kanyagio
JF-Expert Member
- Dec 10, 2009
- 1,021
- 373
siku chache zilizopita nilienda pale Balton (njia ya Coca cola Dar) kufuatilia agricultural inputs mbalimbali, bahati nzuri nilikutana na mzee mmoja ambaye tuliongea mengi sana. Mojawapo ya kssue tuliyoongea ni upandaji wa miti kibiashara- yeye alinieleza kuwa anapanda miti aina ya mifudufudu kwa kitaalamu unaitwa Gmelina Arhobea (white teak). maelezo yake yapo hapa http://www.winrock.org/fnrm/factnet/factpub/FACTSH/Gmelina%20arborea1.pdf
yeye amesema ni miti mizuri na inakubali ukanda wa Pwani.. kama unataka kuiona fika Bagamoyo mjini maeneo ya petrol station , mkono wa kulia kuna kanisa la lutheran (KKKT) na hapo hapo kanisani kuna kitalu cha miti.. kwenye hicho kitalu kuna mifudufudu mikubwa ambayo ina diameter isiyopungua 1meter (ipo tayari kuvunwa).-- in fact nimeshaenda Bagamoyo kwa ajili ya kuona hiyo miti- nimeiona na inavutia sana!!
Alisema miti hii matumizi yake ni mbao na inakuwa tayari kuvuna baada ya miaka 10-12. miti hii inanyoooka vizuri sana kama utakuwa umefanya prunning vizuri na umepanda miche iliyonyooka vizuri.
nimewapigia wakala wa mbegu Morogoro wamenihakikishia kuwa kweli miti hiyo inalimwa kwa ajili ya mbao na kilimo mseto na bei ya kilo moja yenye mbegu zipatazo 1200 ni Tsh 7500. aidha wamesema, ukipanda mbegu hizi zinakuwa tayari kwenda shambani zikifia urefu wa sm 30-45. ila kumbuka mizizi isishike sana chini na ikishika chini lazima ukate mizizi kwa kisu kikali na uiache hapo kwenye kitalu ili ipone vidonda. ukishafanya hivyo miche mingi itapona ukiipeleka shambani. kumbuka kuipanda wakati wa mvua!!
Je kuna mtu ambaye amejishughulisha na upandaji wa miti hii ili tubadilishane taarifa, mawazo na uzoefu?
yeye amesema ni miti mizuri na inakubali ukanda wa Pwani.. kama unataka kuiona fika Bagamoyo mjini maeneo ya petrol station , mkono wa kulia kuna kanisa la lutheran (KKKT) na hapo hapo kanisani kuna kitalu cha miti.. kwenye hicho kitalu kuna mifudufudu mikubwa ambayo ina diameter isiyopungua 1meter (ipo tayari kuvunwa).-- in fact nimeshaenda Bagamoyo kwa ajili ya kuona hiyo miti- nimeiona na inavutia sana!!
Alisema miti hii matumizi yake ni mbao na inakuwa tayari kuvuna baada ya miaka 10-12. miti hii inanyoooka vizuri sana kama utakuwa umefanya prunning vizuri na umepanda miche iliyonyooka vizuri.
nimewapigia wakala wa mbegu Morogoro wamenihakikishia kuwa kweli miti hiyo inalimwa kwa ajili ya mbao na kilimo mseto na bei ya kilo moja yenye mbegu zipatazo 1200 ni Tsh 7500. aidha wamesema, ukipanda mbegu hizi zinakuwa tayari kwenda shambani zikifia urefu wa sm 30-45. ila kumbuka mizizi isishike sana chini na ikishika chini lazima ukate mizizi kwa kisu kikali na uiache hapo kwenye kitalu ili ipone vidonda. ukishafanya hivyo miche mingi itapona ukiipeleka shambani. kumbuka kuipanda wakati wa mvua!!
Je kuna mtu ambaye amejishughulisha na upandaji wa miti hii ili tubadilishane taarifa, mawazo na uzoefu?