Kilewo: Wabunge wa Dar acheni kulalamikia kauli ya Magufuli, chukueni hatua

Haraka haraka unaweza kumuona Magufuli kama Kichaa ama mtu alielewa madaraka, lakini mimi namtizama kama mtu shujaa , anaetaka kusimamia yale ambayo ndio msimamo wa ccm na ndio vile ambavyo cabinet imekubaliana ndani ya vikao vyao vya siri .


Wanaccm wengi wamekua wakiunga mkono swala la kuongezewa posho kwa wabunge wao, ingawa kunakurushiana maneno juu ya hili, lakini ukweli unabaki swala hilo la posho linabaraka la wajumbe wengi wa NEC ya ccm , na huenda hata Bwana Mkubwa pale kitalu namba moja anahusika.

Hatujasikia kauli madhubuti za Viongozi waandamizi kukataa posho hii, japo Nape aliwahi kutoa msimamo wake binafsi juu ya swala hilo.

kwanini Magufuli kaongeza gharama za Nauli pale Kivukoni ?
Ameongeza kwakua anatafuta pesa za kufidia pesa watakazaongezewa wabunge wetu KAMA AMBAVYO MMESIKIA, ameamua kuongeza vyanzo vipya vya mapato ili kuweza kuifanya serikali kumudu gharama za kuendesha Bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania.
Hata hili ukute linabaraka za wakubwa , na tusubiri kupanda kwa rate za ushuru maeneo kadhaa. kelele za wabunge wa ccm kule Kigamboni na Ilala ni ukosefu wa kumbukumbu kwamba ni wao wanaolimbikiza madeni kwa serikali na waache kutafuta sifa kwa matatizo ya wananchi.
Viva Magufuli, unatekeleza Ilani ya CCM ipasavyo, na Bado cha moto tutakiona.

Mkuu, vipi kuwa lugha ya jeuri kwa watu? Yeye kama kiongozi alitakiwa kuelezea sababu ya ongezeko la 100%. Ukiwa kiongozi vitu hivi ni muhimu sana. Vile vile, kuhusu ubadhirifu wa makusanyo mbona hajaongelea?
 
Mkuu, vipi kuwa lugha ya jeuri kwa watu? Yeye kama kiongozi alitakiwa kuelezea sababu ya ongezeko la 100%. Ukiwa kiongozi vitu hivi ni muhimu sana. Vile vile, kuhusu ubadhirifu wa makusanyo mbona hajaongelea?
Ndio Lugha za wanaccm wote hizo baada ya kushinda chaguzi , daima kejeli na matusi ndio lugha tulizozizoea, huwezi kutenga magufuli na CCM , hiyo ndio rangi yao halisi

 
Tatizo ni kuweka siasa kwenye kila kitu, katika WABUNGE hawahawa kuna mmoja alimuwakia Prof Tibaijuka juu ya wakazi wa Jangwani eti hatakubali wapiga kura wake wanyanyaswe, hao hao wamechukuliwa na mafuriko juzi wengi wakapoteza Mali na maisha Yao. Mbunge yule Yukon wapi sasa? Jiji hili kutwa lina kero kibao; foleni, usalama, ujenzi holela, sewage system mbovu...kwa nini wabunge hawaungani kukabili shida hizo kwa kuiwekea pressure serikali kutatua matatizo hayo kwa mji huu mkuu wa nchi kibiashara? kwani like it or hate it, Dar is the heartbeat of this country! Dar deserves better than this...
tatizo jingine ni hao wanaoongozwa hawajitambui wanapelekwapelekwa tu na hao wachumia tumboni...wapiga kura wa temeke acheni hizo! amkeni mjiletee development...mbona mdundiko na sare za harusi kila siku mnashona MIA iwe tabu!!
 
Dr. John Pombe Magufuri mguu ni mbele hakuna kurudi nyuma, achana na hao wabunge ambao wana play siasa za maji chooo.
 
