Kilimo ni biashara pekee inayolipa kwa 100%

Yaani watu wanapotishana kwenye mitandao humu,toa mchanganuo ulilima wapi,kilimo cha kutegemea mvua au kumwagilia,ulipata jumla ya gunia au tani ngapi na uliuza kwa bei gani??,mimi pia ni mkulima wa mahindi nzuri tu ila kwa hekali 2 ukapata mil3 ,mmmhhhh?!???

Nakuambia wewe acha tu huku mitandaoni. Nilijaribu kuingia kwenye kilimo nikawekeza vya kutosha. Kila siku nikawa nawaaga wafanyakazi wenzangu kwamba huu ni mwaka wa mwisho kuwa ofisini. Nilichokipata huko kwenye kilimo ni Mungu tu anajua. Asikudanganye mtu, ni bora ubaki kwenye ajira hata kama unatukanwa kuliko kujichanganya kwenye kilimo kwa hizi hadithi za mitandaoni. Kilimo ni wito sio kitu cha mchezo.
 
Mimi nawashauri vijana wasijidanganye kwenda shambani ni bora wabaki mjini wakiwa wanabeti kuliko kufuata hizi porojo za huku mitandaoni. Hivi kilimo kingekuwa kinalipa leo tungewaona wakulima wakiwa wamechoka kiwango kile? Mbona hata hao mabwana shamba wenyewe hawawekezi kwenye kilimo? Kuliko kwenda kulima ni bora uajiriwe kazi ya ulinzi huko kwa wahindi. Ukitaka kuwa masikini nchi hii danganywa ukalime.
Hivi unafahamu matajiri wakubwa wa nchi hii ni wakulima !!???
Duniani unafahamu wenye pesa ni wakulima!?
Usilolijua usilicrash hata hao viongoz wako wa serikali ni wakulima ,you cant see if you aint trained to see,jifunze sasa na tazama utapata majibu .
Sema kilimo unatakiwa uwe na mahesabu makali na usitegemee faida za siku mbili lazima ufanye kazi kweli ya kueleweka ,only msimu huu unaoishi moshi mile sita (rambo mferejini) somebody kalima 16 acres za nyanya kwa gharama ya million 50 na ushee ,kavuna more than million 700 ni investment kubwa but alitupa fedha nyingi na imerudi kwa faida ya ajabu huo mfano mdogo sana ,ukianza kilimo dont start with acre 10 nop anza na nusu eka au moja jifunze mazuri na changamoto than add more land utaona kilimo kilivyovyema ,wakulima ambao hawaendelei ni wale ambao wao wanafanya kilimo mazoea lazima ufahamu kilimo ni science utafanikiwa
 
Acha fix kilimo kwa nchi yetu kina changamoto nyingi kuanzia shambani hadi sokoni,tena huko sokoni ni kikwazo utawakuta madalali wana vitambi kupitia migongo ya wakulima acha kabisa ndugu,ukitaka kilimo sharti ujipange na kilimo kinacholipa ni cha kisasa na niliazima uwe na mtaji vinginevyo utaambulia patupu.
Watu wanang'ang'ania ajira ni kwa sababu hawana starting point ambayo ni mtaji!
Ni hayo tu....Asante kwa kusoma
Umenena vyema but unadhani kuna mtu atakuja akupe mtaji !? Tumia kidogo ulichonacho kwa kuanza taratibu na ukiwa na malengo ya mbali ,rulw namba one ya kilimo dont produce if you dont have soko la mavuno yako .
 
Nakuambia wewe acha tu huku mitandaoni. Nilijaribu kuingia kwenye kilimo nikawekeza vya kutosha. Kila siku nikawa nawaaga wafanyakazi wenzangu kwamba huu ni mwaka wa mwisho kuwa ofisini. Nilichokipata huko kwenye kilimo ni Mungu tu anajua. Asikudanganye mtu, ni bora ubaki kwenye ajira hata kama unatukanwa kuliko kujichanganya kwenye kilimo kwa hizi hadithi za mitandaoni. Kilimo ni wito sio kitu cha mchezo.
Wewe kama ulishindwa sio wote wanaoshindwa wengine wamelima na wanaendelea kulima, na wananufaika na kilimo.
 
Wewe kama ulishindwa sio wote wanaoshindwa wengine wamelima na wanaendelea kulima, na wananufaika na kilimo.

Ni kweli usemayo mkuu, lakini mbona wakulima ndio jamii masikini kabisa humu nchini kama kweli inalipa kihivyo?
 
Ni kweli usemayo mkuu, lakini mbona wakulima ndio jamii masikini kabisa humu nchini kama kweli inalipa kihivyo?
Sio kila anaekwatua ardhi ni mkulima ,wengine wasindikiza . Ukiona mtu anazalisha kwa matumizi ya kula nyumbani huyo si mkulima kilimo cha manufaa ni kilimo biashara ,asikudanganye mtu kilimo kinawatoa sana watu but na wewe uchakarike pia sio kukaa tu kua mtazamaji
 
Sio kila anaekwatua ardhi ni mkulima ,wengine wasindikiza . Ukiona mtu anazalisha kwa matumizi ya kula nyumbani huyo si mkulima kilimo cha manufaa ni kilimo biashara ,asikudanganye mtu kilimo kinawatoa sana watu but na wewe uchakarike pia sio kukaa tu kua mtazamaji

Hizi hadithi tamu tumeshazizoea, lakini watu wanaingia hasara na kubaki na madeni baada ya mikopo.
 
asante kwa kutushirikisha idie yako,
nikuulize kidogo mr huko tarime wenyeji wana wapokea wageni angalao kwa uafadhali kidogo? maana kinadharia wanasema wenyeji wote wa tarime wako na roho mbaya!
 
Kilimo??? Yaani ulinganishe na ajira? Hata kama napata laki 5 kwa mwezi wacha iwe hivyo. Kilimo hakitabiriki ingawa kweli ukkibahatisha unatoka, lakini pia ujiandae kutoka mrisi! Niliingiwa tamaa ya kulima matikiti maji, nikazamisha kama 2.5m (ikijumuisha na ununuzi wa shamba ekari 32). Nikakata kipande kama ekari moja nikalima hayo matikiti maji nikawa napiga hesabu ya kupiga hela si chini ya 5m, kwani niliambulia kitu? Kumbe timing yangu ilikuwa mbovu sokoni kukawa na matikiti kibao na pia timing ya kulima kumbe ilikuwa mbaya mengi yakabaki shambani maana hayakufikia mwisho wa kukomaa! Nashukuru tu nilibaki na shamba ndo faida yangu, sasa hivi ndo napanga nibadili kilimo nifanye ukulima wa samaki,, ha ha ha haaaa (nifuge samaki) maana liko karibu na mto usiokauka (Mto Ruchugi - Kasulu). Mtu hawezi tena kunidanganya eti niache kazi ya mshahara nikabobee kwenye kilimo. Na hiyo kazi ambayo mleta mada anaisema ya laki 5, hiyo si ni ya mtu wa diploma? Bora upige vyote (kilimo na ajira) hapo maisha yataenda!!
 
Kuweni makini kuna watu sio wa kweli hata Kama Ni rafiki yako. Ekari moja ya kitunguu itoe gunia 113?!! Na bei ya shambani 90,000!! Usije kuja kuwa disappointed. Mwambie aseme ukweli maana kuna watu hawataki kuonekana kuwa wamepata hasara
We ni mkweli! Huyo jamaa mwongo.Atuambie alilima wapi.Maana wakulima mwaka huu tumeuza Tshs 40,000 kwa gunia
 
Hizi hadithi tamu tumeshazizoea, lakini watu wanaingia hasara na kubaki na madeni baada ya mikopo.
Yes nakubaliana na wewe ndg thus y lazima ufanye kilimo biashara yaani anza na eneo dogo panda taratibu huku unaendelea kukuza mtaji na kujifunza ,hivi hata biashara ya duka unaweza anza tu na duka la jumla !!?? Au usafirishaji unaweza anza tu na mabasi ya mikoani !? Watu tuache tamaa ya faida kubwa anza na kidogo taratibu upande juu maana leo ulima robo au nusu eka utakapokua unauza unatengeneza wanunuzi watakao kueleza ulime nn na wao wanachukua so ni umakini hapo ndugu yangu unaitajika tujifunze kilimo kwa vitendo na tuanze na kidogo
 
