Kila baraka ina laana ndani yake

Kila baraka ina laana ndani yake

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
361,189
Reaction score
832,001
Wengi huchukulia mafanikio ya kiuchumi kama baraka kubwa kuliko zote..
Kuna waliobarikiwa elimu lakini uchumi mbovu... Familia nzima imejaa wasomi tena wa kaliba mbalimbali lakini maisha yao hayaeleweki
Kuna waliojaaliwa watoto, yani kwao uzazi sio ishu... Wakigusa tu mtoto... Hii ni baraka, lakini maisha yao ni ya kuungaunga,
Kuna familia zimejaaliwa utajiri na ukwasi wa kutisha lakini kati yao hakuna upendo.. N roho mbaya mwanzo mwisho
Asili ya baraka na laana imo kwenye misahafu na ina historia ndefu huku kuliwa na mifano mingi.
Mfano mmojawapo maarufu sana ni mfano wa mfalme Suleiman... Mtu huyu katika mazungumzo yake na Mungu (kwa njia ya maono na unabii) aliulizwa anataka nini toka kwa Mwenyezi Mungu... Yeye akaomba hekima...! Wengi wetu leo hii wanaomba utajiri, tembelea yale makanisa ya kileo utaona...!
Mungu akampa mfalme Suleiman HEKIMA kama alivyoomba lakini akaongezewa na utajiri... Inasemekana mpaka leo hii hakuna aliyeweza kumfikia Suleiman kwa utajiri na ukwasi

Laana ndani ya baraka za Suleiman mfalme ni ipi?
Dhambi ya asili... Chini ya jua hakuna kiumbe mkamilifu la hata mmoja... Wote ni watenda dhambi na wamepungukiwa na utukufu wa MUNGU
Pale kati patamu.... Suleiman pamoja na hekima zote na utajiri uliotukuka lakini alikuwa dhaifu mno kwenye swala zima la masukubasi.. Inasemekana alikuwa na wake 300 wa ndoa na masuria (nyumba ndogo) idadi kama hiyo.. Ama pengine kuzidi.... Lakini akaja kumtamani mke wa mjakazi wake.... LAANA! na ili apate kummiliki kikamilifu nadhani alimfanyia mjakazi wake figisu mbaya

Zitumie vema baraka na vipawa vyako, usipotoke na kuanguka mazima... Makinika kila penye baraka kuna laana....
 
Tatizo tukiwa tunataka kitu humuomba Mungu na tukishapata hapo humsahau Mungu. Laiti wakati Mungu kishatupa tulilo muomba na kuendelea kuomba viwe na heri nasi angetukinga na laana.


Ndukiiiii🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
mshana mimi nitakuwa tofauti kidogo na wewe, iwe unayosema wewe baraka au jaha, lakini kuna vitu ambavyo mungu anampa mtu yoyote na kuna vitu ni kwa ajili ya watu maalumu aliowateuwa, hatuwezi kusema leo kwa sababu mungu alimpa yesu au mussa utume, tukafikiria mtu yeyote anaweza kuwa mtume, labda hawa mitume wetu wakufoji na manabii uchwara, kama mungu kampa nguvu mmasai ya kuuwa simba, ni kichekesho kilioje kwa wewe mpare au muhaya ukakute simba kauliwa na mmasai ukajipaka damu na kusema na wewe ni shujaa, hapo lazima wanaofahamu ishu ilivyo wakucheke sijui wewe mwenyewe unajionaje pale watu wanaofahamu mchezo mzima wakisimama mbele yako na kukupigia makofi utahisi wanakupongeza au wanakucheka?.
Pili mungu kumbariki mja wake jaha au baraka kama usemavyo kuna laana nyuma yake hii si sahihi, kwa sababu chochote anachokupa mungu kinaweza kuwa mtihani kwako, lakini pia ni kawaida ya roho za kibinaadamu kuonelea husda pale mungu anavyomfaidisha katika rehma zake mmoja wetu, lakini pia mungu siku zote akikupa kilema hukupa na mwendo, ni muhimu sana watu kuelewa mwenyezi mungu anapoamua kuleta rehma kwa waja wake na akamchagua mmoja wetu kuwa ndio rehma hiyo ipitie kwake, basi hata binaadamu ufanye vipi kama mungu kaamua rehma hiyo iwafikie waja wake itawafikia kwa sababu binaadamu hawezi kushindana na rehma na uwezo wa mungu, mwisho wa siku ukilaani laana itakufikia mwenyewe, kushindana na uwezo na utukufu wa mungu katika kuumba kwake na kuvitukuza vyengine dhidi ya vyengine ni sawa na kushindana na aliekuumba.
 
mshana mimi nitakuwa tofauti kidogo na wewe, iwe unayosema wewe baraka au jaha, lakini kuna vitu ambavyo mungu anampa mtu yoyote na kuna vitu ni kwa ajili ya watu maalumu aliowateuwa, hatuwezi kusema leo kwa sababu mungu alimpa yesu au mussa utume, tukafikiria mtu yeyote anaweza kuwa mtume, labda hawa mitume wetu wakufoji na manabii uchwara, kama mungu kampa nguvu mmasai ya kuuwa simba, ni kichekesho kilioje kwa wewe mpare au muhaya ukakute simba kauliwa na mmasai ukajipaka damu na kusema na wewe ni shujaa, hapo lazima wanaofahamu ishu ilivyo wakucheke sijui wewe mwenyewe unajionaje pale watu wanaofahamu mchezo mzima wakisimama mbele yako na kukupigia makofi utahisi wanakupongeza au wanakucheka?.
Pili mungu kumbariki mja wake jaha au baraka kama usemavyo kuna laana nyuma yake hii si sahihi, kwa sababu chochote anachokupa mungu kinaweza kuwa mtihani kwako, lakini pia ni kawaida ya roho za kibinaadamu kuonelea husda pale mungu anavyomfaidisha katika rehma zake mmoja wetu, lakini pia mungu siku zote akikupa kilema hukupa na mwendo, ni muhimu sana watu kuelewa mwenyezi mungu anapoamua kuleta rehma kwa waja wake na akamchagua mmoja wetu kuwa ndio rehma hiyo ipitie kwake, basi hata binaadamu ufanye vipi kama mungu kaamua rehma hiyo iwafikie waja wake itawafikia kwa sababu binaadamu hawezi kushindana na rehma na uwezo wa mungu, mwisho wa siku ukilaani laana itakufikia mwenyewe, kushindana na uwezo na utukufu wa mungu katika kuumba kwake na kuvitukuza vyengine dhidi ya vyengine ni sawa na kushindana na aliekuumba.
Asante kwa ufafanuzi na maelezo ya ziada pia.... Nimekusoma vizuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom