Henry Kilewo
JF-Expert Member
- Feb 9, 2010
- 899
- 1,084
Katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema bwana HENRY KILEWO amesema anawashangaa sana wabunge wa Dar es salaam kumlalamikia magufuli ile hali wao wenyewe wamelala bila hata ya kutambua mamlaka walizopewa, Wameshindwa kulifanya jiji kuwa Active *kwa reaction pale linapotokea jambo la msingi kama hili la wananchi kupandishiwa gharama za usafiri bila kushirikishwa.Wabunge hawa wanapaswa kujilaumu wao wenyewe *kulikuwa hamna haja ya kutoa kauli ya kuwa magufuli awatake Radhi wakazi wa dar es salaam, kilichokuwa kinatakiwa kifanyike ni wao kuwaongoza wananchi wao mpaka kwenye ofisi za waziri huyo bila kujali itikadi za vyama vyao vya siasa na kupigania haki za wanyonge. Kiukweli jiji limepooza sana na limekosa mvuto wa kisiasa ukilinganisha na majiji mengine kama Arusha, Mwanza na Mbeya ambayo yapo juu kisiasa kutokana na wabunge wao kujitoa muhanga kusimamia ukweli kivitendo na siyokupiga kelele kwenye vyombo vya habari. Wabunge hawa wanapaswa kujitambua ya kuwa wanaongoza jiji lenye changamoto mbalimbali na katika kukabiliana na changamoto hizo wanapaswa kuwa wajasiri kusimamia ukweli. Dunia ya sasa imebadilika si kila kitu chakupeleka bungeni kufuata eti taratibu za sheria za kuombana radhi ama kutakana radhi, Kama mtu amekiuka maadili ya utu hamna haja ya kumfanyia utu maana magufuli alipotamka maneno hayo alikuwa na akili timamu ya nini kusubiri bunge? ile hali yupo ndani ya jiji mnaloliangoza? mimi ninaamini njia sahihi ya kupinga dhuluma hii ya wasiyonacho kuonewa na wenye mamlaka ya juu ni maandamano ya siyo na kikomo ili iwefundisho kwa wengine. Thamani ya utu wa mwanadamu haiwezi kupiganiwa kwa kelele zisizo kuwa na vitendo. Wabunge hawa waache uoga wawaongoze wananchi kulinda thamani ya utu wao, kwani alichofanya magufuli ni kebehi na dharau kubwa sana kwa wawakilishi wa wananchi wa dar es salaam. Tupoleni sana wakazi wadar es salaam kwa dharau hii kubwa tuliyoonyeshwa na waziri huyu, tusife moyo tunaweza kujiongoza wenyewe kupigania haki zetu za msingi bila hata kusubiri wa wakilishi wetu kutuongoza katika hili. twendeni mbele tusirudi nyuma na harakati hizo lazima zianze sasa, si kwa maana ya uovu, ni kulinda dhamani ya utu wetu na kuwafundisha wenyedharau kuwa na adabu kwani huenda wengine hawajawahi kufundshwa adabu na wazazi wao licha ya kuwa viongozi watawala. Asanteni sana na mungu atubariki by HENRY J KILEWO; KATIBU CHADEMA MKOA KINONDONI NA KANDA YA DAR ES SALAAM.KIL |