Na Mwandishi Wetu

SAKATA la nauli mpya ya kivuko cha mv Magogoni limechukua sura mpya baada ya mfanyabiashara maarufu nchini, Azim Dewji kuwajia juu wabunge wa mkoa wa Dar es Salaam, akiwataka kuacha kumshambuliaji Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli na badala yake wahangaike kutatua matatizo ya msingi ya wananchi katika majimbo yao.

Wabunge hao wakiongozwa na Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, juzi walizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa, kitendo cha Magufuli kutangaza ongezeko nauli ya kivuko hicho kwa asilimia 100 bila kushirikisha wananchi, hakina tofauti na udikteta.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Dewji alisema wabunge hawapaswi kupinga kila jambo kwa lengo la kujijenga kisiasa na kusisitiza kuwa Magufuli ana hoja za msingi, hivyo aungwe mkono kwa lengo la kuboresha usafiri wa majini katika eneo hilo na jiji la Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi.

"Jamani, ongezeko la sh 100 linaleta chokochoko za nini? Leo hii hata ombaomba ukimpa sh 100 anaweza kukurushia usoni. Wanalalamikia shilingi 100 wakati wao walijiongezea posho za laki mbili hawakuona ubaya wowote…nadhani wabunge wa Dar es Salaam walipaswa kumuunga mkono Magufuli ili kivuko kijiendeshe na kutoa huduma bora na za kudumu, badala ya kila kitu kutegemea kitoke serikali kuu.

"Hivi kila kitu kikitoka serikalini, fedha nyingine za maendeleo zitatoka wapi, kama si kuishia kuziba mapungufu kama yanayojitokeza kwenye vivuko vyetu vinapoharibika?" alihoji na kusema kama fedha zisipokusanywa, na vivuko vikapata hitilafu na kushindwa kutoa huduma, watakuwa wa kwanza kudai serikali imewasahau wana-Kigamboni.

Alikwenda mbali zaidi na kusema kuwa, pesa zitakazokusanywa kutokana na nauli mpya zitachangia pia kulipa ongezeko la posho za wabunge, kwa kuwa ni fedha za wananchi na wabunge wanalipwa kutokana na fedha za walipakodi.

"Daladala zinapanda kila kukicha, hatusikii kelele, sasa angalia, Waziri Magufuli amesema kwa mara ya mwisho bei ya kuvuka kwenda na kutoka Kigamboni ilipandishwa miaka 14 iliyopita, hawaoni kuwa bei hiyo imepitwa sana na wakati?

"Na mbaya zaidi nasikia wanataka wakabidhiwe kazi ya kuendesha kivuko, mbona baadhi yao majimbaoni mwao tayari mambo yameanza kuwa ya shingo, hayaendi kabisa. Nadhani wangejikita katika kustawisha majimbo kwanza, wakishamaliza ndipo waombe kusaidia kazi za wengine, huu kwao si wakati sahihi wa kutoa msaada," alisema na kuhoji kwanini wasizungumze kumaliza kero nyingine za jijini, ikiwemo foleni.

Kauli ya Dewji, aliyekuwa anazungumza kwa hisia kauli, huku akisisitiza wabunge kuacha kudandia mambo kwa lengo la kupata umaarufu aliouita wenye kuwajenga zaidi kisiasa badala ya kuwanufaisha wananchi wa kawaida, imeibuka huku kukiwa na mjadala mkali tangu kupandishwa kwa nauli za kivuko cha Magogoni.

Jumapili iliyopita, Dk. Magufuli alitangaza kuwa, serikali imeamua kupandisha nauli hiyo kutoka kati ya sh 50 na Sh 100 hadi sh 200 kwa safari moja ya kivuko hicho, kutokana na gharama za uendeshaji kuwa juu. Alisema nauli iliyokuwapo ni ya tangu mwaka 1997, huku nauli ya vivuko vingine zaidi ya 30 nchini imekuwa ikipanda mara kwa mara.

