za kisiasa na kiraia visiwani Zanzibar.”

Katika tamko walilolitoa na kufikishwa mbele ya Mkutano wa 33 wa Baraza hilo uliofanyika Septemba mosi mwaka huu, Liberal International imetaka jumuiya ya kimataifa, kufikiria kuweka vikwazo vya kusafiri na kuzuia mali za watu wote walioshiriki kuidhinisha vitendo vya utesaji wanasiasa wa upinzani na wafuasi wao.

Taasisi hiyo ambayo CUF ni mwanachama wa muda mrefu, imetoa wito kwa wabunge wanaofuata mtizamo wa kiliberali walioko upande wa serikali na upinzani katika mataifa yote duniani kuchukua msimamo imara kupitia mabunge ya nchi zao na kutoa matamko ya kupinga walichokiita “uonevu wanaofanyiwa viongozi wa upinzani Zanzibar na wafuasi wao.”

“Tunaitaka serikali ya Zanzibar na Tanzania kuheshimu utawala wa sheria na kuingia katika majadiliano na upinzani ndani ya muda maalum hatua ambayo itawezesha kuundwa serikali ya mpito na kukubali kuitishwa kwa uchaguzi mpya ili kuondoa mgogoro uliojitokeza baada ya kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba 2015,” imesema taarifa ya LI.

Hatua hiyo ya LI kuandikia Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa inakuja wiki kadhaa baada ya Maalim Seif kukutana na taasisi mbalimbali za kimataifa zinazoshughulikia maendeleo ya demokrasia na utawala bora, pamoja na wakuu wa serikali za Marekani, Ulaya na Canada.

Maalim Seif aliyefuatana na baadhi ya wasaidizi wake pia alifika Mahakama ya Uhalifu wa Kivita ya The Hague, Uholanzi ambako aliwasilisha malalamiko ya uvunjaji wa haki za binadamu unaofanywa Zanzibar kwa idhini ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hatua ya Maalim Seif na CUF imekuja baada ya CCM kumuamuru Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufuta uchaguzi mkuu wa Zanzibar, 28 Oktoba, baada ya kubaini kuwa chama hicho kimepoteza madaraka kupitia sanduku la kura.
Haina haja ya kuweka propaganda nyingi wakati wazanzibar wameshaipata serikali yao inayowahudumia wananchi bila ubaguzi wowote cha msingi maalim akae kimya na kusubiri 2020 huo ndo uanaume siyo kwenda kujikomba komba kwa watu ambao walitutawala na kuchukua Mali zetu!
 
Nilipokuwa mdogo nilifikiri watu wazima wote wana akili, nilivyokuwa mkubwa kidogo nilikuja kugundua sikuwa sahihi. Nilipokuwa shule ya msingi na sekondari nilijua wanasiasa wana akili sana, nimekuwa mtu mzima nimegundua wana akili tu za kawaida....na kwa kweli wanahitaji msaada wa mawazo kutoka kwa watu wasio wanasiasa. Forum hii ina watu wenye akili sana, wanasiasa wa pande zote piteni hapa mtajiongeza
 
ZIARA ya kimataifa aliyoifanya Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Marekani, Ulaya, Canada na Umoja wa Mataifa kulalamikia uvurugaji wa uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba mwaka jana, imeanza kuzaa matunda, anaandika Jabir Idrissa.

Tayari taasisi ya kimataifa ya umoja wa wanaliberali – Liberal International (LI) – imeliandikia Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) kutaka kutolewa kwa vikwazo dhidi ya Serikali ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kwenye tovuti ya LI, taasisi hiyo imetaka baraza hilo lenye jukumu la kulinda misingi ya haki za binadamu kwenye mataifa yote wanachama wa UN, kuchukua hatua kali ili kukomesha “uvunjaji mkubwa wa haki za binaadamu na ukandamizaji wa haki za kisiasa na kiraia visiwani Zanzibar.”

Katika tamko walilolitoa na kufikishwa mbele ya Mkutano wa 33 wa Baraza hilo uliofanyika Septemba mosi mwaka huu, Liberal International imetaka jumuiya ya kimataifa, kufikiria kuweka vikwazo vya kusafiri na kuzuia mali za watu wote walioshiriki kuidhinisha vitendo vya utesaji wanasiasa wa upinzani na wafuasi wao.

Taasisi hiyo ambayo CUF ni mwanachama wa muda mrefu, imetoa wito kwa wabunge wanaofuata mtizamo wa kiliberali walioko upande wa serikali na upinzani katika mataifa yote duniani kuchukua msimamo imara kupitia mabunge ya nchi zao na kutoa matamko ya kupinga walichokiita “uonevu wanaofanyiwa viongozi wa upinzani Zanzibar na wafuasi wao.”

“Tunaitaka serikali ya Zanzibar na Tanzania kuheshimu utawala wa sheria na kuingia katika majadiliano na upinzani ndani ya muda maalum hatua ambayo itawezesha kuundwa serikali ya mpito na kukubali kuitishwa kwa uchaguzi mpya ili kuondoa mgogoro uliojitokeza baada ya kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba 2015,” imesema taarifa ya LI.

