Kikwete's most embarassing statements...

Kikwete's most embarassing statements...

..........duuuuu, inatosha

Mbona ndio mwanzo tu game imeanza. Kina January Makamba na wenzake huko ikulu inabidi waeleze ni wapi walikuwa na nini walikuwa wanafanya wakati Kikwete akijionyesha utupu wake kwa watanzania.
 
nakuelewa, kusema ukweli anatia huruma kweli baba wa watu. sijui baada ya kujikanyaga mpaka kutoa vidole na kutema pumba zoote hizo mbele ya kadamnasi huwa anajisikiaje, ningekuwa mimi ningekuwa nakosa usingizi,
na akienda nje afadhali wamshauri awe anaongea kiswahili halafu kunakuwa na mkalimani...


Duh!
Ila jamaa anajitahidi sana kutoa kauli mkanganyiko.
Hivi huwa hana watu ambao wanamshauri cha kuongea mbeke ya kadamnasi?
 
Duh!
Ila jamaa anajitahidi sana kutoa kauli mkanganyiko.
Hivi huwa hana watu ambao wanamshauri cha kuongea mbeke ya kadamnasi?

aisee jamaa akicheza anaweza kuifikia record ya mzee Kenyatta hapo kwa watani zetu...
 
Ila kusema kweli, viongozi wetu wanahitaji kuwa 'serious' mara nyingine, hasa pale hotuba inapolenga wananchi (masikini), kwani kwao u 'seriousness' unaweza kuwafuta jasho...hata kama hawatarajii mabadiliko makubwa sana!
Franki
 
aisee jamaa akicheza anaweza kuifikia record ya mzee Kenyatta hapo kwa watani zetu...

Sure!
Mwingine mwenye kauli chafu sana ambaye alistahili kuwa katika kitabu cha Kumbukumbu ya Guinness ni mshitakiwa Basili Pesa2 Mramba!
Sijapata kusikia mtu mwenye kauli chafu kama mzee huyu, hasa katika utawala wa awamu ya tatu!
 
Mpaka sasa huwa najiuliza kwa nini huyu jamaa aliutaka sana urais. Ingawa pia nafahamu kuwa watu kama akina Rostam ambao walitaka huyu awe rais kuliko hata yeye mwenyewe alivyotaka. Tangu mwanzo niliwaonya watu washimshabikie huyu mtu kwa sababu nilijua hana uwezo, ni mswahili tu. Laiti Mwalimu angekuwa bado hai angalao mpaka 2005 bila shaka angetuepushia 'kikombe' hiki.
 
Huyu alishindwa kabla hajaanza hata huo urais! Ujasiri ni pale mtu unapoweza kujigundua kuwa kuna mambo mengine huwezi, inawezekana kuna mambo anayaweza kwa ufasaha kabisa, lakini hili la Urais angesema jamani inatosha, mnisamehe!


Huo ndio ukweli. Nitashangaa sana akiomba second term. Huyu anapaswa kukaa pembeni, imetosha! Miaka mingine mitano hapana, jamani. Tunataka mtu mwenye sifa zinazostahili, sio mswahili asiye na agenda yoyote katika kuipeleka nchi kwenye mafanikio.
 
Laiti Mwalimu angekuwa bado hai angalao mpaka 2005 bila shaka angetuepushia 'kikombe' hiki.

Braza Punch,
Ndo tushauvaa mkenge hivyo, kikombe tunakistahili kabisa, kwa miaka hii mitano! Ila mwakani nitapiga kura, ila simpi yeye, hata akishinda nitakuwa uhakika kuwa hakushinda kwa kura yangu!



Huo ndio ukweli. Nitashangaa sana akiomba second term.

Utashangaaje ilhali mwamuzi wa kugombea ama kutogombea si yeye?
Kuna watu wanamwamulia, iwapo agombee ama la, na huwa anawasikiliza sana!
Watanzania tunajutia sana kumpa kura mtu huyu, asiyejua kuwa kwa nini nchi anayoiongoza ni maskini hadi sasa!
 
mara nyingi kikwete akizungumza huwa sometimes nafeel embarased

top three ya mazungumzo ya kikwete yaliyo ni disappoint ni hii

1. Alienda Mwanza mara baada ya kuchaguliwa kuwa rais alizungumza mengi lakini mwisho alisema namnukuu "Wananchi wa Mwanza nataka kulibadilisha hili jiji lenu liwe kama Carlifornia" na hii ilikuwa hadharani kwenye uwanja wa CCM Kirumba.

