Ndugu wana JF kwanza kabisa poleni na majukumu. Shida yangu ni hii, mimi ni mwanaume, mwaka jana mwezi wa 12 nilikutana na mpenzi wangu humu jf, tukafanya mawasiliano tukafahamiana vizuri. Tukapanga siku ya kuonana, nikatoka Moshi kwenda Dar kuonana nae akanipokea vizuri sana. Alikuwa mzuri wa sura na kimtazamo alionekana kabisa kuwa tayari kwa maisha ya ndoa. Pia kwenye vigezo tulivyopeana kila mtu aliridhika na mwenzie. Kweli nilimpenda sana na yeye vivyo hivyo. Mwezi wa kwanza mwaka huu tulianza rasmi kuwa wachumba na tukapanga kwenda kutambulishana kwa wazazi. Siku moja katika ofisi niliyokuwa nafanyia kazi ilivamiwa na majambazi usiku, vikaibwa vitu vya ofisi ikiwemo check ya shilingi milioni 10, computer 2 na baadhi ya nyaraka za ofisi. Pia niliibiwa laptop yangu. Nakumbuka Siku hiyo jioni mimi nilikuwa wa mwisho kutoka ofisini kwani wenzangu walinitangulia. Hivyo kesi ikawa imeniangukia nikajikuta mimi na aliyekuwa mlinzi wa ofisi yetu tunapelekwa rumande. Tulikaa rumande kwa muda wa wiki mbili bila dhamana. Baadae nilitoka rumande kesi ikawa inaendelea, roho iliniuma sana kwa kuhusishwa na ujambazi. Wazazi wangu walichukia sana kwa kitendo hicho na waliona hakuna haja ya malumbano na mwenye ofisi wakaona waingilie kati na kuongea na mwenye ofisi na kumlipa gharama zote za vitu vilivyoibiwa isipokuwa nyaraka hazikupatikana. Kesi ikawa imeisha nikarudi nyumbani. Wakati haya yote yanatoke mpenzi wangu alikuwa hana taarifa kwani simu zangu zilizimwa na mdogo wangu niliekuwa naishi nae hadi nilipotoka rumande. Mpenzi wangu alinitafuta sana hadi akakata tamaa. Baada ya hayo yote nilimpigia mpenzi wangu kumweleza yaliyonitokea lakini hakuamini na aliniambia wazi kuwa namdanganya. Nilijaribu kumwelewesha akawa hanielewi. Baada ya kuona hivyo nilijikuta namuongelesha kwa hasira na ukali uliomfanya akakata mawasiliano. Hadi leo ninavyoandika simu yake haipatikani wala humu Jf simuoni tena. Nimejaribu kuPM lakini inaonekana alishabadisha ID yake. Ombi langu kama yuko humu jf namuomba anisamehe tuendelee na mahusiano yetu. Pia awe na imani tu kuwa ni kweli haya mambo yalinitokea kwani kuna kipindi nilimpa mdogo wangu cm akaongea nae lakini alidai kwa nini hakupewa taarifa wakati haya mambo yanatokea. Wana Jf nisaidieni nifanyeje ili nipate kuwasiliana na huyu mpenzi wangu niliempenda sana. Pia nilikiri kwa kumuomba samahani kwania nilijikuta niko mikononi mwa polisi ghafla. Asanteni!