Magufuli alisema kivuko cha Magogoni kimekuwa kikitoza nauli za chini ikilinganishwa na Chato, kinachotoza sh 300, Pangani Sh 200, Kisorya Sh 300, Lugolora Sh 500, Nyakarilo Sh 300, Chato-Bukombo Sh 2,000, Kirambo sh 500 na Utete Sh 300, huku wanafunzi wakisafiri bure.

Sambamba na upandishaji nauli kwa watu, pia nauli ya magari imepanda ambapo madogo yatatozwa Sh 800 na Sh 1,500, pick up sh 1,000 na Sh 2,000 na yale ya kuanzia tani tatu na nusu Sh 5,000 hadi Sh 7,500.


TUESDAY, JANUARY 03, 2012 ~ COPYRIGHT: MICHUZI BLOG

"Wabunge wa Dar es Salaam wanafikiri kwa kutumia makalio"
 
Tatizo ni kuweka siasa kwenye kila kitu, katika WABUNGE hawahawa kuna mmoja alimuwakia Prof Tibaijuka juu ya wakazi wa Jangwani eti hatakubali wapiga kura wake wanyanyaswe, hao hao wamechukuliwa na mafuriko juzi wengi wakapoteza Mali na maisha Yao. Mbunge yule Yukon wapi sasa? Jiji hili kutwa lina kero kibao; foleni, usalama, ujenzi holela, sewage system mbovu...kwa nini wabunge hawaungani kukabili shida hizo kwa kuiwekea pressure serikali kutatua matatizo hayo kwa mji huu mkuu wa nchi kibiashara? kwani like it or hate it, Dar is the heartbeat of this country! Dar deserves better than this...

Yaani unaweza kuona uongozi wa pamoja wa wabunge wetu wa Dar es Salaa! kama siyo wabunge wote, viongozi wengi wa kuchaguliwa hapa Tanzania.

Wameungana pamoja kutetea nauli za kigamboni, kwa maslahi ya kisiasa kama alivyosema mh. Dewji na si jingine.

Nilisikia kwenye redio, wapo redio kwamba kuna zahanati / hospitali inayoitwa Tungi Kigamboni, dawa za mseto wanazo dozi kumi kwa ration ya miezi mitatu, daktari kwa sasa yupo likizo hakuna wa kumshikia nafasi yake, maabara haina mpimaji vipimo, ukiugua wanabashiri huu utakuwa ni ugonjwa fulani, halafu unaandikiwa dawa ya kununua duka la dawa.

Zahanati hiyo ipo Kigamboni, lakini mbunge wa eneo hana habari kushughulika na matatizo hayo na mengineyo.

Ukiwauliza hawa wabunge, kazi za msingi walizo ahidi kufanya, hawajafanya chochote kwa tathimini ya mwaka mmoja waliopo madarakani.

Mbunge wangu, madaraja yameharibiwa na mvua, barabara zimeharibika, lakini mbunge wetu hajafanya mkutano wowote na wapiga kura wake, lakini amepata muda wa kwenda press conference.

Tunaweza kujiuliza swali la msingi Tanzania, hivi viongozi wa kuchaguliwa, wabunge, serikali za mitaa, madiwani wanaonyesha uongozi wowote? Au uongozi hauwezi Tanzania ? Basi kwanini tunapoteza muda kuchagua viongozi ??
 
nimefungua uzi huu kwa jazba balaa. kumbe mwandishi tupo pamoja. kikwete na timu yake wapuuuzi sana.
 
Kutokana na kauli na maaumuzi magumu na ya kijasiri ya Mh Waziri Magufuli juu ya kupandisha nauli ya kivuko cha kwenda kigamboni Watanzania wengi wenye mtizamo wa kimaendeleo wanaona ni vyema sasa nchi ikapata kiongozi dikteta atakayesimamia maendeleo ya nchi kiubabe kama alivyo Magufuli.