2. Akifanya mkutano wa waandishi wa habari mwanzoni kabisa, kuna mwandishi mmoja wa kike alimuuliza swali kuhusu nchi kurusu bidhaa duni kuingia na uhai wa manufacturing industry, yeye alijibu huku akijionyesha mtoto wa mjini anaejua mavazi, akaanza kutaja labels za nguo, na mwisho akasema kwa kuwa sio wote wanamudu nguo mpya, basi ruksa watu kuingiza nguo duni

3. HII ilikuwa ile hotuba yake maarufu ya bungeni, watu nchi nzima tunasubiri ripoti ya EPA ataizungumziaje, yeye akatumia muda mwingi kuchekesha watu, top ilikuwa pale aliposema "Kula uliwe"

wewe upo kama mimi.......sijui ni lini watanzania tutabadilika
 
Lakini hata Mwalimu aliwahi kuuambia mkutano wa akina mama kwamba "uchumi wanao, wameukalia"! Na mzee Mwinyi aliwahi kuuongelea "ukuni" mmoja hauvishi chakula.
 
Ni pale aliposema " Kelele za mpanagaji hazimnyimi mwenye nyumba kupata usingizi" pale wapinzani walipokuwa wanapiga kelele kuhusu ufisadi.
 
Hata hivyo, amesema tatizo hilo halikutokana na uzembe wa mtu yeyote, bali ni mitihani ya Mwenyezi Mungu.

Oct 2006 JK
 
Mimi kilichoniboa ni pale alipodai kuwa hajui kwa nini TZ ni maskini na kabla hata ya kupata jibu la swali hilo ameendeleza umatonya toka nchi za nje mtindo mmoja! Wakati mwenzake Mkapa anasikitika kuhusu matokeo mabaya ya ubinafshaji alioupigia debe wakati wa utawala wake JK anazunguka nchi mbalimbali kutafuta wezi kwa mgongo wa "uwekezaji."

nakubaliana na wewe mkuu Buchanan, huyu bwana mimi alinimaliza kabisa aliposema kuwa haelewi sababu kwanini nchi yake ni maskini tena anazungumza mambo haya akiwa ughaibuni kwenye nchi za watu!! Kila siku toka enzi za Mussa nchi hii tunaimba kuwa tuna maadui wakuu watatu na mmoja wao ni umaskini; kwahiyo mtu unatagemea yeyote atakayeusaka urais wa nchi yetu kazi yake kubwa ni kutafuta jinsi ya kupambana na maadui hawa na huwezi kumshinda adiu bila kumjua na kutafuta mbinu za kumshinda. Inaelekea Jakaya aliusaka urais bila ya kujua akiupata ataufanyia nini zaiadi ya uVASCO DAGAMA!
 
Ni pale aliposema " Kelele za mpanagaji hazimnyimi mwenye nyumba kupata usingizi" pale wapinzani walipokuwa wanapiga kelele kuhusu ufisadi.

Alikuwa anadanganya tu .... kelele zimemnyima usingizi hadi anakimbilia nchi za nje kila kukicha!
 
Kali nyingi ya mheshimiwa raisi hii hapa!