Kilimo??? Yaani ulinganishe na ajira? Hata kama napata laki 5 kwa mwezi wacha iwe hivyo. Kilimo hakitabiriki ingawa kweli ukkibahatisha unatoka, lakini pia ujiandae kutoka mrisi! Niliingiwa tamaa ya kulima matikiti maji, nikazamisha kama 2.5m (ikijumuisha na ununuzi wa shamba ekari 32). Nikakata kipande kama ekari moja nikalima hayo matikiti maji nikawa napiga hesabu ya kupiga hela si chini ya 5m, kwani niliambulia kitu? Kumbe timing yangu ilikuwa mbovu sokoni kukawa na matikiti kibao na pia timing ya kulima kumbe ilikuwa mbaya mengi yakabaki shambani maana hayakufikia mwisho wa kukomaa! Nashukuru tu nilibaki na shamba ndo faida yangu, sasa hivi ndo napanga nibadili kilimo nifanye ukulima wa samaki,, ha ha ha haaaa (nifuge samaki) maana liko karibu na mto usiokauka (Mto Ruchugi - Kasulu). Mtu hawezi tena kunidanganya eti niache kazi ya mshahara nikabobee kwenye kilimo. Na hiyo kazi ambayo mleta mada anaisema ya laki 5, hiyo si ni ya mtu wa diploma? Bora upige vyote (kilimo na ajira) hapo maisha yataenda!!
Mkuu naomba number yako ya simu kwa PM.

Nataka niwe jirani yako
 
Mwanafunzi wa chuo anaweza kujipanga mwenyewe kabisa, ila ubaya ni kwamba watu wengi hatuna kitu kinacho itwa "saving culture" tunategemea mwisho wa siku tutapewa au tutaomba kila kitu.

Tuchukulie mfano wa kijana aliyejitambua na mwenye malengo thabiti kabisa. Anapo anza mwaka wa kwanza akaweza kuhifadhi 50,000 kwenye pesa yake ya kujikimu kila mwezi ndani ya miezi minne kijana huyo atakuwa na 200,000 na akiendelea kufanya hivyo kwa miaka mitatu atakuwa na 600,000 kama pesa hii itakuwa alikuwa akiiweka fixed account kwa bank kama Azania wana account unayo weza kuongeza pesa kila mwezi ila ina act kama fixed account.

Pesa hii baada ya miaka mitatu itakuwa mtaji wa kutosha kabisa kwa kijana kuanza maisha na sio lazima kijana huyo aweke 50,000 ila anaweza weka kiwango chochote anacho ona hakita haribu matumizi yake ya kila siku.

Ila kwasababu hatuna desturi ya kuthamini vidogo tulivyo navyo inatusumbua sana baadae tunaanza kulalamika ajira hakuna, mitaji hakuna, serikali hithamini vijana.

Cha msingi hapa ni vijana tuelewe kwamba kabla ya kunyoosha vidole kwa watu wengine na kusema hatujasaidiwa, sisi tumechukua hatua gani ya kujisaidia.??
WAJINGA NDIO WALIWAO NANI KAKUAMBIA BOOM LINATOKA KILA BAADA YA MWEZI KAFANYE TAFITI URUDI UPYA
 
We ni mkweli! Huyo jamaa mwongo.Atuambie alilima wapi.Maana wakulima mwaka huu tumeuza Tshs 40,000 kwa gunia
Sijui mwenye topic alilima aina gani ila kweli kitunguu cha kuzaa gunia 113 kwa ekari kipo ,mbegu hizi
Jambar f1 -gunia 200 mpaka 250 kwa ekari
Neptune gunia 120 mpaka 150 kwa ekari
Meru super gunia 70 mpaka 100 kwa ekari
Red bombay -gunia 30 mpaka 50 kwa ekari.
So mbegu zinatofautiana na bei pia sema kwa msimu uliopita kiangazi kilikua kikali sana most of the places kitunguu hakikufanya vyema ,kwa huku niliko Arusha na moshi baadhi ya wilaya kilikubari ila kwingine kiligoma kwa joto kali sana
 
Sijui mwenye topic alilima aina gani ila kweli kitunguu cha kuzaa gunia 113 kwa ekari kipo ,mbegu hizi
Jambar f1 -gunia 200 mpaka 250 kwa ekari
Neptune gunia 120 mpaka 150 kwa ekari
Meru super gunia 70 mpaka 100 kwa ekari
Red bombay -gunia 30 mpaka 50 kwa ekari.
So mbegu zinatofautiana na bei pia sema kwa msimu uliopita kiangazi kilikua kikali sana most of the places kitunguu hakikufanya vyema ,kwa huku niliko Arusha na moshi baadhi ya wilaya kilikubari ila kwingine kiligoma kwa joto kali sana
Kuna mambo mengi sana Idd ya kuzingatia kupata viwango unavyo onesha.

Haiwezekani kwa mtu anayeanza kilimo kufikia kiwango hicho.BIG NO.

Idd pamoja ya kuwa kilimo kinalipa lakini kinahitaji passion. Kama huna passion ya cho chote unachofanya hakitakulipa.Ukiajiriwa as a teller wakati huna passion , you won't be happy!!!
 
Kuna mambo mengi sana Idd ya kuzingatia kupata viwango unavyo onesha.

Haiwezekani kwa mtu anayeanza kilimo kufikia kiwango hicho.BIG NO.

Idd pamoja ya kuwa kilimo kinalipa lakini kinahitaji passion. Kama huna passion ya cho chote unachofanya hakitakulipa.Ukiajiriwa as a teller wakati huna passion , you won't be happy!!!
Hakika ndio maana nasisitiza kwenye kuanza taratibu sio kuanza na eneo kubwa nop ,anza na eneo dogo unapata mafunzo na kuendelea zaidi
 
Fanya utafit kwanza ndipo utoe ushaur, japo ushaur wako ni mzur sana
Lakin tuangalie risk katika kilimo tanzania tena kilimo endelevu.
Ni kweli mazao ya chakula soko lake ni lauwakika sana
Ila swali la kujiuliza shortage ya mahid iliyopo maeneo ya mikoa ya kaskazin wakulima wa kusuni ambao wanasuplus ya mahid wataweza faidika na hali hiyo
Je nyanya za dumila, mkulima anaweza faidika na shortage ya nyanya dar.
Kisha waza mtu alie chukua mkopo bank na anatakiwa kulipa na riba, kwa hali kama hiyo ataweza.
Maana utafit unasaidia kupunguza riski, ila kuingia ktk biashara bila utafik na kuangalia flan alipata nin tena kwa kipind kifup ni hatar sana.
Ni vema kujua taarifa za zao utakalo kulilima kama sehemu ya uwekezaji wako kuanzia mazingira ya uzalishaji (inputs) kama chanzo ya maji yako kwa hali ya sasa, usafirishaji, pembe jeo na mambo mengine.
Naunga mkono wazo lako

Ndyo mana watu waliosoma ni wagumu kufankiwa kwasabbu they tend to b much analytical and less risk takers! Lkn kwa mtu ambae hajasoma sana na hana ujuaji mwingi anatake risk na akiivuka risk anakua amefankiwa na most of the tym hachoki akiloose atarudia tena kwa kurekebsha kasoro zake za mara ya kwanza na sio kuacha' Tumezoezwa vbaya na elimu yetu what we see on papers as risk kweny kitu fulan they csn some tym be avoided jpo tunavipa uzito sanaa!
 