Mh Magufuli amezidi kuonyesha ujasiri wake hadi kwa kupingana na wabunge wa chama chake katika kusimamia msimamo wake kwani wabunge wa Dar katika sakata hili waidhirisha dhahiri kauli ya meya wa Jiji kuwa wanafikiria kupitia Makalio kwani badala ya kuwaongoza wananchi waliowachagua kupinga mchakato wa katiba na kupanda kwa bei za vyakula kama mchele, dagaa, unga, mafuta ya kula, sukari etc wanaibuka kupinga ongezeko la nauli.

Hivi huyu mbunge wa Kigamboni alishawahi kupinga hata ongezeko la posho za wabunge jibu ni hapana sasa anawalaghai watumishi kwa kuungana nao kupinga ongezeko la nauli ya kivuko tu na sio kupinga ongezeko la gharama za Maisha kwa ujumla.

kutokana na kauli ya Magufuli naona sasa imefika wakati wa nchi hii kutawaliwa kidikteta ili kufanikisha maendeleo ya nchi kwani siasa zimekuwa nyingi kuliko utendaji hongera Magufuli simamia msimamo wako wasio taka wapige mbizi au wachonge mitumbi yao;
 
Dr Magufuli anawachanganya hawa jamaa,maana wanataka wapewe panton ili wauze kama UDA,hakuna hakuna wamezidi kupenda vya kunyonga hao mafisadi wa jiji
 
GreatThinkers,

Sishangai kuona wapiga mabenchi hoja imepita wanamuona Magufuri amelewa madaraka, Magufuri amejibu ipasavyo na hiyo nauli ni heri ipande!
Huo ni upunguani mkubwa kubisha Sh.200 hilo Daraja mnalolitaka mtaliweza kulilipia?

WanaKigamboni,Mjimwema,Kibugumo,Gezaulole,Mwongozo,Dege,Gomvu,Ngobanya,Kimbiji, Kidagaa,Kisarawe,Kibada na hata mbutu kwa nini hamlalamiki wanaotekenya na kushort circuit kwenye Umeme na mafuta?

Huo ndio Upeo wa Mtemvu(Tmk) na Ndugulile(Kg) si kila kitu ulizishe wananchi, Sishangai kuona Zunga nae alikataa watu wasihame Jangwani leo hii watu 40 wamekufa na wengine wamepotelea Baharini hilo kwenu mnalichekelea. No way Magufuri was Right

Nauli ya Daladala yenyewe kituo hadi kituo ni bei gani achilia mbali Diesel inayotumika ktk zile Feri ni ile ile ya Sh.2000/lt inayotumika ktk Daladala kwa nini hamkatai. nani ajuaye ktk Utendaji zile ni four stroke Engines, kila combustion inakula kiasi gani cha mafuta kumbuka ni Twin screw namaanisha zinatembea Engine mbili pamoja(simulteneously).

Kama mnaona haifai sisi Kanda ya ziwa Kigongo-Busisi tunalipa Tsh 400 badala ya Tsh.300 lakini inamake sence. Hamtaki kulipa Magufuri Relocate hiyo fund uje ujenge Daraja hapa Busisi So far hapa tunahitaji zaidi kuliko hao wanaotaka kwenda kujirusha Amani beach,Ras kutani,Baracuda na Kipepeo beach.

Hapa Busisi kuna trucks(malori) zaidi ya 500 kila siku yanapeleka mitambo kwenye Migodi ambayo hata hivyo pesa inayotoka kule manaifaidi nyie manaotaka kujenga mji mpya wa Kigamboni kwa Trilion 30. Tuna Sehemu nzuri tu Luchelele(Rocky City) ambayo inaweza kuwa kivutio hata zaidi ya Kg kwa kuweka daraja kuunganisha upande wa Sengerema. Mahoteli na Sky Scrapers zikajengwa.

Kama siyo mmetumwa na hayo makundi yenu ya Urais basi nyie ni wale wale mnaofanya kampeni chafu zilizo mlengo wa kushoto na mjue hilo hatutalivumilia kuchafua watu kada hiyo, Rais atatoka kada yoyote. Mmeshawaumiza sana watu wa Mbeya sasa mnaona tatizo liko kwa Magufuri na lile fisadi papa la monduli wakati chama chote kimeoza-We can't afford it.

