Kilango amwambia waziri kasema uongo!

naona waasisi wa CCJ wanaunganisha nguvu kuiua na kuizika ccm...well done
 
ndo wamefikia huko lakini cha ajabu na kusikitisha hakuna hatua zozote zinazofuatwa baada ya tatizo kutokea..
 
mawaziri wababaishaji huteuliwa na rais m babaishaji. Jeykey ni m babaishaji...
 
Jamani mtujuze..Kilango kaambiwa kuleta ushahidi wa maandishi au..Mama Makinda kasemaje?
 
Kwa wana mageuzi kama kin ZK, TL, GL, HM, PM na wengineo wangekuwa nje muda huu..
 
Asinge weza kuomba kwa sababu n/waziri kakiri kuwa taarifa alizopewa na mkurugenzi zinaweza kuwa si za kweli,ila ameomba waongozane na mbunge kwenda kuangalia hiyo miradi.jamaa kaonesha ukomavu kwa kukiri kudanganya na hii inatokana na kupewa taarifa za uongo na watendaji wake.

Agrey Mwanri namkubali sana pamoja na kwamba anaganga njaa ndani ya Magamba. Lakini mara nyingi yuko mkweli kukiri udhahifu na kuufuatilia akishaambiwa.

Big up Mwanri
 
Mwanri uwa anajifanya anajibu kwa kujiamini sana na kwa speed kumbe wakati mwingine anatudanganya.
 
Asinge weza kuomba kwa sababu n/waziri kakiri kuwa taarifa alizopewa na mkurugenzi zinaweza kuwa si za kweli,ila ameomba waongozane na mbunge kwenda kuangalia hiyo miradi.jamaa kaonesha ukomavu kwa kukiri kudanganya na hii inatokana na kupewa taarifa za uongo na watendaji wake.

Huyo mtendaji aliyempa waziri taarifa za uongo achukuliwe hatua ili iwe fundisho kwa wengine, maana inaonekana wanatudanganya sana hawa! Na bado mawaziri wataendelea kuumbuliwa hivyo hivyo kwa kutegemea watendaji vihiyo na wanaofanya kazi kwa kulipua wawahi vikao vyenye posho.
 
Mawaziri waongo huteuliwa na rais muongo.

Waziri anaposema uongo ili apindishe majibu sahihi kwa makusudi, au kusema uongo kwa kutojua ni upungufu wa kutofuatiria shughuli zake ipaswavyo. Wote hao ni wahalifu kwa taratibu za kiutendaji, kuwajibika ni lazima.Lakini Mkuu wa Kaya kama hawezi kutofautisha baya na jema imekula kwetu.
 
Majibu ya waheshimiwa Mawaziri
Nimemshukuru sana Mh mama Kilango kwa kuwaumbua, baadae saa 7 mchana katibu wao mh mhagama amewaita wabunge wakinamama wote wa CCM, wana kikao chao mama spika amewatangazia!

Kama akikemewa na wenzio ktk kikao chao kw kumuumbua n waziri, Mwana jamvi atakaye pata habari atujulishe!

Aina ya majibu yale yanatokana na uvivu wa kufanya kazi zao na kufikiri, so njia rahisi ni kujibu wanavyojisikia kusema lolote mbele ya bunge!
Na tena huwa hawaoni aibu kabisa..., wakichoka kusema la maana huwa wana msamiati wao wa
''SUNGURA WETU NI MDOGO BADO HAJAKUWA!!''
 
Back
Top Bottom