Kilichojiri bungeni Tarehe 13 April (Muswada wa mafao)

CDM wasingepiga kelele. Makosa ya CCM kwao ni mtaji. Tuwashukuru wabunge wa CDM kwa kukaa kimya. Kwa kupitisha sheria haramu na kandamizi kama hii, CCM wamejiongezea maadui na kufifisha hali yake ya kukubalika kwa wafanyakazi. Kwa maneno mengine, wamechimba na kusakafia kaburi lao wenyewe. Ukweli hata wakiifuta leo, tayari wameshatujeruhi kisaikolojia.
 
hakuna watu wanyonge nchi hii kama wafanyakazi, mtu anaweza kusema wakulima, lakini ukiangalia kodi ya m/kazi kwa serikali ni kubwa sana.LEO HII CHADEMA WAMETUACHA HEWANI

Acheni unafki nyinyi, pension ni kwa faida yenu, mbona wafanyakazi wa serikali kuu hawalalamiki na pspf yao. CHADEMA CHADEMA. Kazi ya wabunge wa CHADEMA ni kutetea maslahi ya wananchi na siyo kutetea watu wasioelewa faida za pension zao kama ninyi bali kukuelimisheni ili muelewe. Ka vipi acha kazi uone ka kuna mtu atakukata pension
 
ule mswaada hauna kipengere hicho ..kilichomekwa baada y kusainiwa kuwa sheria...

mkuu nimekuwa nikijiuliza maswali sana kuwa hivi hiyo section cdm hawakuiona pamoja na umakini wao wote? ed tupe data walichomeka vp?
 
Hii acha ilambe kwetu maana sisi wafanyakazi ndo huwa tunatumia nguvu kubwa kuchakachua kura. Na huwa tunasimama kidete ile mbaya! Ngoja tuipate fresh! DUGUNYA!
 
Hivi siku zote unadhani Chadema wapo kwa ajili ya kusaidia wananchi hawa Chadema wapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi.

unataka kutuambia CDM mara nyingine wapo kwa maslahi ya wananchi? Je, CCM wapo kwa ajili ya nani? Ni serikali inayoongozwa na chama gani ndiyo iliyowasilisha mswada uliopelekea sheria hiyo? Ni kweli CDM hawakuliona hilo; lakini serikali ya CCM ndio wakulaumiwa kwa kuandaa sheria kandamizi dhidi ya wafanyakazi?
 
Hili ni swala la msingi kabisa kujiuliza... Je hawa wapinzani walikuwa wapi wakati hii sheria inapitishwa? Au ni kwasababu haiwaathiri?

Nahisi hawakuwa bungeni, walikuwa bize na M4C kampeni
 
Hivi siku zote unadhani Chadema wapo kwa ajili ya kusaidia wananchi hawa Chadema wapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi.

Una akili sana mkuu.
Yesu alikuja ili tuwe na uzima, kisha tuwe nao tele.
 
unataka kutuambia CDM mara nyingine wapo kwa maslahi ya wananchi? Je, CCM wapo kwa ajili ya nani? Ni serikali inayoongozwa na chama gani ndiyo iliyowasilisha mswada uliopelekea sheria hiyo? Ni kweli CDM hawakuliona hilo; lakini serikali ya CCM ndio wakulaumiwa kwa kuandaa sheria kandamizi dhidi ya wafanyakazi?

Wasingeweza kuona maana haikuwepo! Limechomekwa baada ya kupitishwa na bunge!
 
Mimi ni kati ya watu niliomuunga mkono dr.slaa wakati kugombea urais lakini pengo lake bado linaoneka pamoja na hoja moto moto zinazotolewa na wabunge wa upinzani bado pengo lake linaonekana naamini kwa hoja kama hii dr angeshawawashia moto lakini kuna mambo mengi yanapitishwa kimya kimya huku wabunge wetu waking'ang'ania hoja zile zile tulizozoea
 
Magamba mngejua msivyopendwa na wananchi,suburini 2015 chozi litakavyo watoka.
 