Yote hayo mliyataka wenyewe-CCeM Hoyee, Ubwabwa Mtamu hoyeee, mnakera sana ila ni bore leo nifyatuke ili mjue mnatuboa. Ukitoa Segerea na Ubungo pamoja na Kawe sehemu iliyobaki CCeM inajichanganya na ile Kada inayohangaishwa huku na kule kila awamu. Mnataka nini zaidi?

Mmefanywa maskini wa kufikri watu wanatriger akili zenu, Bei ya Pipa moja lita 200 ni kama dola 90 ambayo ni sawa na sh.130,000 ivi hii bei ni sawa takribani Sh.650 kwa lita kule Uarabuni. kufikisha hapa kwetu inweza fika Tsh. 750 sasa kwa nini hamuhoji bei kuwa Tsh.1800 kwa lita?

Tusibabaishane bwana, Magufuri kweli ni Mbabe lakini huwa mara nyingi yuko sahihi na ni mtendaji sitaki kutoa mifano ni mingi mnaijua.

HITIMISHO:
CCM IMEOZA-KICHAKA CHA MADILI DHARIMU.
Nampa Big Up Hutaki Unaacha endelea hivyo siku nyingine utoe video na picha ktk waraka wako wa pili
 
J. Maguli huyu ndiyo huyhuyu J. Magufuli. Halafu umesema watanzia wengi wanasema wanataka rais dikteta kama Magufuli. Wamesema lini? Naona umetengeneza kifungu cha maneno kisicho na ukweli ndani yake.
 
J. Maguli huyu ndiyo huyhuyu J. Magufuli? Halafu umesema watanzia wengi wanasema wanataka rais dikteta kama Magufuli. Wamesema lini? Naona umetengeneza kifungu cha maneno kisicho na ukweli ndani yake.
 
Hivi zile Boat za Azm Dewji ziliishia wapi?...maana nakumbuka Mh POMBE alizikomalia kweli kweli

Ziko kwenye makumbusho huko Mwanza. Alilazimisha zikapitia Kenya zikafika ziwa Victoria zikaenda Mwanza. Wakati huo SUMATRA nadhani haikuwepo, zilifanya kazi mwezi mmoja tu zikawa chini ya mawe!! Zilikuwa ni boat CHAKAVU kwa maana ya CHAKAVU.
 
Na Mwandishi Wetu

SAKATA la nauli mpya ya kivuko cha mv Magogoni limechukua sura mpya baada ya mfanyabiashara maarufu nchini, Azim Dewji kuwajia juu wabunge wa mkoa wa Dar es Salaam, akiwataka kuacha kumshambuliaji Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli na badala yake wahangaike kutatua matatizo ya msingi ya wananchi katika majimbo yao.

Wabunge hao wakiongozwa na Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, juzi walizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa, kitendo cha Magufuli kutangaza ongezeko nauli ya kivuko hicho kwa asilimia 100 bila kushirikisha wananchi, hakina tofauti na udikteta.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Dewji alisema wabunge hawapaswi kupinga kila jambo kwa lengo la kujijenga kisiasa na kusisitiza kuwa Magufuli ana hoja za msingi, hivyo aungwe mkono kwa lengo la kuboresha usafiri wa majini katika eneo hilo na jiji la Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi.

"Jamani, ongezeko la sh 100 linaleta chokochoko za nini? Leo hii hata ombaomba ukimpa sh 100 anaweza kukurushia usoni. Wanalalamikia shilingi 100 wakati wao walijiongezea posho za laki mbili hawakuona ubaya wowote…nadhani wabunge wa Dar es Salaam walipaswa kumuunga mkono Magufuli ili kivuko kijiendeshe na kutoa huduma bora na za kudumu, badala ya kila kitu kutegemea kitoke serikali kuu.

