Mkikita imenilia elfu 10 kujiunga , Adam sasa kabadili gia angani sasa yupo kwenye koroshoNa Kijani Kibichi ya Adam Rashid Ngemange, matapeli wakubwa
Huu ndio ukweli.Ukiamua kuwekeza kwenye kilimo, jitahidi uwepo shambani kwa zaidi ya asilimia 70. Kama huwezi kuwepo huko shamba, acha kafanye kitu kingine. Kilimo cha simu na mtandao...UTAIBIWA, narudia tena, UTAIBIWA. Na mkishaibiwa msisahau kwenda kwenye medias kuomba serikali iwasaidie
gharama haiwezi fika laki sita katika heka hata ulime na tractor na upige alow haifikiSiwajui, lakini jitahidi kufanya uchunguzi sana kabla ya kutoa pesa yako. Gharama za jumla za kilimo cha mahindi kwa wastani kwa ekari moja inawezafika hiyo laki sita na point, ila sijaona wao faida ya kujiendesha itatoka wapi na pia nina wasiwasi wa kufikisha hayo mavuno ya gunia 30 kwa ekari.
Siwajui, lakini jitahidi kufanya uchunguzi sana kabla ya kutoa pesa yako. Gharama za jumla za kilimo cha mahindi kwa wastani kwa ekari moja inawezafika hiyo laki sita na point, ila sijaona wao faida ya kujiendesha itatoka wapi na pia nina wasiwasi wa kufikisha hayo mavuno ya gunia 30 kwa ekari.
Binafsi naomba niwaeleze watanzania na wengine wenye nia ya kujiunga na hii kampuni. Nimefanya nao kilimo kuanzia mwaka 2020/2021. Mavuno yalipaswa kuwa 2021. Nimeweka pesa nyingi kwao, nadhani kati ya wakulima 10 na mimi nimo.
Kwanza customer care yao sio nzuri. Yaani unasumbuka sana kufanya kitu cha kawaida. Wanapenda sana pesa ila unapohitaji huduma wanakusumbua sana. Kwa siku unaweza kuongea na watu kama 10 bila mafanikio.
Pili, kuna kila dalili za uongo kwenye kilimo chao. Mfano CEO wa hiyo kampuni anakaa anabadilisha simu. Yaani unaweza kuongea naye leo, kesho akawa na namba nyingine ya simu. Hii ni dalili ya kukwepa watu. Anaweza akawa anakwepa watu hili kuepuka usumbufu wa maswali ya ujinga lakini pia anaweza kuwa anakwepa watu sababu hana majibu.
Nimeongea na manager, CEO...hawa wote mtindo wao wa kukwepa watu ni mmoja tu. Hawawezi kukupa jibu lolote. Hii inaonesha kampuni yao ipo kupiga watu na si kilimo kama wanavyotangaza.
Mavuno ya mwaka huu 2021 yamefanyika ila hawakutangaza maharage wamepata nini...eti mpaka mwezi wa kumi. Sasa jipimie mwenyewe. Yaani unalima kitu kwa mwaka mmoja...pengine hutapata pesa yako mpaka baada ya miaka miwili. Ni nani huwa analima hivyo?
Sasa hivi wametangaza mazao yaliyopatikana kwenye mchele na mahindi. Cha ajabu sasa, wanakwepa simu za watu...yaani huwezi kupiga simu ukaulizia kwamba unataka kuuza mazao yako wakapokea au wakakwambia kitu chochote. Hi ni kuanzia kwa CEO (huyu huwezi kumpata), manager (huyu nadhani anadanganya tu) na wafanyakazi wa kawaida (hawa ndo basi)...yaani management ikiisha sasa wafanyakazi wafanye nini?
Kwa ufupi uhusiano wao na wewe ni pale unapopeleka pesa tu. Hakuna mahusiano zaidi ya hapo. Baada ya hapo huwapati tena. Manager huwa anadai yupo busy kwenye mikutano. Sasa swali ni kwamba, unafanya mikutano na kina nani kama unawakwepa wawekezaji wako?
Serikali ya Magufuli ilikuwa imeanza kuwachunguza. Ilidhani wanauzia watu mashamba ya maharage ambayo hawana. Kwa kuogopa walikuwa wamestisha kuwauzia watu. Baada ya Rais Magufuli kufariki, wakaaza kuwauzia tena watu. Nina wasi wasi kama kweli wana hekari za kutosha za maharage na inaonekana ndio maana hawakutangaza kiasi walichopata.
Kampuni ina kila adalili za ubabaishaji. Wewe hata usiende mbali. Mtafute manager wao..ongea naye kwa week 1. Utajua! Akishajua wamechukua pesa zako anakukwepa.
Nitaendelea kufatilia zaidi na kutoa update kadri ntakavyowasoma. Kwa sasa sitashauri watu wasiwekeze kwao. Ntasema tu watu wawe makini. Kama kuna kitu chochote ntakachojifunza zaidi chenye kunionesha mambo tofauti na haya niloandika ntakisema hapa. Ila kwa sasa, haya ndo nimeona. Hakuna kampuni duniani haithamini wawekezaji. Ukiona kampuni ya hivyo, ni dalili za uhuni.
Watanzania kwenye hizi scheme wengi ni wapigaji....Fuatilia mkuu ili uokoe wengine wasipigwe ,niliwaona hawa JATU wakifanya makongamano na Mjomba MPOTO wanauza hisa kwa elfu 5.
Mtindo ule ule wa MR kuku, uliona wapi kilimo au ufugaji wa namna hiyo kwamba wewe utoe pesa ukalale nyumbani usubiri mavuno! Na wanaopigwa ni wazembe tu na lazima mwisho waishie kutapeliwa
Na mimi kuna mtu kawekeza kwao namjua wanamzungusha yeye ashaandaa kabisa zigana yake ina risasi 12 ashanieleza iko siku JATU zitaokotwa maiti tu atafagia wote wasipompa chake mapema.





hakuna jibu unapata linaeleweka ata umtafute CEO wao lugha ni ile ile subiri mchakato 


