Kilimo cha Mitiki: Utaalamu na biashara yenyewe

Wadau habari zenu.

Nimenunua eneo lenye ukubwa wa ekari 10 huko Tanga, lengo ni kupanda michungwa. Lakini kuna wazo la kupanda miti aina ya Mitiki badala ya Michungwa.

Mwenye uzoefu wa miti hii tafadhari nipe ushauri, yaani tathmini kipi kinalipa kati ya michungwa na mitiki. Najua mitiki kuvuna hadi ipite zaidi ya miaka 15. Mwenye uzoefu anipe tathmini kati ya mazao haya mawili.
 
Kama utapanda mitiki ujue unawekeza kwa wanao sio mbaya sababu ni 30 years. Kama unataka kwasasahivi panda michungwa.
 
Hata mimi nilishawahi sikia tetesi juu ya uyaongeleayo mkuu,ngoja waje wadau kama kina Malila watatoa elimu ya uhakika hapa

Mkuu nimepata wito wako,

Mitiki inahitaji uangalifu sana, ni lazima kufanya utafiti wa kutosha kwenye udongo na hali ya hewa ya eneo husika kabla ya kuotesha miti. Fanya utafiti kwenye soko la ndani kama lipo ili usije ukaanza kulalamika huko mbeleni, pia angalia scale ya shamba unayotaka kuwa nayo. Nina mzee wangu mmoja anataka kuuza mitiki kwa bei ya soko la Dunia wakati ana eka mbili kule Kilombero ndani, nani atanunua? Nilimshauri auze kibongo bongo.

Fuata maelezo ya Watalaam vizuri na usiwe mvivu wa kutembelea mashamba ya serikali au hata ya watu Binafsi kule Kilombero/Mtibwa/Longuza/Lindi. Mimi nilifika Kilombero Teak co, na nikafikia uamuzi sawa na nilivyoona. Ninayo mawasiliano ya wauza mbegu wa serikali.

Hakuna mavuno bora chini ya miaka 20, hata kama ni nguzo za umeme, ila unaweza kupata boriti kwa kazi za kawaida kabisa kwa muda wa chini ya miaka 15 hivi. Hapa tunazungumzia uhalisia sio nadharia, twendeni shambani tukapate taarifa sahihi.

Habari za Benki kukopesha wakulima wa Mitiki nazisikia sana, changamoto iko kwenye document na ukubwa wa shamba sio mitiki yenyewe.
 
Mkuu nimepata wito wako,

Mitiki inahitaji uangalifu sana, ni lazima kufanya utafiti wa kutosha kwenye udongo na hali ya hewa ya eneo husika kabla ya kuotesha miti. Fanya utafiti kwenye soko la ndani kama lipo ili usije ukaanza kulalamika huko mbeleni, pia angalia scale ya shamba unayotaka kuwa nayo. Nina mzee wangu mmoja anataka kuuza mitiki kwa bei ya soko la Dunia wakati ana eka mbili kule Kilombero ndani, nani atanunua? Nilimshauri auze kibongo bongo.

Fuata maelezo ya Watalaam vizuri na usiwe mvivu wa kutembelea mashamba ya serikali au hata ya watu Binafsi kule Kilombero/Mtibwa/Longuza/Lindi. Mimi nilifika Kilombero Teak co, na nikafikia uamuzi sawa na nilivyoona. Ninayo mawasiliano ya wauza mbegu wa serikali.

Hakuna mavuno bora chini ya miaka 20, hata kama ni nguzo za umeme, ila unaweza kupata boriti kwa kazi za kawaida kabisa kwa muda wa chini ya miaka 15 hivi. Hapa tunazungumzia uhalisia sio nadharia, twendeni shambani tukapate taarifa sahihi.

Habari za Benki kukopesha wakulima wa Mitiki nazisikia sana, changamoto iko kwenye document na ukubwa wa shamba sio mitiki yenyewe.

mkuu nimekupm
 
Habari wa jf..nilikua nauliza wapi naweza pata miche ya mitiki hapa dar es salaam au maeneo ya jirani mkoa wa pwani..
 
Kama unahitaji miche ya mitiki (stamps) kwa shehena yoyote ile wasiliana nami bei sh200 unaletewa mpaka nyumbani na kama utahitaji msaada zaidi wa namna ya kupanda nitatoa hiyo service free of charge na kama utahitaji kupandiwa ninao vijana wazoefu kwa kazi hiyo.
cc julisa gwijimimi n.k
 
Last edited by a moderator:
Kisima

Unapatikana wapi naomba nitumie ktk pm namba yako tuwasiliane. Mm nipo dar es salaam
 
Kisima

Unapatikana wapi naomba nitumie ktk pm namba yako tuwasiliane. Mm nipo dar es salaam

Nipo Moro mkuu na upandaji wa miti ni moja ya shughuri nifanyazo.
Nitakupa abc za namna gani hii miti inapandwa.
Nimekutumia mawasiliano yangu tayari.
 
Je miti ya MITIKI inaweza kulimwa Mwanza? Naombeeni msaada

Hapana mkuu mitiki inastawi vzr ukanda wa joto kiasi. Nafikiri utakuwa unapafahamu shamba la miti Buhindi, huko walipanda mitiki ya majaribio zamani sana miaka ya 1980s lakini matokeo yake hayakuwa mazuri sana make miti ilidumaa tu bila kujaza kiini chenye kipenyo kinachoshauriwa kwa muda maalum.
Nakushauri panda saipras kama wafanyavyo wenyeji wa mkoa wa mwanza hasa kule sengerema na baadhi ya vijiji vya mkoa wa geita vilivyo pembezoni mwa wilaya ya Sengerema.
 
kaka Malila hizo Mbegu za PINES/Mlingoti kutoka Zimbabwe ZINAPATIKANA wapi? Nazihitaji saana
 
Wadau habari zenu.

Nimenunua eneo lenye ukubwa wa ekari 10 huko Tanga, lengo ni kupanda michungwa. Lakini kuna wazo la kupanda miti aina ya Mitiki badala ya Michungwa.

Mwenye uzoefu wa miti hii tafadhari nipe ushauri, yaani tathmini kipi kinalipa kati ya michungwa na mitiki. Najua mitiki kuvuna hadi ipite zaidi ya miaka 15. Mwenye uzoefu anipe tathmini kati ya mazao haya mawili.

Hongera sana mkuu.kwa ushauri kdgo mana hata mm niko tanga,wilaya ya korogwe.kuhusu mitiki ningekushauri kama hill shamba lako lipo kwenye bonde kdgo na udongo mweusi,lkn kama ukiweza kupanda mikaratusi utakula hela nzuri mapema zaidi ya mitiki na maeneo mengi ya huku kwetu ya stawi vzuri.mi nashukuru nimeanza kupanda mwaka huu tena kipindi hichi cha mvua na pia nakushauri upate miche ya mda mfupi(miche ya kikonyo)
 
Kama unahitaji miche ya mitiki (stamps) kwa shehena yoyote ile wasiliana nami bei sh200 unaletewa mpaka nyumbani na kama utahitaji msaada zaidi wa namna ya kupanda nitatoa hiyo service free of charge na kama utahitaji kupandiwa ninao vijana wazoefu kwa kazi hiyo.
cc julisa gwijimimi n.k

Habari za humu ndani!!!! Nahitaji mawasiliano ya bwana kisima mwenye miche ya mitiki
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom