kabiriga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 1,163
- 1,213
Kuwa na ujuzi au elimu Fulani ni taaluma iwe ya kusomea au kujifunza kwa mtu anayejua vizuri taaluma hiyo. Lakini kinyume na hayo utakuta watu wengi kuonekana au kujifanya wana taaluma ya computer, ingawa sio kweli!
Mtaani VIJANA wengi na ata watu wazima wakishanunua au kumilikishwa komputer iwe ya Mpakato au ya mezani wakajua kutumia baadhi ya mifumo na ata kujua kidogo kufunga na kufungua shehemu mojawapo ktk computer kwao ni tiketi ya kujifanya wanaujuzi wa computer.
Ujuzi ni kwenda mbali zaidi ya kumiliki au kumilikishwa chombo husika, utawasikia wakisema computer hii imeharibika kitu Fulani lakini ukihoji wadadavue kwa undani wanaishia kujing'ata au kutoa majibu yasiyo na mantiki ya kifani.
Kujua kufomati au kubadili mfumo mmojawapo katika computer yako haina maana unaijua computer, kwa Kila mtaalamu ujuzi ni kufanya kitu kwa sababu na sio KWA kuiga au kukopi wengine wanafanyaje bila kuzingatia sababu ya msingi ya mabadiliko ktk computer husika.
Kwa wale walovamia fani za watu wajitafakali waachane na kuwadanganya watu Kuwa ni wajuzi wa computer kwani wanaharibu komputer za watu wengine. Vinginevyo waende shule wajifunze computer ni pana na ina fulsa Kubwa ya ajira.
Mtaani VIJANA wengi na ata watu wazima wakishanunua au kumilikishwa komputer iwe ya Mpakato au ya mezani wakajua kutumia baadhi ya mifumo na ata kujua kidogo kufunga na kufungua shehemu mojawapo ktk computer kwao ni tiketi ya kujifanya wanaujuzi wa computer.
Ujuzi ni kwenda mbali zaidi ya kumiliki au kumilikishwa chombo husika, utawasikia wakisema computer hii imeharibika kitu Fulani lakini ukihoji wadadavue kwa undani wanaishia kujing'ata au kutoa majibu yasiyo na mantiki ya kifani.
Kujua kufomati au kubadili mfumo mmojawapo katika computer yako haina maana unaijua computer, kwa Kila mtaalamu ujuzi ni kufanya kitu kwa sababu na sio KWA kuiga au kukopi wengine wanafanyaje bila kuzingatia sababu ya msingi ya mabadiliko ktk computer husika.
Kwa wale walovamia fani za watu wajitafakali waachane na kuwadanganya watu Kuwa ni wajuzi wa computer kwani wanaharibu komputer za watu wengine. Vinginevyo waende shule wajifunze computer ni pana na ina fulsa Kubwa ya ajira.