Ashakum si matusi,
Lakini unapoamua kuwatukana watu waziwazi.........unatupa wasiwasi........
Ekari 2 za mahindi mauzo yawe Mil.3 ???
Hebu tujuze kwenye Ekari 2 ulipata magunia mangapi?
.....
Halafu shamba ulisafisha kwa bei gani?
Kulima ni sh'ngapi?
palizi?
Dawa?
gharama za kuvuna?
Kupukuchua?
Gharama za usafiri kwenda shamba? (angalau kwa uchache gharama hizi hazikwepeki).Mbolea?? mfuko ulinunuaje? USD/Tsh.?
Mkuu unapoamua kuwa mkulima maana yake sehemu kubwa ya nguvu kazi unatoa wewe mwenyewe na usaidizi uupate pale tu unapozidiwa. Tatizo kubwa la ninyi vijana ni kufanya kazi ya kilimo kama wewe ni mwajiri vile. Kwa mfano mimi mwaka jana nililima ekari 12@ekari sh 25,000 kwa trekta jumla laki tatu. mbegu za kupandia kila ekari mifuko mitano yaani 10kg each ekari, kila mfuko elfu sita. kwa hiyo kila ekari elfu30x12= 360.000/. kupanda nilipanda mwenyewe ekari nne na ekari nane niliweka watu kila ekari elf tano =40,000/. Kupalilia kila ekari sh 12,000x12x2= 280,000/, Gharama za kuvuna na kusoma laki sita. .Mapato nilipata magunia 230 nikauza gunia 210@ sh 90,000/ nikapata 18900000. Niliacha gunia 20 ambazo nimetumia mwaka huu kuwalipa nguvu kazi na matumizi binafsi.
N.B sikuweka mbolea ya viwandani mimi shamba langu huwa naweka samadi mara moja kila baada ya miaka mitatu. Angalia mapato na matumizi majibu unayo mwenyewe.
 
Nakuambia wewe acha tu huku mitandaoni. Nilijaribu kuingia kwenye kilimo nikawekeza vya kutosha. Kila siku nikawa nawaaga wafanyakazi wenzangu kwamba huu ni mwaka wa mwisho kuwa ofisini. Nilichokipata huko kwenye kilimo ni Mungu tu anajua. Asikudanganye mtu, ni bora ubaki kwenye ajira hata kama unatukanwa kuliko kujichanganya kwenye kilimo kwa hizi hadithi za mitandaoni. Kilimo ni wito sio kitu cha mchezo.

Tatizo ulikurupuka
 
Hivi unafahamu matajiri wakubwa wa nchi hii ni wakulima !!???
Duniani unafahamu wenye pesa ni wakulima!?
Usilolijua usilicrash hata hao viongoz wako wa serikali ni wakulima ,you cant see if you aint trained to see,jifunze sasa na tazama utapata majibu .
Sema kilimo unatakiwa uwe na mahesabu makali na usitegemee faida za siku mbili lazima ufanye kazi kweli ya kueleweka ,only msimu huu unaoishi moshi mile sita (rambo mferejini) somebody kalima 16 acres za nyanya kwa gharama ya million 50 na ushee ,kavuna more than million 700 ni investment kubwa but alitupa fedha nyingi na imerudi kwa faida ya ajabu huo mfano mdogo sana ,ukianza kilimo dont start with acre 10 nop anza na nusu eka au moja jifunze mazuri na changamoto than add more land utaona kilimo kilivyovyema ,wakulima ambao hawaendelei ni wale ambao wao wanafanya kilimo mazoea lazima ufahamu kilimo ni science utafanikiwa

Nakubaliana na wewe mkuu.
Nilianza na heka 6, matokeo hayakuwa mazuri na kidogo nikikichopatikana nikaingizwa mjini. Sikukata tamaa.
Nilijipanga msimu uliofuata nikalima tena, mambo yakawa si mabaya nilizabwa fanikiwa kupata tani 15 za mahindi pamoja na gunia 80 za alizet.
Ilitakiwa nipate zaidi ya hapo lakini kutokana na changangamoto mbalimbali nilipata kama nilivyo eleza hapo juu.

Moja ya changamoto nilizozipata msimu huo ni kama ifuatavyo:

1. Vipimo vya shamba havikukamilika. Kila heka ilikuwa na ukubwa wa 60 kwa 60m badala ya 70 kwa 70

2. Maagizo niliyoyatoa ni kulima heka 45 lakini Baraka yake nilikuwa heka 30

3. Baadhi ya sehem mazao yaliharibika kwa kutopalilia nilipotez heka 12 ambazo hazikupaliliwa

4. Mazao yaliibiwa sana shambani kutokana na Mimi kutokuwepo jirani ( shamba liko Manyara mimi niko Zanzibar)

5. Kuzidishiwa gharama kwenye shughuli za shamba. Nilipigwa pesa isiyo pungua 3M
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom