Kilimanjaro Express Kuanza Safari za Usiku

Abiria ndio ataamua apande treni, basi, bajaji, bodaboda au atembee kwa miguu hadi Arusha.
Acha mlaji/mtumiaji/abiria ndio aamue.
✊hell yes to free market economy acha soko lenyewe lijiendeshe atakayeshindwa ku compete afee.
Huu ndo ule ujima wa kuzui watu wasiuze maindi nje kisa watakufa njaa
 
Buses wako rough. Kinachowazuia mchana ni uwepo wa Askari wengi na tochi. Sasa usiku watakuwa huru kucheza rafu zao unafikiri madhara hayatakuwepo? Mabasi mengi yanaendeshwa na machizi fresh hawajali watumiaji wengine hasa wenye magari madogo.
Sijawahi ona KLM wapo rough.

Labda kampuni nyingine.
 
Hapa tunazungumzia mabasi kusafiri usiku. Sio KLM.
KLM ni moja ya kampuni ya mabasi ambao wameanza safari za usiku.

Sio kila basi linaendeshwa rough.

Mengi ni yanayoenda nyanda za juu kusini na kanda ya ziwa ndo yapo rough sana.

Kaskazini wastaarabu kidogo.
 
Dodoma ndio ilikuwa moja ya chanzo za safari za usiku kufutwa...
Mkuu rudisha avatar picha yako ya Michael Jackson thriller
maxresdefault (2).jpg
 
Hii ni hatua nzuri ya kukuza uchumi,saa 2 4 uchumi unazunguka!
1.Wenye basi anasafirisha abiria mchana na usiku.
2.Anaye uuza chakula, atauza mchana na usiku.
3.Vituo vya mafuta,watauza mchana na usiku.
4.Maduka yakiuza mpaka usiku
5.TRA watapata mapato zaidi
Nchi jirani usafiri upo mchana na usiku.

Utaratibu wa kuongeza muda wa kufanya shughuli za kiuchumi, ni sawa na mwenye kiwanda afanye uzalishaji usiku na mchana(unaongeza uzalishaji,kipato na ajira).
"Tumechelewa sana" kwa kukosa ubunifu na mbinu za kuchangamcha ukuaji wa uchumi na kufungua fursa!
 
Kwa wachaga uko wakiuza na mvinyo itapendeza,ishu ni kuchimba dawa,wangekua na vyoo kama Scandinavia enzi hizi,ingependeza zaidi
 
Enzi hizo Dar to Iringa gari ilikua inaondoka saa mbili usiku pale mnazi mmoja Iringa Stand saa Moja asubuhi
 
KLM ni moja ya kampuni ya mabasi ambao wameanza safari za usiku.

Sio kila basi linaendeshwa rough.

Mengi ni yanayoenda nyanda za juu kusini na kanda ya ziwa ndo yapo rough sana.

Kaskazini wastaarabu kidogo.
Kama umeamua kubishana sawa. Nazungumzia mabasi in general. Si ya kaskazini wala nyanda za juu,most buses ziko rough.
 
Siku ikifika imefika tu. Hata kama ulisimama dukani kwa Mangi, kuna dereva mmoja tu break zitafail atakuparamia.

Ya Dar - Arusha? Watamwaga Wami au? Acha kuwa na mawazo hasi babu
Zamani ndio ilivyokuwa.. tena barabara zikiwa zimejaa pot holes za kutosha, vumbi la kutosha, speed 70 to 80 km/h .
 
Unaondoka saa 2 usiku saa mbili asubuhi unafika. Unafanya shughuli zako jioni unageuza tena.

Wenye Guest house watapata tabu sana. Usingizi tutamalizia kwenye basi.
Wenye Guest lazima watahujumu safari za usiku, maana wateja wao watapunguwa sana na wao kupata faida kiduchu!!
 
ABIRIA MKILALA DEREVA ANAWEKA GARI PEMBENI NA YY ANALALA..! MNASHTUKA ASUBUHI NDO KWANZA MPO PICHA YA NDEGE..🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom