beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Bweni la Shule ya Sekondari ya Kaloleni Islamic inayomilikiwa na Africa Muslim Agency limeteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo ikiwa ni mara ya 3 kwa Shule hiyo kuungua.
Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Jeremiah Mkomagi amesema moto huo mkubwa ulianzia kwenye chumba ambacho hutumika kama stoo.
Ameeleza, "Ni bweni la ghorofa moja na wakati tunafika tulikuta 'wing' ya kwanza vyumba 6 vyote vimeshika moto, tulipambana na tukauzima huo moto kwenye saa 5:45 usiku"
Amesema "Chanzo hakijabainika kwa sababu kumekuwa na mlolongo wa shule kuungua na hii ni mara ya tatu, tunaendelea na uchunguzi wa kina ili kujua kwanini hizi shule zinaungua mara kwa mara"
Kwenye tukio hilo hakuna majeruhi wala kifo kwa sababu wanafunzi waliondolewa mapema na kupelekwa sehemu salama, vitu vilivyoungua ni nguo zao, vitanda na madaftari
Mkaguzi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Jeremiah Mkomagi amesema moto huo mkubwa ulianzia kwenye chumba ambacho hutumika kama stoo.
Ameeleza, "Ni bweni la ghorofa moja na wakati tunafika tulikuta 'wing' ya kwanza vyumba 6 vyote vimeshika moto, tulipambana na tukauzima huo moto kwenye saa 5:45 usiku"
Amesema "Chanzo hakijabainika kwa sababu kumekuwa na mlolongo wa shule kuungua na hii ni mara ya tatu, tunaendelea na uchunguzi wa kina ili kujua kwanini hizi shule zinaungua mara kwa mara"
Kwenye tukio hilo hakuna majeruhi wala kifo kwa sababu wanafunzi waliondolewa mapema na kupelekwa sehemu salama, vitu vilivyoungua ni nguo zao, vitanda na madaftari