Hivi siku zote unadhani Chadema wapo kwa ajili ya kusaidia wananchi hawa Chadema wapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Ni kama vile Magamba ambao wao wapo kwaajili ya kuwaangamiza wananchi kule Mabwepande!
 
Ndugu zangu wana jf,nimeshangazwa sana na kusikitishwa sana na sheria mpya ya SSRA juu ya mafao ya wafanyakaZI,NIMESIKITISHWA SANA NA WABUNGE AMBAL TUNAWAONA KAMA WATETEZI WETU KUPITISHA SHERIA HII KIMYA KIMYA WAKIJUA KUWA WAO HAIWAATHIRI... NA KWAKWELI HAPA NAMAANISHA WABUNGE WA UPINZANI HASA HASA CHADEMAA, Hapa namaanisha akina ZITO,MNYIKA,TUNDU,MBOWE.MDEE.etal...

SISEMI KUWA MNA UAMUZI WA KUIZUIA MAANA HAIWEZEKANI MAANA WA NDIOOO wengi lakini angalau mngepaza sauti tungewawikia. Lakini kwa sasa mtawaambia nini wa Tz?

I must admit,i am utterly disappointed with you guys... you havent done your home work properly..

Ngoja nikueleze ndugu, mswada huo ulipopitishwa wabunge wa CDM hususani Mh Mnyika walijitahidi sana kutaka mabadiliko katika vipengele vingi sana vya mswada huo lakini wabunge wenzao wa upande wa pili hawakukubali. Hili nililishuhadia bungeni, hasa CAG alikuwa akisimama kukwamisha hoja nyingi za Mh Myika.
 
Vyama vyetu vya wafanyakazi ndio bure kabisa. Hebu angalia chama cha wafanyakazi cha Afrika Kusini! Kina-influence hata ya kumpata rais wa nchi. Sisi vyama vyetu mabuda buda tu. Tuunde chama kingine cha wafanyakazi. wanachukua hela za wafanyakazi kula tu, hawatoi miongozo yoyote. Waliitwa kwenye utunzi wa hii sheria, wakapewa allowance ya kikao wakatulia wakapitisha, sasa tunalia. Kikwete akiwatisha tu wanayeyuka. Napendekeza Dr. Ulimboka akirudi tufanye kikao na kada zote za wafanyakazi tuanzishe chama tofauti na hivi tulivyo navyo. Ikiwezekana COTU tuifumui kabisa. Tunahitaji mabadiliko.
 
Hivi siku zote unadhani Chadema wapo kwa ajili ya kusaidia wananchi hawa Chadema wapo kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
Eh!na wewe mbunge wa CCM ambae upo kwa ajili ya kusidia wananchi ulichukua hatua gani kuzuia sheria ya kidharimu iliyoletwa na chama chako cha kidharimu, zaidi ya kuburuza makalio yako kwenye kiti chekundu na kupiga meza za bunge kama mwendawazimu!
 
kwa vyovyote vile chadema na chama cha wafanya kazi tunawategemea watuongozi juu ya hii sheria ya kijinga yaani mpaka sasa siamini kama ilipita bungeni..
 
Huu utegemezi wa CHADEMA kwenye kila kitu utatupeleka pabaya, kuna siku mtu atapigwa na mke wake alafu asubiri CDM ije imtetee,kama we ni mfanyakazi ni wakati wako wakuonyesha kwamba hukubaliani na hili swala. Chadema wakisema tufanye maandamano ya amani kupinga huu unyonyaji, nyie ndio wa kwanza kusema hiki ni chama cha wapenda vurugu, kwa hiyo subirini hivyo hivyo.
My take:
Nani atakukomboa mwaka huu? Je utaisubiri CHADEMA?
 
Back
Top Bottom