hakuna kazi ngumu kama ya kuwaongoza wanaadamu, hakuna nabii ambae hakupata shida katika kutangaza neno la mungu, mwanaadamu siku zote anapoona umemzidi huangalia kasoro zako ili akukosowe, ijapokuwa kile ambacho anachokipata kutoka kwa aliemzidi ni kikubwa kuliko kuangalia udhaifu, ndio wengine wajifanyao wajanja na hawataki kuona kuwa binaadamu wako tofauti na wamezidiana hubuni njia tofauti za kujitetea, leo hii utasikia kama kuna makosa basi tujifunze kutokana na makosa, huwezi kuendelea au kupiga hatua yoyote kama utafuata methali hii, mungu alivyowachagua watu ambao watafikisha neno lake miongoni mwa wanaadamu hakuwaumba tofauti, aliwaumba wakiwa ni wanaadamu kama tulivyo sisi, wanamapungufu ya kiubinaadamu kama tulivyo sisi, sisi tunaumwa na wao wanaumwa, sisi tunakula na wao wanakula, na mengi mengimeyo, hawakuwa malaika leo hii ukimuangalia nabii mussa alikuwa na kasoro ya kimaumbile katika lafidhi yake, alikuwa hayapati vizuri maneno, na ndio maana kuna dua alikuwa akiomba kila siku ( rabbi-shrahlii swadrii, wayassirly amri, wahlul-uqdata min lisaanii, wajaally waziira min ahly, yafqahuu qaulii) alikuwa akiomba mungu amjaalie na uwezo wa kupata lafudhi nzuri mbele ya umma wake na akaomba amjaalie msaidizi katika jamaa zake na ndio maana mungu akamteulia haroun kuwa msaidizi wake, hii ni dua tangu nabii mussa mpaka leo hii waislamu huisoma hasa kwa masheikh wanaotangaza neno la mungu, sasa ukisema unataka kumtoa kasoro nabii mussa kwa kutokuwa na lafudhi nzuri kuliko wewe ukajiona wewe ni bora kuliko yeye, jaribu kwanza kuangalia historia yake, asili ya nabii mussa kukosa lafudhi nzuri ni kutokana siku aliotafuna kaa la moto, mussa baada ya kufikishwa kwenye kasri la firauni, ikumbukwe tayari firauni alishatoa amri kila mtoto wa kiume atakaezaliwa auwawe, eti kisa aliota ndoto kuna mtoto atazaliwa na kuja kuupindua utawala wake, na firauni kama ilivyo kwa watoto wengine aliowauwa na mussa pia hakuaminika mbele ya firauni, ndipo alipotoa rai ya kujaribiwa kama kweli anayo akili inayoweza kuwa sababu ya yeye kuja kumpindua, liliwekwa kaa la moto na tende, nabii mussa aliekewa mbele yake achague, na kwasababu alikuwa mtoto hakuwa na akili hiyo, alitaka kuchaguwa tende lakini ghafla mwenyezi mungu akamteremsha malaika wake jibril akaukwepesha mkono na kuupeleka kwenye kaa la moto, halikuwa chaguo la mussa lilikuwa chaguo la mungu, kaa la moto lilikuwa na madhara makubwa kwake lakini hiyo ni mipango ya mungu, ni binaadamu wachache sana wenye uthubutu ya kujishusha mbele ya wengine, hata kama wamezidiwa vipi na siku zote asiekubali kushindwa si mshindani ni bepari.