Kila baraka ina laana ndani yake

Kila baraka ina laana ndani yake

Lakini akaja kumtamani mke wa mjakazi wake.... LAANA! na ili apate kummiliki kikamilifu nadhani alimfanyia mjakazi wake figisu mbaya

nilikuwa nataka nijue... hiyo HEKIMA aliyopewa.. ni ipi
Mkuu pamoja na hekima aliyopewa, ilifika mahali kale ka dhambi ka Asali kakaibuka na kumpelekea kufanya hayo aliyofanya.
 
Kwa muktadha wa mada na uhalisia wake (binadamu) chini ya mbingu hakuna mwanadamu mkamilifu la hata mmoja na kila mmoja wetu ana udhaifu wake.... Hivyo pamoja na hekima kuu aliyojaaliwa bado udhaifu wa kibinadamu haukumwepuka
Hakika mkuu, maana ukamilifu wa binadam si wa milele
 
Wengi huchukulia mafanikio ya kiuchumi kama baraka kubwa kuliko zote..
Kuna waliobarikiwa elimu lakini uchumi mbovu... Familia nzima imejaa wasomi tena wa kaliba mbalimbali lakini maisha yao hayaeleweki
Kuna waliojaaliwa watoto, yani kwao uzazi sio ishu... Wakigusa tu mtoto... Hii ni baraka, lakini maisha yao ni ya kuungaunga,
Kuna familia zimejaaliwa utajiri na ukwasi wa kutisha lakini kati yao hakuna upendo.. N roho mbaya mwanzo mwisho
Asili ya baraka na laana imo kwenye misahafu na ina historia ndefu huku kuliwa na mifano mingi.
Mfano mmojawapo maarufu sana ni mfano wa mfalme Suleiman... Mtu huyu katika mazungumzo yake na Mungu (kwa njia ya maono na unabii) aliulizwa anataka nini toka kwa Mwenyezi Mungu... Yeye akaomba hekima...! Wengi wetu leo hii wanaomba utajiri, tembelea yale makanisa ya kileo utaona...!
Mungu akampa mfalme Suleiman HEKIMA kama alivyoomba lakini akaongezewa na utajiri... Inasemekana mpaka leo hii hakuna aliyeweza kumfikia Suleiman kwa utajiri na ukwasi

Laana ndani ya baraka za Suleiman mfalme ni ipi?
Dhambi ya asili... Chini ya jua hakuna kiumbe mkamilifu la hata mmoja... Wote ni watenda dhambi na wamepungukiwa na utukufu wa MUNGU
Pale kati patamu.... Suleiman pamoja na hekima zote na utajiri uliotukuka lakini alikuwa dhaifu mno kwenye swala zima la masukubasi.. Inasemekana alikuwa na wake 300 wa ndoa na masuria (nyumba ndogo) idadi kama hiyo.. Ama pengine kuzidi.... Lakini akaja kumtamani mke wa mjakazi wake.... LAANA! na ili apate kummiliki kikamilifu nadhani alimfanyia mjakazi wake figisu mbaya

Zitumie vema baraka na vipawa vyako, usipotoke na kuanguka mazima... Makinika kila penye baraka kuna laana....
Mkuu Suleman alikuwa na wake 700 na masuria_maids 300 na aliyetamani mke wa mtumishi wake ni Daud,baba yake sele.ni hayo tu
 
Hujawahi kuniangusha pamoja na tofauti zetu kiimani, ndani ya intelligence tu wa moja... Ngoja nisake ushahidi nikiukosa nitasema nimeukosa
Daudi ndo alifanya figisu kwa mke wa jemedari wake hulia....

Ila msingi wa hoja yako umeeleweka
 
Asante sana mkuu. Huwezi pewa kila kitu, tukipewa kila kitu hatutakuwa na haja ya kitu chochote, na ikiwa hatutahitaji kitu chochote kutoka kwa yeyote tutamsahau hata aliye tupatia kila kitu.
 
Asante sana mkuu. Huwezi pewa kila kitu, tukipewa kila kitu hatutakuwa na haja ya kitu chochote, na ikiwa hatutahitaji kitu chochote kutoka kwa yeyote tutamsahau hata aliye tupatia kila kitu.
Neno la hekima
 
.
in-your-hands-lies-the-future-of-your-world-and-the-fulfilment-of-the-best-qualities-of-your-...jpeg


Jr
 
Umenena !! Ni kama umenipiga nyundo kwani hayo maisha nayashuhudia . Mmoja kapanda chati ila tunapukutika mmoja baada ya mwingine .Wazee wanasema ni kazi ya Mungu kumbe ni shetani . Tufanyeje na hawa wanaosababisha majanga katika jamii ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hatuna cha kuwafanya asili inachukua mkondo wake.. Nasi tuna mapungufu yetu japo hayazidi yao
Umenena !! Ni kama umenipiga nyundo kwani hayo maisha nayashuhudia . Mmoja kapanda chati ila tunapukutika mmoja baada ya mwingine .Wazee wanasema ni kazi ya Mungu kumbe ni shetani . Tufanyeje na hawa wanaosababisha majanga katika jamii ?

Sent using Jamii Forums mobile app

Jr
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom