Miti yote inahitaji mbolea
Hongera sana Mkuu FUSONimepitia uzi huu mwanzo mwisho - napenda kuwafahamisha pia kwamba na mimi ni mwanachama wa kilimo cha Mitiki - nimepanda heka mbili mwaka huu, plan ni kupanda heka mbili mbili kila mwaka - wazo ni kufikisha heka 20. Kilimo changu nafanyia Tuliani Morogoro.
Nimepanda 2.5m space.
Kwa hiyo kwa 70m urefu wa heka (Kizamani) ni miche 28
Kwa heka ya mita 70 kwa 70 ni jumla ya miche 784.
Nawashukuru wachangiaji wote kwa mawazo mazuri, na kuhusu miaka 7 - 40 ili kukomaa hilo si tatizo kwangu maana pia na mimi ningefurahi kama baba yangu angelinifanyia hili ili na mie nipate pa kuanzia, so its not bad if i do this to my kids.
Hata mie mwenyewe who knows, nani anajua siku ya kundoka duniani... Lets go for 40 yrs investment.