JK: Vumilieni shida


na Anna Makange, Tanga


RAIS Jakaya Kikwete, amewataka Watanzania kuwa wavumilivu kutokana na hali ngumu ya maisha inayowakabili kwa sasa, inayosababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta duniani.
Rais Kikwete ametoa kauli hiyo katika kipindi ambacho Watanzania wengi, hasa wa kipato cha chini wamekuwa wakilia kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.
Rais Kikwete alitoa kauli hiyo jana, wilayani Muheza, wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo, ikiwa ni siku ya tisa ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo, mkoani Tanga.
Rais Kikwete alisema kupanda kwa bei ya mafuta, kumechangia kwa kiasi kikubwa kulipuka kwa mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali duniani kote.
Alisema hali hiyo pia imechangia kuzorotesha kasi ya ukuaji wa uchumi hasa kwenye nchi zinazoendelea na hivyo watu wenye kipato duni kukabiliwa na hali ngumu ya maisha, hususan katika upatikanaji wa mahitaji muhimu, jambo ambalo aliongeza kuwa hata yeye limekuwa likimuumiza kichwa.
“Ndugu zangu Watanzania wenzangu…naelewa sana jinsi maisha yanavyozidi kuwa magumu siku hadi siku…na hali hii inasababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta hapa nchini, hivyo kila bidhaa kwa sasa gharama zake ni za juu sana, kuanzia vyakula hadi vitu vingine ambavyo ni muhimu kwa maisha ya kila siku. Linatuumiza sana hasa wale wananchi ambao ni maskini wa kipato,” alisema Rais Kikwete.
Hata hivyo alisema Watanzania wasikate tamaa kwa kuona kwamba maisha yataendelea kuwa hivyo, na kusisitiza kwamba yeye kama Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali duniani wanalishughulikia suala hilo.
Wakati Rais Kikwete akiwataka Watanzania kutokatishwa tamaa na hali hiyo, Chama cha NCCR- Mageuzi, jana kilisema wananchi hawana sababu ya kuilaumu Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) kwa kupandisha bei ya nauli na badala yake lawama hizo zielekezwe kwa serikali ya Rais Kikwete.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni, Kampeni na Uchaguzi, Faustine Sungura, alisema kutokana na matatizo hayo, kuna haja ya kuwepo kwa serikali mbadala, kwa madai kuwa serikali imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi, hasa ya upandaji wa gharama za bidhaa mbalimbali.
“Watanzania wanapaswa kujifunza kutokana na makosa, kwani muda waliowapa viongozi wa CCM kutawala unatosha na haujaonyesha mafanikio yoyote katika maisha zaidi ya kuzidisha ugumu wa maisha,” alisema.
“Watu wanakosea sana wanapoilaumu Sumatra badala ya kuilaumu serikali ambayo imeshindwa kudhibiti upandaji wa bei kwenye bidhaa mbalimbali yakiwemo mafuta,” alisema Sungura.
Alisema hata ziara anazofanya Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake, Ali Mohamed Shein ni dhihaka kwa Watanzania, kwani ahadi zao hazitekelezeki na wameshindwa kuwasaidia wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao wanashinda Ikulu.
“Hivi hawa ni viongozi wa aina gani kama wameshindwa kuwasaidia wazee wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaoshinda pale Ikulu, wataweza vipi kuwasaidia watu wa huko mikoani?” alihoji Sungura.
Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amesema serikali itahakikisha inafanya kila jitihada za kutafuta wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuwekeza kwenye kiwanda cha usindikaji wa matunda wilayani Muheza, kwa lengo la kuwatafutia wakulima wa machungwa soko la uhakika.
Alisema lengo la kujenga kiwanda hicho licha ya kumtafutia soko mkulima, lakini pia itakuza kipato cha wakulima sambamba na kupunguza kiwango kikubwa cha machungwa yanayoharibika mashambani kwa kukosa wanunuzi hasa nyakati za msimu.
“Serikali inaamini kwa kufanya hivi tutakuwa tumemsaidia mkulima kwa kiasi kikubwa kuwa na soko la uhakika sambamba na kukuza kipato chake ambacho hivi sasa kinapotea kutokana na kiasi kikubwa cha matunda kuharibika…nawaahidi kwamba hili tutalitekeleza haraka iwezekanavyo,” alisisitiza Rais Kikwete.
Miongoni mwa ahadi alizotoa rais wilayani Muheza ni pamoja na kupeleka darubini katika zahanati ya Kijiji cha Kicheba, kuchangia sh milioni mbili katika ujenzi wa madarasa ya Shule ya Sekondari ya Mtindiro, sambamba na kutafuta magari ya wagonjwa katika wilaya zilizokosa huduma hiyo mkoani hapa.


Chanzo: Tanzania Daima, 21/7/2008

Mjadala uendelee
 
Na pale aliposema anawajua wala RUSHWA akawapa muda wajirekebishe je?
 
Back
Top Bottom