Hatua hiyo ya LI kuandikia Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa inakuja wiki kadhaa baada ya Maalim Seif kukutana na taasisi mbalimbali za kimataifa zinazoshughulikia maendeleo ya demokrasia na utawala bora, pamoja na wakuu wa serikali za Marekani, Ulaya na Canada.

Maalim Seif aliyefuatana na baadhi ya wasaidizi wake pia alifika Mahakama ya Uhalifu wa Kivita ya The Hague, Uholanzi ambako aliwasilisha malalamiko ya uvunjaji wa haki za binadamu unaofanywa Zanzibar kwa idhini ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hatua ya Maalim Seif na CUF imekuja baada ya CCM kumuamuru Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufuta uchaguzi mkuu wa Zanzibar, 28 Oktoba, baada ya kubaini kuwa chama hicho kimepoteza madaraka kupitia sanduku la kura.
watakosea sana kama watawawekea vikwazo vya kusafiri viongozi wetu maana itakuwa sherehe kwa rais wetu. labda wafanye kinyume chake huenda vikwazo vyao vikawa valid.
 
Akipewa robo moyo wakati moyo una chamber nne. hiyo robo itafanyaje kazi na aliyebakiwa na robo tatu ya moyo ut afanyajte kazi?
Nadhani hujaelewa, yaani watabadilishana robo moyo ili kubalance... angalau kila mmoja awe na chembechembe mchanganyiko
 
Jecha atakufa kwa presha akiipata hii taarifa.
Hasa ukizingatia ya kuwa badala ya kutunukiwa nishani ya utumishi uliotukuka kwa kufunga goli la mkono kwenye uchaguzi wa mwaka jana kule Zanzibar kama alivyopendekeza JPM, anaweza kujikuta badala yake anatunukiwa nishani ya kwenda gerezani........
 
hakuna kitu hapo. mbona marekani bado wanamwaga misaada?


Mmarekani haleti msaada wa cash, ukisikia mmsrekani kaleta msaada basi ni arvs,methadone, dawa za tb na chanjo mbalimbali ili makapuku msife kwa kuwa siyo walengwa
 
ZIARA ya kimataifa aliyoifanya Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Marekani, Ulaya, Canada na Umoja wa Mataifa kulalamikia uvurugaji wa uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba mwaka jana, imeanza kuzaa matunda, anaandika Jabir Idrissa.

Tayari taasisi ya kimataifa ya umoja wa wanaliberali – Liberal International (LI) – imeliandikia Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC) kutaka kutolewa kwa vikwazo dhidi ya Serikali ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kwenye tovuti ya LI, taasisi hiyo imetaka baraza hilo lenye jukumu la kulinda misingi ya haki za binadamu kwenye mataifa yote wanachama wa UN, kuchukua hatua kali ili kukomesha “uvunjaji mkubwa wa haki za binaadamu na ukandamizaji wa haki za kisiasa na kiraia visiwani Zanzibar.”

Katika tamko walilolitoa na kufikishwa mbele ya Mkutano wa 33 wa Baraza hilo uliofanyika Septemba mosi mwaka huu, Liberal International imetaka jumuiya ya kimataifa, kufikiria kuweka vikwazo vya kusafiri na kuzuia mali za watu wote walioshiriki kuidhinisha vitendo vya utesaji wanasiasa wa upinzani na wafuasi wao.

Taasisi hiyo ambayo CUF ni mwanachama wa muda mrefu, imetoa wito kwa wabunge wanaofuata mtizamo wa kiliberali walioko upande wa serikali na upinzani katika mataifa yote duniani kuchukua msimamo imara kupitia mabunge ya nchi zao na kutoa matamko ya kupinga walichokiita “uonevu wanaofanyiwa viongozi wa upinzani Zanzibar na wafuasi wao.”

“Tunaitaka serikali ya Zanzibar na Tanzania kuheshimu utawala wa sheria na kuingia katika majadiliano na upinzani ndani ya muda maalum hatua ambayo itawezesha kuundwa serikali ya mpito na kukubali kuitishwa kwa uchaguzi mpya ili kuondoa mgogoro uliojitokeza baada ya kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa 25 Oktoba 2015,” imesema taarifa ya LI.

Hatua hiyo ya LI kuandikia Baraza la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa inakuja wiki kadhaa baada ya Maalim Seif kukutana na taasisi mbalimbali za kimataifa zinazoshughulikia maendeleo ya demokrasia na utawala bora, pamoja na wakuu wa serikali za Marekani, Ulaya na Canada.

Maalim Seif aliyefuatana na baadhi ya wasaidizi wake pia alifika Mahakama ya Uhalifu wa Kivita ya The Hague, Uholanzi ambako aliwasilisha malalamiko ya uvunjaji wa haki za binadamu unaofanywa Zanzibar kwa idhini ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hatua ya Maalim Seif na CUF imekuja baada ya CCM kumuamuru Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kufuta uchaguzi mkuu wa Zanzibar, 28 Oktoba, baada ya kubaini kuwa chama hicho kimepoteza madaraka kupitia sanduku la kura.

Chanzo: Mwanahalisi Online
Hhahahahahahahahaa bwabwabwabwabwaaaa Ama kweli wajinga ndiyo waliwao
 
Back
Top Bottom