"Hivi kila kitu kikitoka serikalini, fedha nyingine za maendeleo zitatoka wapi, kama si kuishia kuziba mapungufu kama yanayojitokeza kwenye vivuko vyetu vinapoharibika?" alihoji na kusema kama fedha zisipokusanywa, na vivuko vikapata hitilafu na kushindwa kutoa huduma, watakuwa wa kwanza kudai serikali imewasahau wana-Kigamboni.

Alikwenda mbali zaidi na kusema kuwa, pesa zitakazokusanywa kutokana na nauli mpya zitachangia pia kulipa ongezeko la posho za wabunge, kwa kuwa ni fedha za wananchi na wabunge wanalipwa kutokana na fedha za walipakodi.

"Daladala zinapanda kila kukicha, hatusikii kelele, sasa angalia, Waziri Magufuli amesema kwa mara ya mwisho bei ya kuvuka kwenda na kutoka Kigamboni ilipandishwa miaka 14 iliyopita, hawaoni kuwa bei hiyo imepitwa sana na wakati?

"Na mbaya zaidi nasikia wanataka wakabidhiwe kazi ya kuendesha kivuko, mbona baadhi yao majimbaoni mwao tayari mambo yameanza kuwa ya shingo, hayaendi kabisa. Nadhani wangejikita katika kustawisha majimbo kwanza, wakishamaliza ndipo waombe kusaidia kazi za wengine, huu kwao si wakati sahihi wa kutoa msaada," alisema na kuhoji kwanini wasizungumze kumaliza kero nyingine za jijini, ikiwemo foleni.

Kauli ya Dewji, aliyekuwa anazungumza kwa hisia kauli, huku akisisitiza wabunge kuacha kudandia mambo kwa lengo la kupata umaarufu aliouita wenye kuwajenga zaidi kisiasa badala ya kuwanufaisha wananchi wa kawaida, imeibuka huku kukiwa na mjadala mkali tangu kupandishwa kwa nauli za kivuko cha Magogoni.

Jumapili iliyopita, Dk. Magufuli alitangaza kuwa, serikali imeamua kupandisha nauli hiyo kutoka kati ya sh 50 na Sh 100 hadi sh 200 kwa safari moja ya kivuko hicho, kutokana na gharama za uendeshaji kuwa juu. Alisema nauli iliyokuwapo ni ya tangu mwaka 1997, huku nauli ya vivuko vingine zaidi ya 30 nchini imekuwa ikipanda mara kwa mara.

Magufuli alisema kivuko cha Magogoni kimekuwa kikitoza nauli za chini ikilinganishwa na Chato, kinachotoza sh 300, Pangani Sh 200, Kisorya Sh 300, Lugolora Sh 500, Nyakarilo Sh 300, Chato-Bukombo Sh 2,000, Kirambo sh 500 na Utete Sh 300, huku wanafunzi wakisafiri bure.

Sambamba na upandishaji nauli kwa watu, pia nauli ya magari imepanda ambapo madogo yatatozwa Sh 800 na Sh 1,500, pick up sh 1,000 na Sh 2,000 na yale ya kuanzia tani tatu na nusu Sh 5,000 hadi Sh 7,500.


TUESDAY, JANUARY 03, 2012 ~ COPYRIGHT: MICHUZI BLOG

Hakika Dewji umenigusa siyo siri. Alichofanya Magufuli labda ni approach tu lakini suala la kupandisha lina mantiki tena kubwa sana. Haiwezekani bei iongezwe kwa Sh. 100 halafu eti wabunge wa Dar es Salaam nzima wajifanye wanalalamikia kwa niaba ya wananchi. Mbona wao wanataka waongeze posho ya vikao vya Bunge kutoka Sh. 70,000 hadi Sh. 200,000!!!! Kama huu siyo uhayawani ni nini!!! Watanzania tuwapuuze wabunge hao kwa nguvu zetu zote.
 
Back
Top Bottom