Miaka miwili iliyobaki inahitaji commanding/order nzito kama hii vinginevyo tutaendelea kulaumiana huko mambo yanaharibika.Binafsi nilitegemea kauli kama hii kutoka kwa mh. Rais,hii inadhihilisha jinsi gani raisi wetu anavyoweza kufanya maamuzi magumu yasiyo na chembe ya unafiki wala uoga kwa taifa.
Nitoe rai kwa wale wote ambao wao suala la Gesi wanaona ni dili lao kisiasa,hili sio dili ni balaa kubwa wanatafuta maana kuna mambo mengi ya msingi wamesahau kuyafanya ikiwa ni pamoja na,
1.Kujenga vyama vyao kimkakati kuelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
2.Kujenga uwezo wa ndani wa vyama vyao kukabiliana na mamluki wanaovivuruga vyama vyao.
3.Kutanua wigo wa uongozi na matumizi ya fedha ndani ya vyama vyao.
4.Kutafuta njia iliyo bora kuona jinsi gani vyama hivyo vinakuja na nguvu mpya ya kuungana na kupata chama kimoja chenye nguvu na ushawishi kwa wananchi tofauti ilivyo sasa.
5.Kuacha kuwasumbua wananchi ambao maisha kwao bado yataendelea kuwa magumu tu hata kama Gesi hiyo itabaki kwao.
6.Kuwatumia wataalamu walionao/ama kuwatumia wale waliopo katika masuala muhimu kama haya kwani kwa kufanya hivyo kutawapatia wataalamu wetu nafasi ya kutumia vibaji vyao kuwaeleza wananchi ukweli.
7.Vyama kuondoa dhana potofu kwamba eti siasa ni kwa wanasiasa na si wataalamu,vyama vijenge tabia ya kufanya consultation kwa wataalamu kabla ya kutafuta nguvu ya umma.
Vyama kwa kutokufanya hivyo navyo vitaonekana kama ni sehemu mojawapo ya dili la mtu/watu na si kwa maslai ya taifa.
Chama bora ni kile tu amabacho msingi wake uko katika kujenga nchi hata kama ni polepole maana haraka haraka haina baraka.
Napenda kuviomba vyama vya siasa na wadau wengine kuwa msingi mkuu wa Rasilimali za Taifa ni AMANI.AMANI Ikitoweka sidhani kama kuna yeyote kati yetu atakayethubutu kuzungumzia Rasilimali hizo akiwa Ukimbizini,mifano tunayo sema tu tunajisahaulisha kwa makusudi.
La mwisho ni kuwaomba ndugu zangu tupende kumheshimu Rais wetu hata kama hatumpendi,lakini heshima ni kitu kikubwa sana na kama alikwisha kukosea msamehe tu na umuachie mwenyezi Mungu.Tofauti za vyama zisitufanye kukosa adabu kwa Mkuu kama huyu na kwa wale ambao wana tabia ya kumkebehi,kimdharau na kumsema hovyo bila sababu waache tabia hizo kila mtu na atimize wajibu wake.
Asanteni.